SI KWELI Kanu ni Mnyama anayenukia harufu ya ubwabwa porini/vichakani

SI KWELI Kanu ni Mnyama anayenukia harufu ya ubwabwa porini/vichakani

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Huyu ni mnyama mkali sana, mkorofi, na mwenye nguvu katika jamii ya paka.

Akiingia bandani, anondoka na kuku mzima na anaenda kula kichwa mpaka shingoni. Kama ni kifaranga, anakula chote au akikuta mayai ambayo bado kidogo ya yaanguliwe, ndio soshi wake.

Anakaa vichakani au porini, sehemu yenye msitu mkali. Akigundua kwamba yupo kwenye eneo lenye adui kama mbwa, chui, fisi au binadamu, anaachia ushuzi wake ambao unanukia kama wali au ubwabwa, kiasi kwamba utadhani mtu kaficha huo wali vichakani.

Kumekuwa na dhana kwamba ukisikia harufu ya ubwabwa vichakani, ni chatu. Hapana, sio kweli; ni huyu mnyama anayeitwa kanu katika Kiswahili (kwa huku mtaani, sijui upande mwingine).

Naendelea kutega; nikikamata nitawaletea mumjue.

Huyu nimetega baada ya kula kuku wangu sana.


Kanu.jpg
 
Tunachokijua
Kanu ni wanyama wadogo, Wanyama hawa ni warefu na wembamba wenye mkia mrefu, kichwa kidogo na masikio makubwa. Rangi yao ni nyeupe hadi njano na wana madoa meusi na mkia wenye miviringo. Mpaka sasa kuna spishi 17 za kanu zilizoainishwa.

330px-Rusty-spotted_Genet_%28Genetta_maculata%29_%2832484079077%29.jpg
Kumekuwa na hoja inayodai kuwa mnyama Kanu hutoa ushuzi wenye harufu ya wali pale anapohisi adui kama njia ya kujilinda.

Je, ukweli wa hoja hiyo ukoje?
JamiiCheck imepitia makala na tafiti mbalimbali kuhusu maisha ya Kanu ili kupata uhalisia wa madai kuwa Kanu hutoa ushuzi ambao una harufu kama wali na kubaini kuwa madai hayo hayana ukweli wowote.

Kanu wana tezi zinazozalisha harufu ambazo zipo kati ya mwanzo wa mikia yao na karibu na sehemu ya haja kubwa. Tezi hizo za harufu hutoa majimaji yenye harufu ya mkojo ambayo kanu hutumia kwa mawasiliano, kuashiria maeneo yao, na wakati mwingine kuwatisha wanyama au maadui wanaowawinda.

Kama wanyama wengine wengi, kanu hutegemea kuacha alama za harufu kama njia ya kutoa taarifa kuhusu uwepo wao, hali yao ya uzazi, na mipaka yao kwa wanyama wengine.

Aidha, Harufu inayotolewa na tezi za kanu hainuki kama wali kam inavyodaiwa bali Kanu hutoa harufu ya mkojo kutoka kwenye tezi zao, harufu ambayo mara nyingi huelezwa kuwa kali na isiyopendeza, sawa na harufu ya wanyama wengine walao nyama.

Pia JamiiCheck imemtafuta na kuzungumza na Afisa habari wa TAWA Beatus Maganja ambaye ameeleza kuwa harufu ya Ubwabwa au wali porini haihusiani na wanyama mbalimbali ambao wamekuwa wakihusishwa nayo, aidha amesema kuwa harufu hiyo hutolewa na aina fulani ya miti.

"Kuhusu harufu ya ubwabwa porini wengi huihusisha na wanyama mbalimbali. Lakini Kiuhalisia kuna aina fulani ya miti Mti kama Potato Bush (kiingereza) na Jina la kisayansi ni PHYLLANTHUS RETICULATUS ambayo hutoa harufu ya aina hiyo na sio Kanu wala Gamba la nyoka maana wengine wanahusisha na nyoka kujivua gamba".:-Afisa habari wa TAWA Beatus Maganja
Huyu ni myama mkali sana na mkofi,na mwenye nguvu jamii ya paka.

Akiingia bandani anondoka na kuku mzima anaenda kula kichwa mpaka shingoni. Kama kifaranga anakula chote au akikuta mayai ambayo bado kidogo yaanguliwe ndiososi wake.
Anakaa vochakani au porini sehrmu yenye msitu mkali.

Akigundua sehemu alipo kuna adui kama mbwa chui au fisi au binadamu anaachia ushuzi wake ambao unanukia kama wali au ubwabwa kiasi kwamba utadhani ni mtu kaficha huo wali vichakni.



Kumekuwa na dhana eti ukisikia harufu ya ubwabwa vichakani ni chatu,hapana sio kweli ni huyu mnyama kiswahili anaitwa kanu (kwa huku mtaani sijui upande mwingine.
Naendelea kutega nikikamata karasa nitawaletea mumjue..
Huyu nimetega baada ya kula kuku wangu sana
Kuna jamii wanamla huyu kama sungura tu.
 
Duuh, hili nilikuwa sijui, harufu za wali nilikutana nazo sana msituni, vichakani na maporini kumbe ni huyu jamaa na sijawahi kumuona. Ni kweli hata Mimi nilisikia ni harufu ya nyoka anajivua gamba au anatapika.
Ni huyu anaachi ushuzi anapanda juu ya mti chini kama kuna mbwa hilo eneo watazu nguka kutwa nzima wakitafuta.
Hata ukimgusa huo mkono unanukia balaa hadi ufue nguo ndio harufu kutoka
Ukinawa kwa sabuni tuu na brush harufu haitoki
 
Binadamu tuna kaukatili fulani, ilikua kwenye harakati zake za kutafuta riziki ili aweze kuendelea kuishi kwenye ardhi hii ya dunia kama vile tulivyo sisi ama hao kuku, ila ndio hivyo tena kakutana na binadsmuy mwenye ubinasfi .
Sasa ndio ale kuku wangu?
 

Attachments

  • 20241009_072303.mp4
    32.6 MB
Ana madhara gani kwa binadamu nje ya kula mifugo yake??
Hana ni mikwara tuu ukimbananisha anatuna na milio unaweza vunjika kwa mbio.
Ila akikushika mguu au mkono kidole anaondoka nacho.
Hapo kumuu nimepitisha kitanzi ndani ya banda kwanza.
Yaani kwa mfano utege na mtego ule wa kufyatuka anase labda mguu wake,atautafuna huo mguu hadi ukatike aondoke zake bila huomguu
 
Nikiwa mdogo niliaminishwa kwamba ukisikia harufu ya ubwabwa kwenye msitu basi ujue Kuna majini hilo eneo sasa ikawa nikipita maeneo hayo natoka mbio sana .

Binadamu wabaya sana kumbe walinimezesha sumu?
 
Back
Top Bottom