SI KWELI Kanu ni Mnyama anayenukia harufu ya ubwabwa porini/vichakani

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Ndio huyu hata kipindi niko jkt tulifanikiwa kumwu asee
 
Jamii check rudini upya mkafanye utafiti wenu:huenda tumetofautiana jina la huyu mnyama ila mnyama anaenukia ubwabwa ni huyu.
 
Mimi ninavojua kuna aina fulani ya majani jamii ya nyasi ya maeneo ya porini hukoooo ndo huwa yanatoa harufu hiyoo
Kila mtu atasema lake.
Hata majani ya mkokomanga (yale machanga)ukitafuna kidogo yananukia ubwabwa
 
wa stendi taratibu mzee naona kama umepanic hiv baada ya uzi wako kupata neno "si kweli" punguza mzuka bro
Sawa
Ila ninachoamini ni hiki nilicholeta maana nimekamata mwenyewe harufu ipo na sio mara ya kwanza kunasa.
Labda tuu walichaleta wao ni aina ingine jamii hii hii.maana hata fisi wa mikumi hawafanani na wa serengeti au ni kama unavyoona chiter leopard au tiger.
 
wa stendi unataka kupotosha Umma Mzee.
Hawa jamii heck wamegoovle wakaletewa mnyama tofauti maelezo walopewa wakaleta kama walivyoambiwa.
Yaani ni kama unavyoona beberu kuna wanaonukia na ambao hawanukii ila ukweli ni huyu nimemkamata na anaukia ubwabwa kama hamuamini amini hawa jamii check na google yao.
 
Kubali tu kuwa ulichemka na uombe msamaha kwa kuuongopea umma. Umekazana ubwabwa ubwabwa. Mwanaume kwanza unaaanzaje kung'ang'ania hilo jina. Omba msamaha wananzengo.
 
Fungo ni mwingine ambae ni huyu nae nimenasa jana kwa jina jingine ni karasa
Bro wewe ni noma nahitaji unifundishe au uniuzie huo mtego nami niwanase watesi wangu, huku nilipo kuna yale yenye mikia mirefu mieupe yanatembea usiku tu, na yale mavicheche yanamikia mirefu huwa yanatembea solo mchana ni yana nitesa sana.
 
Wa stendi Unasema mnyama mwingine? Waliomuweka kwenye picha naona anafanana na huyo wako, pia kwenye hizo video hapo ukifungua mnyama ni huyo huyo na maelezo yako kama walivyoweka hapo.

Pia Kuna majibu ya mtaalamu wa wanyama hapo wote wawe wamekosea kasoro wewe?
 
Jamii check rudini upya mkafanye utafiti wenu:huenda tumetofautiana jina la huyu mnyama ila mnyama anaenukia ubwabwa ni huyu.
Sio kweli. Mnyama anayetoa harufu ya chakula Kama Ni kanu anafanya hivyo kwa lengo gani? Yani Kwanini atoe hiyo harufu? Tunajua wanyama au wadudu wanaofanya hivyo Ni kwa lengo la kuwavutia wanyama wanaopenda vyakula ili wawale
 
Yaani nifanye tafti zangu alafu niandike uzi hapa jamvini alafu moderator waje kusema sio kweli ,🙃🙃 hakika nitatafuta nauli nifike mpaka ofisini kwao na nimuhitaji mkuu wao maana ni Kama juhudi zangu ni bure
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…