Mtoto halali na hela
JF-Expert Member
- Aug 10, 2012
- 52,160
- 48,974
Pole sana mkuu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Acha utoto, mwanaume mwingine yupi angeshakimbia? Jisemee wewe mjinga ungeshakimbia.Pole sanaa! Hongera kwa kumuuguza mkeo
mwanaume mwingine angekua ashakimbia.
Usianze siku yako vibayaAcha utoto, mwanaume mwingine yupi angeshakimbia? Jisemee wewe mjinga ungeshakimbia.
Mwanaume kuhudumia mkeo ni wajibu siyo fadhila awe mgonjwa au mzima. Wapumbavu kama wewe mnawaza kukimbia.
Naomba nisaidie tafadhali, japo wangu ameshakatwa.Kaka me naweza kukusaidia kabisa, huwezi amini zipo dawa mkeo anapona kabisa.....kama inawezekana fungua PM yako nakupa no umtafute kuna dada mmoja yeye aliumwa sana mpaka alitaka kukatwa saivi amepona kabisa
Ahsante sana, nitafanya hivyo kakaMaji lita 5, na majani ndoo ya kilo 10
Dawa hii nlimponesha shemeji yangu ambaye alilazwa bugando kwa kansa ya tezi dume alipofikia mwisho wakatuambia tumrudishe hom ja asingemaliza 4 weeks, akarudishwa hospitali ya wilaya. Ndo nikawaambia tujaribu hii tiba and baada ya miez 2 tu mzee alikuwa mzima na hospitali wakamdischarge aliishi 2years alikuja kuugua enimonia ikamwondoa na tulimrudisha bugando walishangaa kumwona ana afya nzuri
Ahsante sana kwa ushauri na faraja yako.Kwenye shavu tu mkuu,kakidonda kadogo kalianzia mdomoni kwa ndani.
Japo dunia ya leo imeshaharibika, kwanza upewe maua yako kwa kumjali mkeo na kufanya kila unaloliweza kuona anapata faraja ya moyo.
Si rahisi kusema kwamba tunatafuta tiba,maana wanaodai walipona huu ugonjwa sijui sijawasikia.
Bahati mbaya,mbaya sana,unajikuta matumizi ya pesa ni makubwa sana,na mtu badae anaondoka,anaacha simanzi na hali duni kwa familia. Hayayepukiki,hatuna namna.
Binafsi nakuelewa,ndugu yangu mmoja hivi karibuni nae kafiwa na mke,alikuwa Kenya. Kazaa kitoto,hajakinyonyesha,kikaletwa na kuhudumiwa. Kimefikisha miezi 6,mama anaonekana kapata nafuu,huyo,kaondoka.
Nachojaribu kusema hapa nikiangalia jama alivyobaki,asikwambie mtu. Jitahidi kujenga ukaribu na watu,pamoja na maumivu apate watu wa kuwa nae karibu,asijikatie tamaa. Wewe pia hivyo hivyo. Kuumia kwako(ni lazima kama binadamu usieona hatma ya jambo hilo),ila kumbuka unapomuonyesha kuishiwa nguvu,hili linamuathili kisaikolojia,huenda anakuona hutoweza kukabiliana na changamoto za maisha ikitokea akatangulia. Uwepo wa watu,utakusaidia hata wewe kutotokwa na machozi au kuonyesha huzuni.
Binafsi nawazaga,kama jf watu wanaweza kujadiliana mambo ya maana, wanashea upuuzi,kungekua hata na namna watu kama wewe wafikiwe,kwa nyakati tofauti tofauti,hakika mpaka unaandika hapa,mawazo yamezidi. Mpaka unahitaji msaada wa kimawazo kwa watu usiowaona na usiowajua,mi nakuelewa. Watu wangejua wenzao walipo,miongoni mwa watu 100 hata wakikutembelea 5, mnacheka,mnafurahi,unaona haupo mwenyewe,watu wanakufariji,hakiki hili linaweza kusaidia pia.
