Kanuni ya kukokotoa utajiri unaotakiwa kuwa nao kulingana na umri wako

Kanuni ya kukokotoa utajiri unaotakiwa kuwa nao kulingana na umri wako

Story za kijiweni tu hz, hakuna kanuni!
Obama kastaafu urais akiwa na miaka 55! Trump kawa Rais akiwa na miaka 70!
Boss wa Facebook, mark Zuckerberg, kawa bilionea akiwa na miaka 24! Bill gates kawa bilionea akiwa na miaka 40+!
Ulichokieleza bro! Ni, story za, dhahania tu,
Mkuu,
Mbona kama umedandia treni kwa mbele hivi?
Sioni uhusiano wa ulichoandika na nilichoandika.
Sikia mkuu, kama umechelewa, chukua hatua, makasiriko hayatasaidia.
 
Huenda hujakokotoa kwa usahihi.
Unaweza kutushirikisha namba zako hapa tuone? Kwa jumla tu, hatutaki kujua kuhusu wewe. Tupe umri, pato la mwaka na thamani ya utajiri wako kwa kuainisha mali na madeni.
Siwezi kutoa siri za utajiri na kipato changu.

Nina

*chombo cha moto,

*mali zisizohamishika,

*kazi yenye mshahara, na

*biashara.

Vyote hivi ndipo nimepatia jibu kwamba mimi ni moja ya matajiri.
 
Siwezi kutoa siri za utajiri na kipato changu.

Nina

*chombo cha moto,

*mali zisizohamishika,

*kazi yenye mshahara, na

*biashara.

Vyote hivi ndipo nimepatia jibu kwamba mimi ni moja ya matajiri.
Vizuri na hongera sana mkuu.
Endelea kutunza utajiri wako ili uendelee kuwa na manufaa kwa wengine kupitia kutoa fursa mbalimbali kwa wengine.
 
Rafiki yangu mpendwa,

Kwenye safari ya kujenga utajiri, watu huwa wanashangaza sana.

Wengi wanapokuwa na miaka 20 na 30 huwa wanaona ni mapema sana kwao kuhangaika na kujenga utajiri. Hivyo wanajiachia na kutumia kipato chao vile wanavyotaka.

Wanapofika miaka 40, wanajiona wameshachelewa kuanza kujenga utajiri, kwa sababu ya kipato wanachokuwa nacho na matumizi makubwa yanayotokana na majukumu wanayokuwa nayo.

Katika pande zote mbili, wanakuwa wamekosea. Kwenye kujenga utajiri huwa hakuna kuwahi wala kutokea. Bali kila wakati kwenye maisha ya mtu ni wakati sahihi kwake kujenga utajiri.

Wengi wamekuwa hawajui hili na hivyo kujikuta wakipoteza muda na kushindwa kujenga utajiri kwenye maisha yao.




Kwa bahati nzuri sana, ipo kanuni ya kukokotoa thamani ya utajiri ambao mtu anapaswa kuwa nao kulingana na umri wake na kipato chake. Kwa kanuni hii hakuna kuwahi wala kuchelewa, bali unapata uhalisia wa maisha yako.

Kanuni hiyo ni kama ifuatavyo; umri wako zidisha kwa pato la mwaka gawanya kwa 10.

Kwa mfano kama una miaka 40 na pato lako la mwaka ni milioni 12, kwa kanuni inakuwa; 40 X 12 / 10 = 48. Hivyo kwa mtu mwenye umri wa miaka 40 na ambaye pato lake la mwaka ni milioni 12, anapaswa kuwa na thamani ya utajiri wa milioni 48.

Baada ya kupata namba hiyo, mchezo haujaisha, bali sasa kuna kuitafsiri namba hiyo kwa kulinganisha na uhalisia wako.

Hatua inayofuata ni wewe kukokotoa thamani halisi ya utajiri wako. Unafanya hivyo kwa kujumlisha thamani ya mali zote unazomiliki na kutoa jumla ya madeni yote unayodaiwa.

Ukishapata thamani ya utajiri wako, unalinganisha na jibu ulilopata kwenye kukokotoa.

Kama thamani halisi ya utajiri wako ni mara mbili au zaidi ya jibu ulilokokotoa, upo kwenye njia ya kujenga utajiri mkubwa kwenye maisha yako. Endelea na hayo unayofanya, kwani utafika pazuri zaidi.

