Kampuni za mabasi, ni vema kumwambia abiria gharama ya mzigo wake wakati anapanda basi

Kampuni za mabasi, ni vema kumwambia abiria gharama ya mzigo wake wakati anapanda basi

Michael mbano

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2022
Posts
820
Reaction score
570
Zipo baadhi ya kampuni za mabasi wahudumu wake wanakosa sifa za huduma bora ili kuepusha migogoro.

Mfano kuna kampuni inaitwa Kisumapai ya Songea, kuna siku nimesafiri nimepokelewa na mhudumu aliyevaa tishet yao akaweka mzigo wangu kwenye buti. Wakati huo mkatisha tiketi wa kampuni hiyo anaona.

Nilipofika kituo cha kushuka kondakta ananiambia lipia mzigo. Sasa ishu haikuwa kulipa ila kwanini hamumjulishi mteja mapema wakati mnapokea mzigo wake kuwa utagharimu kiasi fulani kabla gari haijatoka ili mtu ajijuwe mapema?

Kitendo cha kufika mahala pakushuka ndipo mnamwambia mnaleta mgogoro tena mgogoro unachangiwa na kondakta kwasababu anapaswa awepo wakati mizigo inapakiliwa. Ajabu pia anajibu hamjuwi aliyepokea mzigo kwahiyo walimuachaje mtu hadi anavaa tishet yao na kuwajibika kwenye gari yao?

Jambo hili limetokea kwa watu tofauti pia, hata ukituma maoni na ushauri ktk namba walizokuandikia haujibiwi. Mjirekebishe na siyo kampuni hiyo tu na kampuni nyingine pia wenye tabia kama hizo mtafukuza wateja.
 
Alafu stendi ya hapo songea huwa kuna mtu tu anatoza ela ya mizigo kwa wasafiri wote ambao wanaenda mikoa mingine,
Huo utaratibu hauaminiki kwakuwa jamaa anakupa karisiti tu hakaeleweki,
Alafu huo utaratibu mbona stendi nyingine kubwa haupo kwa nin hapo tu ..
 
Huu uhuni upo sana hata kwa super Feo, pale songea mjini kabisaa wanachukua nauli ya mzigo, na kule shule ya tanga wanadai tena, ukiuliza na wanasema wao hawausiki.

Wanakera mnooo.
 
Niliwahi kuwakazia hadi wakakubali mziki. Bahati nzuri wakati mzigo inapelekwa kwenye buti, niliuliza kama nalipia au lah!! Wakasema mzigo hautalipiwa. Nikapanda garini. Kushuka wanadai kwanini sina tiketi, nikawambia tiketi inatolewa kwa mzigo uliolipiwa. Jamaa akasema nilipie. Nikagoma akasema sitoki na mzigo. Nikamwambia fesh, mzigo wangu una thamani ya milioni mbili na nusu na nikataja vilivyomo (nilidanganya) nikamwambia naandikisha jina lake na langu ofisini kwao, siku nikipata pesa naurudia. Jamaa akasema poa (alidhani namtania kuhusu kuandikisha) nikamwambia aubebe hadi ofisini, akakataa. Nikamwambia ita mbebaji akakataa. Nikamuuliza nauli nalipa ya nini, akasema ya usafiri. Nikamuuliza nisingekuwepo nani angewajibika kuupeleka ofisini akasema waneubeba na toroli (ulikuwa mzito). Nikamwambia siondoki hadi mzigo ufike ofisini na siubebi. Chagua moja, nibbe nisepe ama uubebe ukautunze. Nikaona jamaa anlalamika kwanini wamebeba mizigo ya bure. Nikaamsha na mzigo wangu.
 
Alafu stendi ya hapo songea huwa kuna mtu tu anatoza ela ya mizigo kwa wasafiri wote ambao wanaenda mikoa mingine,
Huo utaratibu hauaminiki kwakuwa jamaa anakupa karisiti tu hakaeleweki,
Alafu huo utaratibu mbona stendi nyingine kubwa haupo kwa nin hapo tu ..
Mzigo ukiwa na uzito flan wanatoza hela.Na vinginevyo kama unatumwa mzigo peke unalipiwa.Ila ajabu mimi nilifunga mzigo flan uzito kama kg50 wakati huo nilitoka dar kuja mkoani wala sikuulipia.Labda watalam wa maswala ya usafiri watusaidiye.
 
Back
Top Bottom