Kanda ya Nyasa: Homa ya Oparesheni 255 yapanda, yasubiriwa kwa hamu

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Kuwa wa kwanza kufahamu kwamba kituo kinachofuata kwa ile Oparesheni kabambe ya 255 KATIBA MPYA , OKOA BANDARI ZETU ni Kanda ya Nyasa .

Bado haikupangwa ratiba ya Oparesheni hiyo kwenye kanda hiyo , lakini tayari mizuka ishawapanda wananchi , kila mtu anasubiri ujio wa Jambo hilo

Taarifa zilizotufikia ni kwamba Chadema imeandaa kikosi kazi kikali mno kitakachotoa Elimu ya kutukuka kuhusu Umuhimu wa Katiba mpya sasa , na Tume Huru ya Uchaguzi , huku likiibuka jambo jipya la kushirikisha Wahadhiri 15 kutoka Chuo Kikuu waliopewa jukumu la kuwatafsiria wananchi Mkataba mbovu wa Bandari za Tanganyika na DP WORLD ya Dubai .

Usiondoke JF kwa Taarifa zote za Uhakika .

 
Acha porojo zako wakati unafahamu ukweli kuwa CDM imekimbiwa na makundi yote na kubakia inahangaika tu.
 

Tungeunganisha nguvu ushindi ungekuwa mapema asubuhi.

Sherehe kubwa Lumumba, CHADEMA wakiparurana

Kama nawaona kina Joni wakiserebuka.
 
Chadema haijawahi kukataa ushirikiano wenye tija , msipotezwe maboya na waliolipwa

Haya ya kulipwa na kutolipwa ni illusion. Sawa na ramli tu ambapo mtuhumiwa anaweza kuwa yeyote ukiwamo hata wewe.

Tunajua maandamano yanayo majibu yetu yote. Kudogosha jitahada za kina Mdude hakuwezi kueleweka.
 
Haya ya kulipwa na kutolipwa ni illusion. Sawa na ramli tu ambapo mtuhumiwa anaweza kuwa yeyote ukiwamo hata wewe.

Tunajua maandamano yanyo majibu yetu yote. Kudogosha jitahada za kina Mdude haziwezi kuwa halali.
Ni nani ameingilia mikutano hiyo ? halafu ninaposema wamelipwa si maanishi Slaa au Mdude , kuwa makini na Magazeti yanayochochea jambo hilo
 
Mungu Ibariki CHADEMA..!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Your browser is not able to display this video.
 
Ni nani ameingilia mikutano hiyo ? halafu ninaposema wamelipwa si maanishi Slaa au Mdude , kuwa makini na Magazeti yanayochochea jambo hilo

Hakuna anayesema ameingilia mikutano yao isipokuwa nani asiyejua nchi hii itakombolewa kwa maandamano na si majukwaani?

Magazeti au awaye yote atuhusu sisi nini wapi, kama hoja zetu ni kuikomboa nchi kutokea kwa adui anayejulikana?
 
Hakuna anayesema ameingilia mikutano yao isipokuwa nani asiyejua nchi hii itakombolewa kwa maandamano na si majukwaani?

Magazeti au awaye yote atuhusu sisi nini wapi, kama hoja zetu ni kuikomboa nchi kutokea kwa adui anayejulikana?
Sasa shida yako ni nini ?
 
Kuwa makini na hizo kauli zao

Tuko makini na kauli zote. Zaidi sana katika zote misahafu iko wazi: mtawajua kwa matendo yao. Tulipo tunataka kumwagika barabarani. Majibu yetu yako huko.
 
BREAKING: Tumepokea taarifa kutoka ndani ya TISS kwamba, Kongamano la Sauti ya watanzania limeingiliwa, na halitafanyika tena leo. Waliolipa fedha za ukumbi wameambiwa wakazichukue. Pia, chanzo kinataarifu OPERESHENI ya Chadema +255 ipo hatarini kuzuiwa. Msiache hoja ya DP World.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…