Kanuni ya haki ya msingi haikufuatwa kuwafukuza uanachama Halima Mdee na wenzake 18

Kanuni ya haki ya msingi haikufuatwa kuwafukuza uanachama Halima Mdee na wenzake 18

dndagula

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
1,602
Reaction score
1,650
Nimetafakari sana kisheria kuhusu kufukuzwa akina Mdee uanachama ninapata shida kidogo. Sina uhakika kama suala hili lilifanyika with due diligence. Hii ni kwa sababu kwa hali ya kawaida walipaswa waandikiwe barua ya mashtaka (kimaandishi)kuhusu makosa/tuhuma zinazowakabili na wapewe muda wa siku 14 kuzijibu na utetezi wao kuupeleka kwa mamlaka yao ya nidhamu ambayo ninaamini ni Kamati Kuu.

Aidha kamati kuu ingechambua utetezi wao kujiridhisha kuhusu tuhuma zao.

Vinginevyo kama kamati isingeridhika na utetezi ingehusisha pia kuunda Tume/kamati ya uchunguzi ili kuwahoji na kupata undani wa tuhuma hizo na kamati hiyo kuwasilisha mapendekezo yake kwa kamati kuu.

Hoja nyingine ya kujiuliza je kulikuwa na uharaka gani kuchukua hatua za kuwafukuza bila kuzingatia misingi ya haki "natural justice principle" kama ilivyo kwenye kanuni za nidhamu ili kukamilisha "administrative fairness procedures" kama kuna Sababu zenye madhara au athari mbaya zingeathiri chama chenu na kulazimisha kuchukua hatua za dharura bila mashtaka ya maandishi zilipaswa kujulikana wazi kwa wajumbe wa kikao hicho na watuhumiwa iwapo kama ndiyo ulikuwa msimamo wa kamati kuu ya CHADEMA.

Shauri hili likienda mahakamani kwa mazingira haya lina utata.

Tujadili kwa weledi
 
Nadhani nimeelewa. Iwapo hakuna wapinzani bungeni, watamlaumu nani mambo yakiharibika?
 
Barua ya kuwaita ilikua na mashtaka yaliokua yakiwakabili (Yaliokua dhidi yao).

Kuwafukuza uwanachama zimefuatwa sheria zote za msingi, swala la siku 14 au 21 ni procedure za kimahakama. Ila kwenye kamati, walipaswa;

1) Kufika kwanza ndio kuomba siku wanazo hitaji kujiandaa kwa utetezi.

2) Wangetoa sababu za msingi zilizo nje ya uwezo wao kutoweza kufika (Kama vile maradhi au majukumu mengine kama vile kuwa na kesi mahakamani kwa siku hio ilipangwa).

3) Wangetuma wawakilishi wao (Wanasheria wao) kuwawakilsha mbele ya kamati na kuomba tarehe nyingine ya kikao.

Kifupi, wao Covid-19 ndio waliodharau wito wa kamati, waliweza kuandika barua yneye sababu za mashiko zitakazo wapelekea kutofika kwenye kamati au wangetuma wawakilishi wao (wanasheria) kuwawakilisha kwa niaba yao. Ila hawakufanya hivo, na sio kwamba hawajui (Halima Mdee amesomea sheria), ila wamedharau.
 
mnh!

Kaa ukifahamu kwamba, Katiba ya JMT Ibara ya 78(1) imeeleza wazi kwamba Wabunge Wanawake wa Viti Maalumu wanapendekezwa na chama!!

Hapo kabla, kabla ya akina Halima kuapishwa Katibu Mkuu wa CHADEMA alitamka wazi kwamba yeye hajapeleka majina NEC!! Tamko lake hilo lilitokana na yeye kutuhumiwa kupeleka majina NEC!

Baada ya akina Halima kuapishwa, tuhuma dhidi ya Mnyika zikahamia kwa Mbowe na hasa baada ya Halima kutamka hadharani kwamba wamepata baraka za Mwenyekiti!

Kamati Kuu ikawaita Halima wakajieleze, obviously wakathibitishe madai kwamba walipata baraka za Mwenyekiti!

HAWAKUTOKEA kwenye kikao!!

Ukiangalia huo mtiririko wa matukio unapata picha moja kwamba, the so-called COVID 19 walikusaidia, mosi kuuchafua uongozi wa juu wa chama, na pia kuwagombanisha viongozi hao na wanachama kwa sababu ni kweli, both Mbowe na Mnyika kwa vipindi tofauti waliandamwa sana kuhusika na hujuma hizo!!

Katiba ya CHADEMA inasemaje kuhusu hayo?

