Kampuni ya magari BYD kutumia DeepSeek AI katika magari yake kuboresha ADAS!

Kampuni ya magari BYD kutumia DeepSeek AI katika magari yake kuboresha ADAS!

Ushuru wake unafahamika.

Mie nilivusha Dolphin ya 30 kWh kutoka Nairobi.

Ushuru pekee nilitoboka 98,650,000/=
mmmh.! ya kweli haya basi ni us*ng* wa hali ya juu yaani injinia wenye viwanda wametengeneza gari zuri hadi kukusafirishia wamekuchaji labda milion 30 tu lakini hawa TRA wanachaji mara mbili hadi tatu ya aliyetengeneza hiyo gari..hivi huu wizi wa ushuru hapa kwetu asili ni ipi hasa.! hawa tra hata siku wajapani wakileta kiwanda cha magari tanzania bila aibu wataendelea kuchaji kodi zao hizi hizi za ajabu.
 
Ushuru wake unafahamika.

Mie nilivusha Dolphin ya 30 kWh kutoka Nairobi.

Ushuru pekee nilitoboka 98,650,000/=
Sio mchezo aisee..ushuru mkubwa kuliko ma-fortuner, ma -hilux..

Kwa hiyo jumla kabisa ushuru na manunuzi iligharimu shilingi ngapi?
 
Inakuja na options mbili za battery, either 30 kWh (hii inaenda 300km) au 38 kWh (hii inaenda 400km), zote teknolojia ya LFP (Lithium Iron Phosphate).

Kwasababu ya size yake, ni very efficiency, inaenda 11 km/kWh (yaani inaenda km 11 kwa unit moja ya umeme).

Ina support DC fast charging kwa dk 30, lakini kwa umeme wa nyumbani (120V) ambao ni Level I charging, utatumia masaa 12-18 kuchaji kutoka 0% hadi 100%.

Challenge ya BYD Seagull itabidi uagize kutoka China maana kwa sasa ni exclusive kwa China tu, kwa international itabidi uende na BYD Dolphin, hii ata Kenya ipo (maana Kenya kuna BYD official branch).

Hii Dolphin unapata hapo Kenya 0km full box kwa Million 20 tu za Kitanzania, toa ushuru.

View attachment 3236031
Ni ishu ya mapendeleo ila hala uwa nakaona kazuri zaidi nje na ndani.
View attachment 3236032
Hii Dolphin yenyewe inakuja na options tatu za battery, ndogo kabisa ni 30kWh, inakuja 40kWh na kubwa ni kama performance version inakuja na 60kWh, pia ni LFP battery.
View attachment 3236033
Hiyo battery ndogo ya 30kWh inakupa range ya 300km, ndio base model, na ina power ya 94hp.

Battery ya 40kWh inakupa range ya kilometa 400 na power ya 170 hp.

Na battery kubwa la 60kWh badala ya kufocus kwenye range wamepeleka kwenye performance, linakupa range ya 430km ila power kubwa ya 200+ hp.
Changamoto kodi yake sijui itakuwa imesimamaje.
Nilikaona ka bmw i3, aisee tra calculator walichoniletea nikasonya na kutukana
 
Changamoto kodi yake sijui itakuwa imesimamaje.
Nilikaona ka bmw i3, aisee tra calculator walichoniletea nikasonya na kutukana
Achana na hawa TRA. Ujanja kuchukua gari kama IT Congo, unalisajili uko DRC uku unakuja nalo na permit ya 6 months ya kutumika Bongo. Kama Nenga.
 
Achana na hawa TRA. Ujanja kuchukua gari kama IT Congo, unalisajili uko DRC uku unakuja nalo na permit ya 6 months ya kutumika Bongo. Kama Nenga.
Kisha baada ya miezi 6 inakuwaje?

Mchakato wa kusajili huko congo na the rest nakuwa nasave kiasi gani?
 
Back
Top Bottom