Kanisa kumuombea JK dhidi ya mafisadi

Kanisa kumuombea JK dhidi ya mafisadi

MaxShimba

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2008
Posts
35,771
Reaction score
4,065

Kanisa kumuombea JK dhidi ya mafisadi

Na Peter Mwenda

WAUMINI wa Kanisa Katoliki nchini, leo watakuwa na ibada maalum ya kuombea taifa liendelee kuwa na amani, utulivu na kuitakia mafanikio mema Serikali ya awamu ya nne katika vita dhidi ya ufisadi.

Hayo yapo katika salamu za Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Kadinali Policarp Pengo zilizosambazwa katika makanisa yote nchini.

Paroko Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Ukonga, Padre Joseph Kanduta, akitoa ujumbe wa Askofu Pengo kwa waumini wa kigango cha Kitunda alisema Wakatoliki wote watakuwa na ibada leo itakayokuwa maalum kwa ajili ya kuombea amani.

"Askofu Pengo amewataka waumini kuiombea serikali ya Rais Kikwete isikate tamaa kupambana na ufisadi kwa kuwa ni kazi ngumu ambayo inahitaji baraka za mungu kufanikiwa, tufike kwa wingi kuombea utulivu katika kipindi hiki kinachohitaji ujasiri," alisema Padre Kanduta.

Ibada hiyo pia imeapewa kipaumbele na Wanawake Wakatoliki Nchini (WAWATA) Jimbo la Dar es Salaam ambao wameandaa ibada ya kuombea amani kwa kuwaunganisha wanawake wote wa jimbo hilo kusali pamoja katika eneo ambalo huenda kuhiji lililopo karibu na shule ya Sekondari ya Pugu.

Habari kutoka kwa wanawake hao zinasema akina mama hao wataanza ibada hiyo kwa maandamano kutoka Shule ya Sekondari Pugu kuingia kwenye eneo maalum la hija ambapo wanatarajia Askofu Pengo ataongoza ibada hiyo.

Comment in this Story Nakala inayochapika





 
Kanisa kumuombea JK dhidi ya mafisadi

Na Peter Mwenda

WAUMINI wa Kanisa Katoliki nchini, leo watakuwa na ibada maalum ya kuombea taifa liendelee kuwa na amani, utulivu na kuitakia mafanikio mema Serikali ya awamu ya nne katika vita dhidi ya ufisadi.

Hayo yapo katika salamu za Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Kadinali Policarp Pengo zilizosambazwa katika makanisa yote nchini.

Paroko Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Ukonga, Padre Joseph Kanduta, akitoa ujumbe wa Askofu Pengo kwa waumini wa kigango cha Kitunda alisema Wakatoliki wote watakuwa na ibada leo itakayokuwa maalum kwa ajili ya kuombea amani.

"Askofu Pengo amewataka waumini kuiombea serikali ya Rais Kikwete isikate tamaa kupambana na ufisadi kwa kuwa ni kazi ngumu ambayo inahitaji baraka za mungu kufanikiwa, tufike kwa wingi kuombea utulivu katika kipindi hiki kinachohitaji ujasiri," alisema Padre Kanduta.

Ibada hiyo pia imeapewa kipaumbele na Wanawake Wakatoliki Nchini (WAWATA) Jimbo la Dar es Salaam ambao wameandaa ibada ya kuombea amani kwa kuwaunganisha wanawake wote wa jimbo hilo kusali pamoja katika eneo ambalo huenda kuhiji lililopo karibu na shule ya Sekondari ya Pugu.

Habari kutoka kwa wanawake hao zinasema akina mama hao wataanza ibada hiyo kwa maandamano kutoka Shule ya Sekondari Pugu kuingia kwenye eneo maalum la hija ambapo wanatarajia Askofu Pengo ataongoza ibada hiyo.

Comment in this Story Nakala inayochapika

Muse A Muse...Kwanza karibu sana ukumbini.
Je habari hii umeipata wapi? Whats the source?
Kwasababu heading inadai kanisa kumwombea JK dhidi ya mafisadi na ukweli ni kuwa ni kuliombea Taifa kama inavyoonyesha kwenye highlight.
Kauli inayokaribiana na kichwa cha habari hata hivyo ni hiyo ya Pengo kuwa sirkali ya JK isikate tamaa kupambana na ufisadi....Sasa wapi hapo penye JK dhidi ya mafisadi kwenye habari hii?
 

Peter Mwenda ni mwandishi wa IPP, kwahiyo, nafikiri hii habari ameipata IPP Media
 
Na hilo Jimbo la Ukonga (para 3) liko wapi? Tuache kulegea legea hivi jamani!
 
Kinachoombewa hapa si JK dhidi ya mafisadi bali nchi ambayo tayari imekosa mwelekeo. Nchi iliyokosa viongozi wenye dira sahihi akiwemo JK mwenyewe. Nchi yenye viongozi waroho na wabinafsi na walio tayari kuiuza nchi yao kwa wageni ilimradi wajikusanyie mabilioni. "Wananchi kuleni majani, ni lazima 10% ipatikane kwenye biashara ya ndege ya Rais na Rada .....". Kanisa limeamua kumwomba Mungu ainusuru nchi na madhila hayo ili aiongoze kupata viongozi waadilifu na wenye kumwogopa (Mungu)
 
Kinachoombewa hapa si JK dhidi ya mafisadi bali nchi ambayo tayari imekosa mwelekeo. Nchi iliyokosa viongozi wenye dira sahihi akiwemo JK mwenyewe. Nchi yenye viongozi waroho na wabinafsi na walio tayari kuiuza nchi yao kwa wageni ilimradi wajikusanyie mabilioni. "Wananchi kuleni majani, ni lazima 10% ipatikane kwenye biashara ya ndege ya Rais na Rada .....". Kanisa limeamua kumwomba Mungu ainusuru nchi na madhila hayo ili aiongoze kupata viongozi waadilifu na wenye kumwogopa (Mungu)

Ntiru umeileza vyema, ila mwandishi na kichwa cha habari kimepinda kidogo kwani kinaelekeza kumuombea JK aka Chaguo la Mungu!!!

Well, hapa ni kuiombea nchi yetu Mungu ainusuru katika makucha ya mafisadi!
 
To me this is crazy.God does not work like this.For God to help, Kikwete first needs to realize that there is a problem,and then have a genuine desire to solve it.He then needs to take action.Only then can God help in solving the problem.
 

Peter Mwenda ni mwandishi wa IPP, kwahiyo, nafikiri hii habari ameipata IPP Media

Ilikua katika majira ya jana na si IPP Media

pia ilitoka katika Dar Leo ya wiki iliyopita kwa njia tofauti kabisa

DarLeo-Gazeti lako la kila siku jioni
Mkapa,Mramba wagusa Kanisa Katolika. •

na

ktk Raia Mwema ya leo nalo kwa njia tofauti pia
 
Back
Top Bottom