Kuhusu Maadili ya Viongozi, Ibara ya 10.1 ( ix) inasema:-
Kiongozi asijihusishe au kushiriki na vikundi au vitendo vya kuchonganisha au kuzua migogoro ndani ya uongozi wa Chama au wanachama wake.
Kabla ya kugusa vifungu vingine, viongozi waliopo ndani ya COVID-19 wanakuwa wamevunja Maadili ya Uongozi kwa kwa kutaka kuchonganisha au kuzua mgogoro ndani ya uongozi na wanachama wake kama ilivyoonekana dhidi ya Mbowe na Mnyika!!

Hivi kuna serious crime kama hiyo?! Jibu NDIYO kama ilivyolezwa kwenye Ibara ya 3.a (iii) kwamba:-
Usaliti katika Chama litakuwa ndilo kosa kubwa kuliko yote kwa misingi ya kimaadili. Pamoja na mambo mengine, kosa la usaliti litajumuisha matendo kama Kupinga misimamo ya Chama hadharani na nje ya vikao vya Chama.
COVID-19 kwenda kuapishwa bungeni inakuwa ni kupinga msimamo wa chama hadharani na nje ya vikao vya chama, na kwa mujibu wa ibara husika, huo ni USALITI na Usaliti ndio kosa kubwa kuliko yote kwa misingi ya kimaadili!!

Wakati ibara ya mwanzo kabisa, yaani Ibara ya 10.1. (ix) hapo juu ilikuwa inawahusu viongozi peke yao, Ibara hiyo ya 3.a.iii inawahusu viongozi na wasio viongozi! Kwa maana nyingine, kundi ZIMA limetenda USALITI kwa mujibu wa Ibara ya 3... hiyo ni kwa Viongozi na Wanachama!!!

Pamoja na ibara hizo hapo juu, pia Viongozi wamevunja Ibara ya 10.1 (xi)

The question is: Adhabu ya Aina Gani na kwa Namna Gani!!!

Ibara ya 5.4.3 inasema mwanachama atakoma kuwa mwanachama kwa:-
Kuachishwa ama kufukuzwa na tawi lake ama ngazi nyingine ya Chama, kwa mujibu wa Katiba kwa kukosa sifa za kuendelea kuwa mwanachama ama kuwa na mwenendo usioendana na Itikadi, Falsafa, Madhumuni, Kanuni, Maadili na Sera za Chama. Mwanachama atakuwa na haki ya kukata rufaa kwa ngazi ya juu kama hakuridhika na adhabu hiyo.
Kwa maana nyingine, wala haina haja ya kuchoshana kuangalia Itikadi, Falsafa and other whatnot zinasema nini kwa sababu hapo juu tumeshaona wamefanya usaliti ambao ndio kosa kubwa kabisa la kimaadili kwa both, Viongozi na Wanachama!!

Kwa maana nyingine, haina haja ya kuchoshana kuangalia ikiwa akina Mdee walipaswa kuvuliwa uongozi kwa sababu so long as walistahili kuvuliwa uanachama kwa usaliti, automatically uongozi wao UNAKUFA kifo cha mende!!

Je, ni kweli kanuni ya Haki ya Kimsingi imevunjwa kama anavyodai mleta mada?! Ibara ya 5.4.4 inasema:-
Bila kuathiri kifungu 5.4.3 cha Katiba, Kamati Kuu inaweza kumwachisha ama kumfukuza mwanachama yeyote kwa utaratibu utakaopangwa na Kanuni za Chama
Nimepita pita huko mitaani na nimesikia COVID-19 wamefukuzwa uanachama na Kamati Kuu! Na hapo juu, inaonesha KK wanayo hayo mamlaka LAKINI, bila kuathiri Ibara ya 5.4.3 ambayo haijataja popote suala la Siku 14 uliloleta mtoa mada!!!

Now, dndagula umetoa wapi hayo mambo ya Siku 14?! Unaweza kutuwekea vifungu husika?!

NInachojua mimi, ofcourse kwa mujibu wa katiba, hao watu wanapewa siku 30 za kuweza kukata rufaa, na Ibara ya 6.5.5 inatoa room kwa mwanachama aliyewahi kufukuzwa uanachama kuomba kwa maandishi kurejeshwa chamani!!

Mkuu TUJITEGEMEE,

Nimeona kwenye thread moja uki-argue ikiwa wale uliowaita Mabwenyenye wa CHADEMA wamefuata katiba kufanya maamuzi!!!