Ahsante sana, huwa tunasema ni mpangobwa Mungu kwa maana huwa tunamwomba sana atuepushe na haya ila tunaishia kuyapata, ndipo tunasema huenda mwenyezi mungu mwenyewe kapanga iwe hivi.Nikupe pole sana kwa kuuguliwa na mkeo... ila ningependa tu kuweka kitu kimoja sawa...
Kwanza kabisa kwa wewe kusema "najua yote ni mipango ya Mungu" Kiukweli si kila jambo ni lakusema mipango ya Mungu sidhani kama Mungu anaroho mbaya kiasi hicho cha kumfanya mkeo ateseke na kupitia magumu na uchungu kiasi hicho...
Watu wengi tumezoea kusema mipango ya Mungu na kujikuta kumsingizia Mungu vitu ambavyo hahusiki na kusahau kua shetani yupo pia na yeye mwenyewe ndio mshitaki wetu na asiependa kuona mtu anaongezeka, kufurahi,kufanikiwa n.k
Ningependa kunukuu tu maneno haya kutoka kitabu cha..
Yohana 10
10 Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
Hivyo kwa kusoma tu hapa nadhani utaona kazi ya adui (Shetani/mwivi) kazi zake hapo na kazi ya Mungu.
Nimeandika tu huenda nikawa nje ya mada ila niseme tu....
Mungu ajawai kushindwa... pale fikra zako zinapoishia na kuona hakuna matumaini tena, ndipo Mungu anapoanzia.
Akili za mwanadamu zina mwisho ila yeye hana mipaka wala ukomo, Mtafute Mungu namaanisha Mungu wa kweli bila kuangalia dini yako wala nini
Mtafute mtumishi wa Mungu Bishop Elibariki sumbe Youtube fatilia mafundisho yake na uchukue hatua ya kufika ibadani, Hakika utamwona Mungu akimfungua mkeo. Akuna lililo gumu kwa Mungu.
Mungu akutie nguvu na ujasiri na roho ya kukata tamaa isipate nafasi, Zidi kumwomba Mungu kutie nguvu wewe pamoja na mkeo mzidi kumwamini yeye na kumtumainia yeye.
Barikiwa Kiongozi.
Ameen kak. Ahsante piaPole sana mkuu, sipendi kuuongea ukweli huu
Ila ni kwa kuwa umetuomba tutoe ushuhuda
Kiukweli hali aliyofikia si rahisi kupona hapo lazima utampoteza mke wako mpendwa.
Pole sana ndugu.
Tunasali Mungu akupe roho ya uvumilivu, usiache kumfariji mke wako mpendwa na kumwonyesha upendo
Mwanzo wa matibabu hospital ripot ilisema ni stage 2 or 3, kama stage zinapanda sijui kwa sasa ipo stage gani maana yapata miaka miwili sasa imepitaHiyo cancer ipo stage gani? It's so sad mtu anapotea na ndugu mnaona huyu anapotea.
Ndiyo kakaAmeen kak. Ahsante pia
Umeshauguza mgonjwa wa namna hii?
Aise vyote hivyo hakufanyiwa maana lilikuwa titi la kushoto karibu na moyoDuuh polen sana
Alipewa chemo?
Upasuaji je?
Mionzi?
Sawa mkuuKuna Mtaalam mmoja wa Tiba mbadala (Sio Mganga wa Kienyeji)
Anatoka Songea na ndo office yake ilipo, ila sasa namuona anazunguka Mikoani kutibu watu wenye Matatizo mbalimbali!
Sijawahi kushuhudia mafanikio ya Tiba yake, ila mara nyingi nimekua namskia akisema anazo Dawa za Miti shamba zinatibu na kuponya Cancer aina yoyote, na katika Stage yoyote, ngoja nijaribu kummuulizia namba yake...!
Mambo ya Tiba hasa za Asili ni kujaribu bila kuchoka, hasa kwa tatizo kama la Cancer, na uzuri Wataalam wa Tiba Mbadala hawana gharama kubwa kulinganisha na matibabu ya Hospital.