Kangi Lugola: Watuhumiwa kufia mikononi mwa polisi ni Mitego ya kifo. Kwani wanaokufa wakifanya mapenzi mnachoma Kitanda?

Kangi Lugola: Watuhumiwa kufia mikononi mwa polisi ni Mitego ya kifo. Kwani wanaokufa wakifanya mapenzi mnachoma Kitanda?

Na fikiri hawa mawaziri wa magufuli hawakuona ndani ya darasa. unaweza aje wewe kaa waziri kujibu swali namna hio, hata mtoto wa kindergarten anaweza fikiria poa kukuliko bwana waziri.sijui ulipata aje hio nafasi ya uwaziri
Inatakiwa aendane na kichaa cha.....
 
"Mtuhumiwa alijaribu kutoroka alipokua anaenda kuonesha alipoficha silaha, alipigwa risasi ya mguu na amefariki akiwa njiani anapelekwa hospitali"
[emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16]
 
Hii ni laana juu ya watawala ndio maana hawaoni aibu kutoa/kuongea maneno ya hovyo hovyo.
 


Katika siku za hivi karibuni kumetokea tabia mbaya na chafu na ovu kabisa ya Mahabusu kufia kwenye vituo vya Polisi. Mahabusu wanapelekwa wanapata mateso yanayopelekea vifo vyao, kuna baadhi ya jamii zimekataa kuchukua maiti kwenda kuzizika

Kangi Lugola: Mwananchi kufa, anakufa wakati wowote na mahali popote . Sijui kwenye Quran lakini kwenye Biblia ukisoma Muhubiri 9:12 kifo ni mtego, kifo humnasa mtu wakati wowote na mahali popote

Mtu anaweza kufa akiwa polisi, akiwa anafanya mapenzi, anaweza akafa akiwa kwenye gari anasafiri na aweza kufia hata humu Bungeni kwahiyo isije ikachukuliwa kwamba nayefika kituo cha polisi ni kwamba ameteswa

Lakini nikiri kuwa kuna matukio ya Watu kufia mikononi mwa Polisi, na pale ambapo matukio hayo yanajitokeza huwa tunafanya uchunguzi na ikibainika Polisi wanahusika huwa tunachukua hatua

> Na ndio maana tunawazuia wananchi wasichukue sheria mkononi na kwenda kuchoma kituo cha polisi. Mbona huyu anayefia akifanya mapenzi mbona hawaendi kuchoma kitanda?

Kwahiyo Polisi na kitanda ni kama original na copi!
 
Mahabusu wanaokufa Polisi wanafia kitandani? J.K. Nyerere alisema '...akishakula nyama ya mtu haachi.' Maana yake ukimwaga damu ya binadamu usipotubu hutaacha.
 
Jina lake lilivyo la ajabu na mpaka akili yake pia ni hivyo hivyo... Jiwe junior
 
Atuwekee takwimu za waliofia bungeni na waliofia jela/mahabusu kama vina uwiano.

Hawa hawathamini uhai wa mtu. Ndiyo maana wanadhani ku pyu pyu watu ni njia ya kuwanyamazisha.
Dah....😎
 
Tujikumbushe hesabu kidogo
Kangi = Konyagi,
Logola = Ugoro.
a²+b²=c²,
Sasa chukua hesabu hii hapo chini unipe jibu kwa kufata kanuni hapo juu kisha utoe jibu sahihi.
Ukichukua Konyagi² + ugoro² = ujiga².
 
Hivi watu wanachoma polisi kwa sababu ya mtu kufia polisi au sababu ya nini kimesababisha kifo hicho? Mungu ibariki Tanzania na viongozi wake
 
Kutothamini uhai wa mtu ni jambo la ajabu sana. Endeleeni kuwapa polisi kiburi kiburi lakini mda wenu pia WS kuachia Dora utafika. Nadhani hapo ndo mtajua umuhimu wa uhai wa watu
 
Hawa jamaa majibu yao siku hizi ni machafu sana, yaani kama sio viongozi wetu vile.. wanajibu kwa dharau, mifano yao ya ajabuajabu tu yaani hawana hata nidhamu
 
Huyu comedian hata kwa shilingi 100000 ningeingia. Maana hatujawahi kupata comedian mzuri kama huyu toka tupate Uhuru.

Ikulu imemuona Masanja hafai ndio maana wamemualika huyu comedian ili atoe uoga wa mawaziri angalau kwa kucheka kwa dakika 3, kuepukana na mziki wa hapa kazi tuu.

Hapa Magu kafanya kazi, kwani hii si Kawaw funika kikombe bali Kanga binti mtandio wachekeshe mawaziri.
 
Watu wengine kama wamelewa madaraka vile eh. Kwa umri huu ni wakulinganisha kufia polisi na kitandani? Kama ametoka kwake mzima,kafia jera,ina maana ameteswa mpaka majeraha kumsababishia kifo. Kwa hiyo kuchoma kituo cha polisi,ni hasira za uovu wao kumdhurumu mtu uhai wake. Sasa mapenzi na uovu wa maskari wapi na wapi? Watu wengine sijui kabisa
 
Back
Top Bottom