Badala ya kuandika tena, jibu ni hilo hapo juu... NDIYOOOOOOOOOO, WAMEFUATA KATIBA, na hivyo kukuonesha what I said earlier is not impartial or even near cuz' y'all guys wanna make people believe CHADEMA violated their own constitution while spraying DDT to COVID-19 Virus!!
 
Barua ya kuwaita ilikua na mashtaka yaliokua yakiwakabili (Yaliokua dhidi yao).

Kuwafukuza uwanachama zimefuatwa sheria zote za msingi, swala la siku 14 au 21 ni procedure za kimahakama. Ila kwenye kamati, walipaswa;

1) Kufika kwanza ndio kuomba siku wanazo hitaji kujiandaa kwa utetezi.

2) Wangetoa sababu za msingi zilizo nje ya uwezo wao kutoweza kufika (Kama vile maradhi au majukumu mengine kama vile kuwa na kesi mahakamani kwa siku hio ilipangwa).

3) Wangetuma wawakilishi wao (Wanasheria wao) kuwawakilsha mbele ya kamati na kuomba tarehe nyingine ya kikao.

Kifupi, wao Covid-19 ndio waliodharau wito wa kamati, waliweza kuandika barua yneye sababu za mashiko zitakazo wapelekea kutofika kwenye kamati au wangetuma wawakilishi wao (wanasheria) kuwawakilisha kwa niaba yao. Ila hawakufanya hivo, na sio kwamba hawajui (Halima Mdee amesomea sheria), ila wamedharau.
Masuala ya kinidhamu yote huzingatia siku 14 kwenye ngazi ya quasi judicial organs.
 
Nimetafakari sana kisheria kuhusu kufukuzwa akina Mdee uanachama ninapata shida kidogo. Sina uhakika kama suala hili lilifanyika with due diligence. Hii ni kwa sababu kwa hali ya kawaida walipaswa waandikiwe barua ya mashtaka (kimaandishi)kuhusu makosa/tuhuma zinazowakabili na wapewe muda wa siku 14 kuzijibu na utetezi wao kuupeleka kwa mamlaka yao ya nidhamu ambayo ninaamini ni Kamati Kuu.

Aidha kamati kuu ingechambua utetezi wao kujiridhisha kuhusu tuhuma zao.

Vinginevyo kama kamati isingeridhika na utetezi ingehusisha pia kuunda Tume/kamati ya uchunguzi ili kuwahoji na kupata undani wa tuhuma hizo na kamati hiyo kuwasilisha mapendekezo yake kwa kamati kuu.

Hoja nyingine ya kujiuliza je kulikuwa na uharaka gani kuchukua hatua za kuwafukuza bila kuzingatia misingi ya haki "natural justice principle" kama ilivyo kwenye kanuni za nidhamu ili kukamilisha "administrative fairness procedures" kama kuna Sababu zenye madhara au athari mbaya zingeathiri chama chenu na kulazimisha kuchukua hatua za dharura bila mashtaka ya maandishi zilipaswa kujulikana wazi kwa wajumbe wa kikao hicho na watuhumiwa iwapo kama ndiyo ulikuwa msimamo wa kamati kuu ya CHADEMA.

Shauri hili likienda mahakamani kwa mazingira haya lina utata.

Tujadili kwa weledi
Acha kupotosha watu kwa kujifanya unajua sheria. Kwani principle of natural justice haina exceptions? Ndio maana ukikamatwa umeiba mtihani kama ni chuoni unafukuzwa papo kwa hapo.

Kama kuna dharula ni lazima utumie principle of natural justice? Mbona wao inasadikiwa hawakuwa na baraka za Cc ya Chadema! Unadhani sheri kuitwa ni msumeno wahenga walikosea?

In short sio kila disciplinary issue ina ulazima wa kufuata principles of natural justices.
 
Nimetafakari sana kisheria kuhusu kufukuzwa akina Mdee uanachama ninapata shida kidogo. Sina uhakika kama suala hili lilifanyika with due diligence. Hii ni kwa sababu kwa hali ya kawaida walipaswa waandikiwe barua ya mashtaka (kimaandishi)kuhusu makosa/tuhuma zinazowakabili na wapewe muda wa siku 14 kuzijibu na utetezi wao kuupeleka kwa mamlaka yao ya nidhamu ambayo ninaamini ni Kamati Kuu.

Aidha kamati kuu ingechambua utetezi wao kujiridhisha kuhusu tuhuma zao.

Vinginevyo kama kamati isingeridhika na utetezi ingehusisha pia kuunda Tume/kamati ya uchunguzi ili kuwahoji na kupata undani wa tuhuma hizo na kamati hiyo kuwasilisha mapendekezo yake kwa kamati kuu.

