Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
Utu ni jambo muhimu sana kwenye huu uumbaji wa Mwenyezi Mungu
Kampuni ya mikopo midogomidogo ya OYA si kampuni rafiki na yenye UTU kwa wakopaji wake. Pamoja na kuwa na vibali halali vya kuendesha hiyo biashara lakini matendo ya wafanyakazi wake kwa wakopaji wanaoshindwa kurejesha kwa wakati yanatia shaka nia ya kuwasaidia watu.
Kuna ukatili mkubwa unyanyasaji, uonevu nk kwa wateja wao. Kwa kifupi wanaogopeka kuliko polisi.. Mbaya zaidi pesa zao ni kama zina laana hazilipiki ukikopa.
Nyakati za Kikwete iliibuka kampuni ya udalali ya MAJEMBE halafu ikapata kazi za serikali za kukamata wadaiwa na wrong parking.. Hakuna rangi wananchi wenye ishu za kikodi na wrong parking walipokutana na wafanyakazi wa MAJEMBE.
Mimi ni mhanga wao.. Walikamata gari yangu wakati kesi iko TRA 2014.. Gari ilikuja kupigwa mnada mwaka 2021 Majembe ikiwa tayari ni Marehemu kwenye biashara.
Nini kiliwapata?
Walikamata gari ndogo ya Professor wa chuo kikuu UDSM maeneo ya Magomeni wakidai alipoegesha ni wrong parking.. Prof akawaomba wamuoneshe alama inayoonesha NO PARKING lakini wakaleta ubabe na kuivuta gari mpaka kwenye maegesho yao mpaka prof alipe faini.
Prof. Akakimbilia mahakamani.. Majembe wakiwa wamepewa kazi ya wrong parking na manispaa ya Kinondoni wakati huo na wenye nguvu serikalini wakaisumbua sana mahakama. Prof. Akawa ana 'document' kila gharama anayotumia kwa kukosa kutumia gari yake.
Mwisho wa siku Gharama zikawa ni zaidi ya BILLION MOJA na utawala wa JK ukawa umefikia mwisho.. Hapo nyuma Prof alishashinda kesi maranyingi tu lakini kulipwa ilikuwa shughuli pevu. Baada ya Magufuli kuingia tu jumba jeupe.. Prof akarudi mahakamani kukazia hukumu.
Majembe sasa wakiwa hawana mbeleko tena.. Wakaamriwa walipe maramoja na wakishindwa mali zao zikamatwe zipigwe mnada.. Walipewa siku 14 kisha wakaongezewa saba jumla siku 21.
Muda ukaisha bila kulipa hata thumni.. Mali zao zikakamatwa na kupigwa mnada.. Mojawapo ilikuwa godown kubwa kona ya kwenda Cocacola pale Mwenge.
Soma Pia:
Kampuni ya mikopo midogomidogo ya OYA si kampuni rafiki na yenye UTU kwa wakopaji wake. Pamoja na kuwa na vibali halali vya kuendesha hiyo biashara lakini matendo ya wafanyakazi wake kwa wakopaji wanaoshindwa kurejesha kwa wakati yanatia shaka nia ya kuwasaidia watu.
Kuna ukatili mkubwa unyanyasaji, uonevu nk kwa wateja wao. Kwa kifupi wanaogopeka kuliko polisi.. Mbaya zaidi pesa zao ni kama zina laana hazilipiki ukikopa.
Nyakati za Kikwete iliibuka kampuni ya udalali ya MAJEMBE halafu ikapata kazi za serikali za kukamata wadaiwa na wrong parking.. Hakuna rangi wananchi wenye ishu za kikodi na wrong parking walipokutana na wafanyakazi wa MAJEMBE.
Mimi ni mhanga wao.. Walikamata gari yangu wakati kesi iko TRA 2014.. Gari ilikuja kupigwa mnada mwaka 2021 Majembe ikiwa tayari ni Marehemu kwenye biashara.
Nini kiliwapata?
Walikamata gari ndogo ya Professor wa chuo kikuu UDSM maeneo ya Magomeni wakidai alipoegesha ni wrong parking.. Prof akawaomba wamuoneshe alama inayoonesha NO PARKING lakini wakaleta ubabe na kuivuta gari mpaka kwenye maegesho yao mpaka prof alipe faini.
Prof. Akakimbilia mahakamani.. Majembe wakiwa wamepewa kazi ya wrong parking na manispaa ya Kinondoni wakati huo na wenye nguvu serikalini wakaisumbua sana mahakama. Prof. Akawa ana 'document' kila gharama anayotumia kwa kukosa kutumia gari yake.
Mwisho wa siku Gharama zikawa ni zaidi ya BILLION MOJA na utawala wa JK ukawa umefikia mwisho.. Hapo nyuma Prof alishashinda kesi maranyingi tu lakini kulipwa ilikuwa shughuli pevu. Baada ya Magufuli kuingia tu jumba jeupe.. Prof akarudi mahakamani kukazia hukumu.
Majembe sasa wakiwa hawana mbeleko tena.. Wakaamriwa walipe maramoja na wakishindwa mali zao zikamatwe zipigwe mnada.. Walipewa siku 14 kisha wakaongezewa saba jumla siku 21.
Muda ukaisha bila kulipa hata thumni.. Mali zao zikakamatwa na kupigwa mnada.. Mojawapo ilikuwa godown kubwa kona ya kwenda Cocacola pale Mwenge.
Soma Pia:
- Mke wa Juma aliyepigwa na Wafanyakazi wa 'OYA' aeleza alivyokopa
- Pwani: Wafanyakazi wa kampuni ya mikopo ya OYA, mbaroni kwa tuhuma za mauaji