Kanuni ya 10%: Jitahidi uishi

Gentlemen_

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2019
Posts
4,431
Reaction score
13,876
Hii rule ipo kwenye nyanja 5;
1. Kibinafsi
2. Kifamilia
3. Kiimani
4. Kikazi
5. Kimahusiano

Naomba nizungumzie kwa upande wa Kibinafsi na Kiimani.

Sisi binadamu tumekuja Duniani kuishi na kumuabudu Mwenyezi Mungu. Basi tujitahidi katika kuishi Tuishi kweli kweli na katika Kuabudu tuabudu Kwelikweli, 10 percent rule inataka hivyo.

Mimi binafsi kwa kila hela inayoingia natenga 10% ya kufarahia maisha (Starehe). Natenga 10% kwa ajili ya Sadaka na mambo ya kijamii, ambayo kiimani inaitwa Fungu la Kumi. 80% zingine nazielekeza katika mambo mengine ambayo sitayaweka wazi.

Nakushauri kama kijana mpambanaji kila hela unayopata basi tenga 20% pembeni. Ambayo 10% inaenda katika starehe na 10% inaenda katika Sadaka na Jamii. Hela yoyote upatayo iwe kihalali au kwa wizi hii rule itakusaidia sana.

Nakuasa kuanzia leo tekeleza 10% percent rule, watu wengi wanafariki/kufa bila kuishi maisha. Just enjoy maisha, tenga 10β„… kwa kila kipato chako kufurahia maisha hapa Duniani.

Haujui siku yako ya kufa utaacha hela nyingi (labda) watu watagombania na kuzitawanya. Muda huo wewe hujazifaidi hela zako. Faidi hela zako kabla haujafa, kifo kipo anytime.

Ukipata 100,000 tenga 10,000 ya starehe, tenga 10,000 nyingine ya Sadaka.

Ikumbukwe sadaka sio lazima uipeleke Msikitini au Kanisani, unaweza mpa mtu yeyote ambae unahisi itamsaidia kwa lolote. Faida yake ni kubwa kuliko hicho kidogo ulichotoa.

Kuna watu wanafanya kazi mpaka wanakufa hawajawahi kuishi.
 
Upo sahihi Sana
 
Ilo nalo neno
Wengine hatujawa na maisha mazuri Bado nafikir tukipata Hela tutafanya hizo starehe kma tukiwa hatujafa
Ila sadak ni muhimu Sana kwakweli
Yeah , Sadaka ina nguvu.

Then, ishu ya kufurahia MAISHA si lazima uwe na hela nyingi.. hapana. Unaweza kutumia hata hicho kdg ulichokuwa nacho ukajisuuzisha nafsi.

Kuna watu AKILI zao ni KUJENGA tu, mtu wa hivi akikukuta upo sehemu umeagiza mguu wa mbuzi unakula atakushangaa hapo kashapiga hesabu ya lori la Mchanga au mifuko 8 ya Cement.

Anajenga hamalizi miaka 10 ANAKUFA na bado ana deni la UJENZI.. Na Maisha hajayafaidi na MWANAUME mwenzie anahamia hapo na kumuoa MKE wake.
 
Hivi wanawake starehe yetu nn hasa au mm ndo mbahiliπŸ˜€πŸ˜€au ndo Sina Hela
Lamomy hebu njoo πŸ˜€
Mabaharia watakuja kukwambia eti raha yenu wanawake ni kupelekewa moto. Mabaharia siyo watu mpwa πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸƒπŸΏβ€β™‚οΈπŸƒπŸΏβ€β™‚οΈπŸƒπŸΏβ€β™‚οΈπŸƒπŸΏβ€β™‚οΈ
 
Watu wengi hatuupendi umaskini hiyo ndo sababu ukikumbuka kunasiku ulilala bila kula kwenda kuichezea laki 3 bar huwezi πŸ˜€ila tatizo tunatak.kuufuta umaskini Kwa haraka japo ni kitu kigumu, kusave kupitiliza nako ni kujichosha kilakitu kiwe na kiasi
 
Ah.. unasave wee mwisho wa siku unakufa na kuziacha. (Unatakiwa uwe na hayo mawazo ya kuwa, kuna siku UTAKUFA) ukiwaza hivyo hutoendekeza kubana bana. "Kitaliwa na Nyenyere".
 
Mabaharia watakuja kukwambia eti raha yenu kupelekewa moto. Mabaharia siyo watu mpwa πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸƒπŸΏβ€β™‚οΈπŸƒπŸΏβ€β™‚οΈπŸƒπŸΏβ€β™‚οΈπŸƒπŸΏβ€β™‚οΈ
Wameshasema mbona mpwa πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
wanawake wengi hatufanyi starehe tunadandia starehe za wanaume mwanamke kuspend 1 million aloitafuta ni kazi sanaπŸ˜‚πŸ˜‚
 
Wameshasema mbona mpwa πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
wanawake wengi hatufanyi starehe tunadandia starehe za wanaume mwanamke kuspend 1 million aloitafuta ni kazi sanaπŸ˜‚πŸ˜‚
Kuna mmoja jana nipo ferry natafuta DALADALA ya kwenda Mwenge, gari hakuna.

Ikaja BAJAJI nauli elfu 2 tuuuu. Yaan buku 2.
Mdada mzuri , classy ile mbaya najua elfu 2 anayo. Ila alijishauri sana anachungulia tu ktk bajaj kupanda anataka ila anawaza elfu 2 kulipia nauli wakati hapo ni jero tu kwa Daladala.

End of the day hakupanda ile bajaji.

Mtu wa hivi ukimuita aje muonane utaskia "Nirequestie Uber/Bolt daladala siwezi"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…