Hoja nyingine ya kujiuliza je kulikuwa na uharaka gani kuchukua hatua za kuwafukuza bila kuzingatia misingi ya haki "natural justice principle" kama ilivyo kwenye kanuni za nidhamu ili kukamilisha "administrative fairness procedures" kama kuna Sababu zenye madhara au athari mbaya zingeathiri chama chenu na kulazimisha kuchukua hatua za dharura bila mashtaka ya maandishi zilipaswa kujulikana wazi kwa wajumbe wa kikao hicho na watuhumiwa iwapo kama ndiyo ulikuwa msimamo wa kamati kuu ya CHADEMA.

Shauri hili likienda mahakamani kwa mazingira haya lina utata.

Tujadili kwa weledi
Hao wameshafukuzwa Chadema na wamekaribishwa CCM mchezo umekwisha

Vijana chapeni kazi!
 
Mbona Wao hawakuandika barua kutaarifu chama kuwa wanaenda kuapishwa dodoma kwa thupikyaaa.
 
Masuala ya kinidhamu yote huzingatia siku 14 kwenye ngazi ya quasi judicial organs.
"Quasi Judicial Organs" zinazofuata hicho kipengele ni ambazo zimeanzishwa kisheria, kwa mfano Labour Dispute Settlement, Industrial and Land Dispute Settlement.

Hizi Dispute Settlement za Vyama, zinakwenda kwa "MEMAT" ya kila chama.
 
Aliyepeleka majina ni nani ?
Mana haiwezekani kuwa wote waliyabeba kama Jeneza na kuyapeleka NEC.
Pamoja na kuwa walipewa wito rasmi wao hawakutaka kwenda kwenye kikao ambako kila mmoja angepata nafasi ya kujieleza, .
Nadhani itakuwa jambo jema kwako ukienda kuwauliza wao wenyewe.
 
Tambua jambo moja la msingi, kila taasisi ina taratibu zake za kujiendesha kupitia katiba zao, kwa suala la Chadema kina Mdee waliitwa kwenye kikao cha Kamati Kuu wakajieleze wakagoma, wote wakatoa sababu za udhuru zinazofanana, Kamati Kuu ikaamua kujadili suala lao na kulitolea uamuzi.

Hivyo, kutokana na Katiba yao bado wana nafasi ya kujitetea kwenye Baraza Kuu la chama, au waandike barua za kuomba msamaha, hizo ndio remedies zilizotolewa na Katiba yao.

Hii principle of natural justice kimsingi ipo, na nafasi hiyo walipewa, badala yake wote kwa pamoja wakaikataa kwa kutoa sababu za kitoto, ndio maana Kamati Kuu yao ikaamua kuwaadhibu, wale hawajaonewa, wanastahili adhabu iliyowafika.
 
Nimetafakari sana kisheria kuhusu kufukuzwa akina Mdee uanachama ninapata shida kidogo. Sina uhakika kama suala hili lilifanyika with due diligence. Hii ni kwa sababu kwa hali ya kawaida walipaswa waandikiwe barua ya mashtaka (kimaandishi)kuhusu makosa/tuhuma zinazowakabili na wapewe muda wa siku 14 kuzijibu na utetezi wao kuupeleka kwa mamlaka yao ya nidhamu ambayo ninaamini ni Kamati Kuu.

Aidha kamati kuu ingechambua utetezi wao kujiridhisha kuhusu tuhuma zao.

Vinginevyo kama kamati isingeridhika na utetezi ingehusisha pia kuunda Tume/kamati ya uchunguzi ili kuwahoji na kupata undani wa tuhuma hizo na kamati hiyo kuwasilisha mapendekezo yake kwa kamati kuu.

Hoja nyingine ya kujiuliza je kulikuwa na uharaka gani kuchukua hatua za kuwafukuza bila kuzingatia misingi ya haki "natural justice principle" kama ilivyo kwenye kanuni za nidhamu ili kukamilisha "administrative fairness procedures" kama kuna Sababu zenye madhara au athari mbaya zingeathiri chama chenu na kulazimisha kuchukua hatua za dharura bila mashtaka ya maandishi zilipaswa kujulikana wazi kwa wajumbe wa kikao hicho na watuhumiwa iwapo kama ndiyo ulikuwa msimamo wa kamati kuu ya CHADEMA.

Shauri hili likienda mahakamani kwa mazingira haya lina utata.

Tujadili kwa weledi

Kachero mbobezi alifanyiwa utaratibu huo kabla ya kufurushwa?

