Kanisa la Wasabato Mnapaswa Mkosoe maovu ya serikali zaidi kuliko kukosoa wenzenu wa Roman Catholic


Sasa mbona hata huko makanisani kwenu mnatumia siasa kupata viongozi au wewe siasa unaielewa vipi?yawezekana hata neno siasa hulielewi mana yake.
 
Sasa kazi ya dini ni nini ? Ikiwa viongozi wa serikali wanatenda unyama, wanaiba kura na nyinyi mnaona hilo msiseme eti sio kazi yenu [emoji849]

Mnamsubiri mbowe awasemee
Ndo mana nakuambia kuna mgawanyo wa majukumu, hayo ya wizi wa kura tupaze sauti mimi na wewe,

Viongozi wa dini zote hii nchi sidhani hata kama wanafika 100k, tunabaki na watu 59.9M wa kusemea hayo masuala, kweli sisi tutashindwa kusema hadi tuombe viongozi wa dini waje waseme ?
 
Unakosea sana, kwamba Katoliki ndo walioandika Biblia?? Elimu yako ya dini ni dhaifu. Roma ndo ilificha Biblia katika kipindi chote cha zama za giza, mpaka uprorestanti ulipoingia ndo Biblia ikaachiwa huru kusomwa. Tambua utume wa kanisa mkuu.
 

Wasabato ni taasisi kubwa iliyosambaa ulimwenguni acha kufananisha na hizi local churches
 
Ukisikia kujiongeza kwa kijinga ndio huku sasa,

"Yani TEC waseme hawaridhishwi na CCM au sera za ACT"
[emoji16][emoji16][emoji16]

Kama umeelewa kuingilia siasa kwa namna hii basi hujamuelewa Robert.

Yani kama hivi kwenye muswada mpya wa uchaguzi, Raisi ateue tume ateue watendaji, yeye pia ni mgombea alafu uite uchaguzi huo ni wa haki ???

Alafu viongozi wa dini muitwe mtoe maoni alafu useme sisi hatuingilii siasa ???
 
Sio kazi ya kiongozi wa dini kumpangia mwana siasa namna ya kuendesha siasa zake na ndio maana hiyo ikaitwa siasa na nyingine ikaitwa dini kwa maana ni vitu viwili tofauti.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app

Dini ni siasa ya kale,huoni primitive religions kama uislam wanalazimisha siasa ya kale dini iendelee kutawala katika ulimwengu wa sasa.
 
Bado siasa huwezi ikwepa, kwenye familia kuna siasa, hata huko kanisani kuna siasa viongozi mnawapataje kama sio kwa kura ?? Hiyo sio siasa
 
Tangu nazaliwa wasabato wanahubiri ishu ileile Mara mnaabudu sanamu Mara Freemason Mara duh! Sijui Ellen G mweupe aliwafundisha hivyo????

Yaaani,hadi unajiuliza huo upendo wanaofundisha makanisani mwao unamaana gani kama wao kutwa wanatangaza chuki dhidi ya rc,huwa na wambia mpinga kristo namba moja ni dini isiyomkiri kristo kama mwana wa Mungu.
 

[emoji28][emoji28] akikujibu nitag
 
Unakosea sana, kwamba Katoliki ndo walioandika Biblia?? Elimu yako ya dini ni dhaifu. Roma ndo ilificha Biblia katika kipindi chote cha zama za giza, mpaka uprorestanti ulipoingia ndo Biblia ikaachiwa huru kusomwa. Tambua utume wa kanisa mkuu.
Shughuli ya kuiunganisha Biblia na kuanza kuitafsiri ilifanyika chini ya Roma ata ukiwampagani Ili lipo wazi kabisa kulitambua maana ni Roma ndiyo ilikuwa na nguvu chini ya wafalme la Akina Costatine/Costatino waliousamba ukristo

Na kanisa la kwanza kujitenga kutoka Roma lilikuwa Lutheran na waliichukua Biblia iliyokwisha andaliwa na wazee waroma Bali Waruthel kunavitabu walivitoa Waruthel wenyewe wanalijua hilo
 
Bado siasa huwezi ikwepa, kwenye familia kuna siasa, hata huko kanisani kuna siasa viongozi mnawapataje kama sio kwa kura ?? Hiyo sio siasa
Hapa tunaongelea siasa za CCM na CHADEMA na ACT, sio hizo za nyumbani sijui uchaguzi wa KKKT,

Viongozi wa dini wabaki kurekebisha watu waishi kadri apendavyo Mungu ila sio kuingilia siasa za nchi, mwanzoni tutaona raha, ila m nakuambia itafika stage watakuwa na nguvu sana halafu wataanza kuipora madaraka serikali hususani dini zenye wafuasi wengi,

Itakuwa ukienda kinyume na RC au Waisalam bas hutoboi kwenye siasa, itakuwa full kuwalamba nyao watu wa dini,

Sasa hapo ndio itakuwa mwisho wa demokrasia
 

Katoliki ilianza kugawanyika kati ya kanisa la magharibi(Roman Catholic) na la mashariki(Othrodox) huyo mlutheri alijitoa katika kanisa la mashariki RC.
 
Unakosea sana, kwamba Katoliki ndo walioandika Biblia?? Elimu yako ya dini ni dhaifu. Roma ndo ilificha Biblia katika kipindi chote cha zama za giza, mpaka uprorestanti ulipoingia ndo Biblia ikaachiwa huru kusomwa. Tambua utume wa kanisa mkuu.

Utakuwa umenielewa vibaya.

Waandishi wa vitabu vya biblia majina yao yapo karibu kwa kila kitabu.
Japo sio vitabu vyote.
Lakini walioviunganisha ni wakatoliki na kuvipa jina moja Biblia(yaani mkusanyiko wa vitabu) na vipo vitabu vingine vingi havikuunganishwa na hao wakatoliki.

Biblia unayoiona imewekwa kwa utashi wa Wakatoliki kuanzia kitabu cha mwanzo mpaka ufunuo na vipo vitabu vingine ambavyo havijawekwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…