Kampuni za mikopo mtaani zina mapungufu ya kibinadam sawa lakini pia na wateja wao (wakopaji) wengi wahuni tutazame kotekote

Kampuni za mikopo mtaani zina mapungufu ya kibinadam sawa lakini pia na wateja wao (wakopaji) wengi wahuni tutazame kotekote

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Kampuni za wakopeshaji pesa zilizozagaa mtaani kwa lugha ya pesa chap chap!

Baadhi zinafanya vizuri na baadhi zinafanya vibaya!
Ifahamike mtandao wa biashara unapoajiri vijana wengi huhitaji weledi wa juu sana kuweza kuwakumbusha Hekima ya biashara!

Nitoe mfano hai!

Jeshi la polisi lina vijana wenye mafunzo na weledi mzuri kutoka chuo cha mafunzo!

Lakini mara moja moja huwa tunashuhudia baadhi yao wanapofikishwa vituo vya kazi huweza kuadhibu watuhumiwa hata matukio kadhaa huwa tunasikia watuhumiwa kufia mahabusu!

Sasa makosa kama hayo ya askari mmoja kumwazibu raia hata kuuwa huwa hakiwezi kufuta taasisi nzima ya jeshi la polisi!

Hivyo basi! Makosa ya kibinadamu kwa watendaji hayapaswi kufuta taasisi kwasababu katiba ya taasisi huwa haina sera ya kuuwa mtu katika madai!

Taratibu za mikopo zinafahamika! Kila mkopaji na mkopeshaji huwa wanamakubaliano!

Utekelezaji wa hayo makubaliano unapovunjwa na wahudumu siyo busara kufuta taasisi nzima!

Nashauri linapotokea jambo kama hilo lililotokea kampuni ya OYA Kesi isikilizwe kama kesi zingine za mauaji mahakamani na inapobainika wahusika wa tukio wawajibishwe wao kama wao!

Lakini kwa upande mwingine WAKOPAJI (WATEJA) Baadhi yao wamekuwa chanjo cha kuvunja makubaliano!
Unachukua mkopo OYA Halafu unakwenda kufanyia shughuli ambazo hazizalishi, hili nalo linachangia usumbufu katika marejesho, lugha na ushirikiano wa wateja baadhi siyo rafiki wengi huzima simu na kujificha!
Sasa Pesa za wakopeshaji ni za mzunguko kwamba wateja wasipolipwa nao hawalipwi n.k

Mambo kama hayo yanaweza ibua vita ya kudaiana!

Ushauri wangu!
Elimu itolewe kwa wakopeshaji na endapo kukiwa na ukiukwaji wa masharti ya malipo, basi wakopeshaji wahakikishe wanachukua barua kutoka kwa mwenyekiti wa mtaa wanapokuja kuchukua dhamana kwa mteja wao!
Pia wakopaji wajiridhishe uhalali wa dhamana kama ina mhusu mkopaji haiwezekani mme hana taarifa ya mkopo halafu wakoshaji wafike kuchukua dhamana!

KUKOPA SHEREHE KULIPA MATANGA!

Soma:

=> Pwani: Wafanyakazi wa kampuni ya mikopo ya OYA, mbaroni kwa tuhuma za mauaji
 
Kampuni za wakopeshaji pesa zilizozagaa mtaani kwa lugha ya pesa chap chap!

Baadhi zinafanya vizuri na baadhi zinafanya vibaya!
Ifahamike mtandao wa biashara unapoajiri vijana wengi huhitaji weledi wa juu sana kuweza kuwakumbusha Hekima ya biashara!

Nitoe mfano hai!

Jeshi la polisi lina vijana wenye mafunzo na weledi mzuri kutoka chuo cha mafunzo!

Lakini mara moja moja huwa tunashuhudia baadhi yao wanapofikishwa vituo vya kazi huweza kuadhibu watuhumiwa hata matukio kadhaa huwa tunasikia watuhumiwa kufia mahabusu!

Sasa makosa kama hayo ya askari mmoja kumwazibu raia hata kuuwa huwa hakiwezi kufuta taasisi nzima ya jeshi la polisi!

Hivyo basi! Makosa ya kibinadamu kwa watendaji hayapaswi kufuta taasisi kwasababu katiba ya taasisi huwa haina sera ya kuuwa mtu katika madai!

Taratibu za mikopo zinafahamika! Kila mkopaji na mkopeshaji huwa wanamakubaliano!

Utekelezaji wa hayo makubaliano unapovunjwa na wahudumu siyo busara kufuta taasisi nzima!

