Kampuni ya mikopo ya OYA itakuwa na mwisho mbaya sana kama ilivyokuwa kampuni ya udalali ya MAJEMBE

Kampuni ya mikopo ya OYA itakuwa na mwisho mbaya sana kama ilivyokuwa kampuni ya udalali ya MAJEMBE

Utu ni jambo muhimu sana kwenye huu uumbaji wa Mwenyezi Mungu

Kampuni ya mikopo midogomidogo ya OYA si kampuni rafiki na yenye UTU kwa wakopaji wake. Pamoja na kuwa na vibali halali vya kuendesha hiyo biashara lakini matendo ya wafanyakazi wake kwa wakopaji wanaoshindwa kurejesha kwa wakati yanatia shaka nia ya kuwasaidia watu.

Kuna ukatili mkubwa unyanyasaji, uonevu nk kwa wateja wao. Kwa kifupi wanaogopeka kuliko polisi.. Mbaya zaidi pesa zao ni kama zina laana hazilipiki ukikopa.

Nyakati za Kikwete iliibuka kampuni ya udalali ya MAJEMBE halafu ikapata kazi za serikali za kukamata wadaiwa na wrong parking.. Hakuna rangi wananchi wenye ishu za kikodi na wrong parking walipokutana na wafanyakazi wa MAJEMBE.

Mimi ni mhanga wao.. Walikamata gari yangu wakati kesi iko TRA 2014.. Gari ilikuja kupigwa mnada mwaka 2021 Majembe ikiwa tayari ni Marehemu kwenye biashara.

Nini kiliwapata?

Walikamata gari ndogo ya Professor wa chuo kikuu UDSM maeneo ya Magomeni wakidai alipoegesha ni wrong parking.. Prof akawaomba wamuoneshe alama inayoonesha NO PARKING lakini wakaleta ubabe na kuivuta gari mpaka kwenye maegesho yao mpaka prof alipe faini.

Prof. Akakimbilia mahakamani.. Majembe wakiwa wamepewa kazi ya wrong parking na manispaa ya Kinondoni wakati huo na wenye nguvu serikalini wakaisumbua sana mahakama. Prof. Akawa ana 'document' kila gharama anayotumia kwa kukosa kutumia gari yake.

Mwisho wa siku Gharama zikawa ni zaidi ya BILLION MOJA na utawala wa JK ukawa umefikia mwisho.. Hapo nyuma Prof alishashinda kesi maranyingi tu lakini kulipwa ilikuwa shughuli pevu. Baada ya Magufuli kuingia tu jumba jeupe.. Prof akarudi mahakamani kukazia hukumu.

Majembe sasa wakiwa hawana mbeleko tena.. Wakaamriwa walipe maramoja na wakishindwa mali zao zikamatwe zipigwe mnada.. Walipewa siku 14 kisha wakaongezewa saba jumla siku 21.

Muda ukaisha bila kulipa hata thumni.. Mali zao zikakamatwa na kupigwa mnada.. Mojawapo ilikuwa godown kubwa kona ya kwenda Cocacola pale Mwenge.

Soma Pia:
Prof. Akajikusanyia mabilioni na ndio ukawa mwisho wa MAJEMBE AUCTION MART WAZEE WA KAZI! Wafanyakazi wa OYA wanatuhumiwa kuuwa mtu kwenye kudai marejesho. Mahakama zenyewe huwa hazifungi wadaiwa. OYA keshajitia gundu. Ndugu wa marehemu wakipata mawakili wazuri OYA Inaenda Kufilisiwa. Na hata kama kesi hii watachomoa lakini mwisho wao hauko mbali.

View attachment 3120149
hawa ndugu zake Januari kwakweli wamezidi yaani kila kona mitandaoni nawaona wao tu hivi wananini? janjajanja nyingi hawa , ila ukiona watu wanahangaika sana mikopo ujue hali mbaya kuna jinsi serikali inatakiwa ijitathmini kila kona ukipita kausha damu sijui kumekuaje huko Bongo.
 
Utu ni jambo muhimu sana kwenye huu uumbaji wa Mwenyezi Mungu

Kampuni ya mikopo midogomidogo ya OYA si kampuni rafiki na yenye UTU kwa wakopaji wake. Pamoja na kuwa na vibali halali vya kuendesha hiyo biashara lakini matendo ya wafanyakazi wake kwa wakopaji wanaoshindwa kurejesha kwa wakati yanatia shaka nia ya kuwasaidia watu.