Mbona mnajitoa ufahamu hivyo?

Ilikuwa nia yenu kuwatumia wakiwa ndani ya CDM? Siyo kuwa wangechelewesha mno maendeleo?

Sasa hivi wako huru kuwa kwenu ili wasukume nanyi maendeleo kama betri siyo wazuie kama magunzi. Kama magunzi tochi haitawaka!
 
Pamoja na kuwa walipewa wito rasmi wao hawakutaka kwenda kwenye kikao ambako kila mmoja angepata nafasi ya kujieleza, .
Nadhani itakuwa jambo jema kwako ukienda kuwauliza wao wenyewe.

Hapana sikubaliani na wewe kwa hilo.
Tulitegemea kuona Chadema ikijengwa kwenya misingi ya Haki uhuru na Demokrasia ya kweli.

Hivi kwa hali hii Mbowe na Chadema ikifanikiwa kuingia madarakani huoni kuwa watu watanyongwa bila hata kufikishwa mahakamani?

Ni mara ngapi Wapinzani wakelalamika kuwa wanakakatwa kwa nguvu bila kuheshimiwa wala kusikilizwa uzuru wanaotoa mbele ya wakuu wa wilaya na hata polisi.

Je,tuendeleze mifumo hiyo isiyowasikiliza watu hata wanapojitetea kuwa wanataarifa ya kufanyiwa fujo na watu waliokua wameandakana na mabango yabkuwatukana na kuwaita COVID 19?
Je,huoni kuwa walikua na sababu ya msingi ukizingatia kuwa wale walikua tayari ni wabunge kwa nini hawakusikilizwa ombi lao kama waheshimiwa? Je,huoni ni mwendelezo ule ule wa kuwakakata wabunge kibabe kwa sababu tu ni wapinzani?

Ni mara Ngapi Tundu Lisu ametoa sababu za kutofika mahakamani na akasikilizwa bila kuhukumiwa moja kwa moja??
Je,huo sio utawala bora tunaoupigania ? Au akishakiuka kanuni za chama anaitwa msaliti na kuonekana kama panya tu asiye na maana ndani ya nyumba?
Mnakosea lakini hamtaki kujifunza mana mnadhani mnajua kila kitu.

Yesu aliwahi kuwaambia wayahudi kuwa wanajioma kuwa wao hawana dhambi hivyo hawana shida ya kumsikiliza jambo linalosababisha dhambi zao zinaenelea kukaa mana hawatubu.
 
Hapana sikubaliani na wewe kwa hilo.
Tulitegemea kuona Chadema ikijengwa kwenya misingi ya Haki uhuru na Demokrasia ya kweli.

Hivi kwa hali hii Mbowe na Chadema ikifanikiwa kuingia madarakani huoni kuwa watu watanyongwa bila hata kufikishwa mahakamani?

Ni mara ngapi Wapinzani wakelalamika kuwa wanakakatwa kwa nguvu bila kuheshimiwa wala kusikilizwa uzuru wanaotoa mbele ya wakuu wa wilaya na hata polisi.

Je,tuendeleze mifumo hiyo isiyowasikiliza watu hata wanapojitetea kuwa wanataarifa ya kufanyiwa fujo na watu waliokua wameandakana na mabango yabkuwatukana na kuwaita COVID 19?
Je,huoni kuwa walikua na sababu ya msingi ukizingatia kuwa wale walikua tayari ni wabunge kwa nini hawakusikilizwa ombi lao kama waheshimiwa? Je,huoni ni mwendelezo ule ule wa kuwakakata wabunge kibabe kwa sababu tu ni wapinzani?

Ni mara Ngapi Tundu Lisu ametoa sababu za kutofika mahakamani na akasikilizwa bila kuhukumiwa moja kwa moja??
Je,huo sio utawala bora tunaoupigania ? Au akishakiuka kanuni za chama anaitwa msaliti na kuonekana kama panya tu asiye na maana ndani ya nyumba?
Mnakosea lakini hamtaki kujifunza mana mnadhani mnajua kila kitu.

Yesu aliwahi kuwaambia wayahudi kuwa wanajioma kuwa wao hawana dhambi hivyo hawana shida ya kumsikiliza jambo linalosababisha dhambi zao zinaenelea kukaa mana hawatubu.
Ndugu yangu usipoteze muda na maandiko marefu ya bure.
Nenda tu ukapate maoni yao pia walikuwa na haraka ya nini mpaka kufikia kuapishiwa garage tena pasipo na 'siwa' kama kweli walikuwa na baraka za 'chama'.
 
Back
Top Bottom