Nashauri linapotokea jambo kama hilo lililotokea kampuni ya OYA Kesi isikilizwe kama kesi zingine za mauaji mahakamani na inapobainika wahusika wa tukio wawajibishwe wao kama wao!

Lakini kwa upande mwingine WAKOPAJI (WATEJA) Baadhi yao wamekuwa chanjo cha kuvunja makubaliano!
Unachukua mkopo OYA Halafu unakwenda kufanyia shughuli ambazo hazizalishi, hili nalo linachangia usumbufu katika marejesho, lugha na ushirikiano wa wateja baadhi siyo rafiki wengi huzima simu na kujificha!
Sasa Pesa za wakopeshaji ni za mzunguko kwamba wateja wasipolipwa nao hawalipwi n.k

Mambo kama hayo yanaweza ibua vita ya kudaiana!

Ushauri wangu!
Elimu itolewe kwa wakopeshaji na endapo kukiwa na ukiukwaji wa masharti ya malipo, basi wakopeshaji wahakikishe wanachukua barua kutoka kwa mwenyekiti wa mtaa wanapokuja kuchukua dhamana kwa mteja wao!
Pia wakopaji wajiridhishe uhalali wa dhamana kama ina mhusu mkopaji haiwezekani mme hana taarifa ya mkopo halafu wakoshaji wafike kuchukua dhamana!

KUKOPA SHEREHE KULIPA MATANGA!
Uko sahihi sana,Ila kwa Mila zetu za kiafrika kuna mambo mengine hayaepukiki ,Inatokea umefiwa na mtu wako wa Karibu,wao hawaelewi hayo! Mwisho wake ndio kama haya kuzima simu au kuingia mitini.La mwisho pia kwa haovwakopeshaji wanakuwa na malengo makubwa yakufikia wateja ili waweze kulipwa commission nzuri,hivyo hujikuta hawana muda wa kuangalia uhalisia wa mtu wanaemkopesha.
 
Mikopo inatesa sana kama huna msuli mgumu lazima upate shida ni vema hii elimu itolewe kwa watu sio vema kukopa na kushindwa kulipa
 
Uko sahihi sana,Ila kwa Mila zetu za kiafrika kuna mambo mengine hayaepukiki ,Inatokea umefiwa na mtu wako wa Karibu,wao hawaelewi hayo! Mwisho wake ndio kama haya kuzima simu au kuingia mitini.La mwisho pia kwa haovwakopeshaji wanakuwa na malengo makubwa yakufikia wateja ili waweze kulipwa commission nzuri,hivyo hujikuta hawana muda wa kuangalia uhalisia wa mtu wanaemkopesha.
Kama huwezi kuvumilia kudaiwa kama mm bora usikope!
Mimi ukinidai hata kama kweli ulinikopesha huwa nakasirika naweza hata kukujeruhi! Sitaki kupigiwa pigiwa simu kuulizwa wakati nafahamu nikipata nitalipa!
Kwa maana hiyo huwa sipendi kukopa kopa
 
Kama wewe unamkopesha mtu kiasi cha pesa ambacho hujajiridhisha kuwa anaweza kukilipa au hajaweka dhamana ya mali isiyo hamishika yenye thamani ya pesa yako wewe mkopeshaji ndo mjinga.

Na tabia ya kwenda kumshambulia mume wakati mke ndo kakopa tena wakati mwingime mwanaume hajui hiyo ni kinyume na Sheria hao watu wanatakiwa sahivi waanze kutembezewa kichapo wao.

Alafu wanawake wengi wanavichwa vigumu sana wanapenda kukopakopa hovyo haliyakua hawana biashara yoyote inayowawezesha kulipa hiyo mikopo mwisho wanaingiza familia kwenye matatizo
 
"kwenye kudai, hasa mteja mkorofi, huwa kuna kiwango kidogo sana cha busara na uvumilivu hutumika!"
 
Kumkopesha mbongo ni jaribio lenye risk sana na linahitaji roho mbaya ya kiwango chake ili walau kuwe na asilimia kadhaa za matuamaini ya kuweza kulipwa.

Bongo ndio sehemu ambayo mdaiwa yuko tayari kwenda gym kutanua misuli na kifua ili kumtisha mdeni wake.
 
Kumkopesha mbongo ni jaribio lenye risk sana na linahitaji roho mbaya ya kiwango chake ili walau kuwe na asilimia kadhaa za matuamaini ya kuweza kulipwa.

Bongo ndio sehemu ambayo mdaiwa yuko tayari kwenda gym kutanua misuli na kifua ili kumtisha mdeni wake.
Haha
 
Back
Top Bottom