Kuna ukatili mkubwa unyanyasaji, uonevu nk kwa wateja wao. Kwa kifupi wanaogopeka kuliko polisi.. Mbaya zaidi pesa zao ni kama zina laana hazilipiki ukikopa.

Nyakati za Kikwete iliibuka kampuni ya udalali ya MAJEMBE halafu ikapata kazi za serikali za kukamata wadaiwa na wrong parking.. Hakuna rangi wananchi wenye ishu za kikodi na wrong parking walipokutana na wafanyakazi wa MAJEMBE.

Mimi ni mhanga wao.. Walikamata gari yangu wakati kesi iko TRA 2014.. Gari ilikuja kupigwa mnada mwaka 2021 Majembe ikiwa tayari ni Marehemu kwenye biashara.

Nini kiliwapata?

Walikamata gari ndogo ya Professor wa chuo kikuu UDSM maeneo ya Magomeni wakidai alipoegesha ni wrong parking.. Prof akawaomba wamuoneshe alama inayoonesha NO PARKING lakini wakaleta ubabe na kuivuta gari mpaka kwenye maegesho yao mpaka prof alipe faini.

Prof. Akakimbilia mahakamani.. Majembe wakiwa wamepewa kazi ya wrong parking na manispaa ya Kinondoni wakati huo na wenye nguvu serikalini wakaisumbua sana mahakama. Prof. Akawa ana 'document' kila gharama anayotumia kwa kukosa kutumia gari yake.

Mwisho wa siku Gharama zikawa ni zaidi ya BILLION MOJA na utawala wa JK ukawa umefikia mwisho.. Hapo nyuma Prof alishashinda kesi maranyingi tu lakini kulipwa ilikuwa shughuli pevu. Baada ya Magufuli kuingia tu jumba jeupe.. Prof akarudi mahakamani kukazia hukumu.

Majembe sasa wakiwa hawana mbeleko tena.. Wakaamriwa walipe maramoja na wakishindwa mali zao zikamatwe zipigwe mnada.. Walipewa siku 14 kisha wakaongezewa saba jumla siku 21.

Muda ukaisha bila kulipa hata thumni.. Mali zao zikakamatwa na kupigwa mnada.. Mojawapo ilikuwa godown kubwa kona ya kwenda Cocacola pale Mwenge.

Soma Pia:
Prof. Akajikusanyia mabilioni na ndio ukawa mwisho wa MAJEMBE AUCTION MART WAZEE WA KAZI! Wafanyakazi wa OYA wanatuhumiwa kuuwa mtu kwenye kudai marejesho. Mahakama zenyewe huwa hazifungi wadaiwa. OYA keshajitia gundu. Ndugu wa marehemu wakipata mawakili wazuri OYA Inaenda Kufilisiwa. Na hata kama kesi hii watachomoa lakini mwisho wao hauko mbali.

View attachment 3120149

Majembe walijaa wapigaji wa mali za watu wanadaiwa, hasa minada ya nyumba kupitia benki. Nategemea waliovuna wasipopanda wanaona hasara yake
 
Niko tofauti na wengi, ni kweli kuua mtu kwa deni la 300k, ni kosa kubwa.
Lakini tusipuuze umuhimu wa hii tasasisi kwa wafanya baishara wengine wengi, wanao nufaika na mikopo toka kwao.

Kukopesha mtu ni rahisi sana, na kurudisha marejesho/mikopo ni jambo gumu mno;
-Wanachama wa uvccm ni wadaiwa sugu toka DCB Commercial Bank mpaka leo
-Kuna makanisa yalianzisha banki zao, tayari hizo banki ni marehemu.
-Kuna bank zimevunja uhusiano wa kibiashara kutokana na wafanyakazi kutolipa mikopo yao
-Kuna wasomi walikopeshwa pesa wasome elimu ya juu, leo wangapi wamelipa?

Mbali ya OYA,
Kuna hizi "kausha damu" au "chupi mkononi".
je mnajua ni mangapi wakopaji wanapitia? Ni mwendo wa stress na kuzikimbia nyumba zao.

au basi tuseme ni watu wangapi leo wanaweza kukopa pesa bank za NMB, CRDB, DTB, EXIM, nk?

https://www.dcb.co.tz/

 
Sometimes we need to lend a voice to those who cannot speak

R I P
 
Back
Top Bottom