Na kama thamani halisi ya utajiri wako ni chini ya nusu ya jibu ulilokokotoa, upo kwenye njia ya umasikini. Unapaswa kuchukua hatua za haraka sana kutoka kwenye njia hiyo kwani inakupoteza.

Pale unapojikuta upo kwenye njia ya umasikini, hatua ya kwanza kuchukua ni kupunguza sana matumizi yako, kuwa bahili hasa.

Kisha chukua hatua ya kuongeza zaidi kipato chako, kuza kipato chako huku ukidhibiti matumizi yako yasizidi na kumeza kipato hicho.

Kwa kuanzia na hayo, utaweza kutoka kwenye umasikini ulionasa na kujenga utajiri utakaokupa uhuru wa maisha yako.

Kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA hapo chini nimefafanua zaidi kuhusu kanuni hii ya kukokotoa utajiri. Karibu ujifunze kwa kina zaidi kutoka kwenye kipindi ili ujue pale ulipo sasa na hatua za kuchukua ili kwenda mbali zaidi.


View: https://www.youtube.com/watch?v=3K1TK0cHewI

Nenda kayaweke haya uliyojifunza kwenye matendo ili uweze kujenga mafanikio makubwa kwenye maisha yako kwa kuiishi kila siku yako kwa mafanikio makubwa.

Kutoka kwa rafiki yako anayekupenda na kukujali sana,

Kocha Dr. Makirita Amani,

Daktari |Mwandishi |Kocha |Mkufunzi

+255 678 977 007 / amakirita@gmail.com

www.amkamtanzania.com

MUHIMU; Rafiki, nikushukuru kwa kuendelea pamoja kupitia mafunzo haya ninayotoa. Karibu kwenye huduma zaidi ninazotoa, kuanzia 1. VITABU, 2. NGUVU YA BUKU, 3. KISIMA CHA MAARIFA, 4. CHUO CHA MAUZO na 5. BILIONEA MAFUNZONI. Kupata maelezo ya huduma hizi, tumia mawasiliano yaliyopo hapo juu. Karibu sana.

Ukisoma sana unakuwa mjinga yani mtu anakaa chini anachukua karamu na karatasi anaanza andika nadharia zake ambazo ni hewa na wala hazipimiki anasahau utajiri ni bahati wala siyo juhudi na marifa ingekuwa utajiri juhudi na marifa jamii yetu matajiri wangekuwa wengi sana tena sana
 
Nashkuru mungu maana mpaka sasa namiliki chombo cha moto ambae ni birika la kisasa la kuuzia al kasusu na kahawa. Pia namiliki usafiri kwa shughuli zangu phoenix new model bila kusahau ghetto la msonge.
 
Kama umechagua kuwa masikini, hakuna anayeweza kukulazimisha kuwa tajiri.
Na itakuwa vyema kama utakaa mbali na haya mambo ya utajiri, ili uendelee kuteseka vizuri na umasikini wako.
Kila la kheri.
Heheheh....ukichukulia kila kitu serious humu Jf, utabandua kucha nyuma ya keybord....
Nawe kila la kheri.
 
Ukisoma sana unakuwa mjinga yani mtu anakaa chini anachukua karamu na karatasi anaanza andika nadharia zake ambazo ni hewa na wala hazipimiki anasahau utajiri ni bahati wala siyo juhudi na marifa ingekuwa utajiri juhudi na marifa jamii yetu matajiri wangekuwa wengi sana tena sana
Kusema utajiri ni bahati ndiyo nimeona akili yako imekorogeka.
Ni kweli nilichoshirikisha hapa chaweza kuwa nadharia, ambayo haiwezi kufanya kazi kwa watu wote.
Lakini kwamba utajiri ni bahati, mbona wanaoshinda bahati nasibu au kurithi mali wanapoteza zote?
Kuna zaidi ya bahati mkuu, usikaze shingo, jifunze na uchukue hatua sahihi.
 
Utajiri siyo wa kila mtu kiongozi, ila maisha bora ndio yanawezekana kwa kila mtu endapo atajituma na kuwa na nidhamu ya maisha, naposema maisha naimanisha jinsi tunavyotakiwa tuishi kila siku nikiwa na maana ili tuishi yapaswa tufanye kazi yoyote ile harari yenye kuweza kukupatia kipato cha kukidhi mahitaji yako ya kila siku yani chakula, maradhi, na mavazi, mtu yoyote anayejituma kufanya kazi basi huweza kukizi hayo mahitaji ya msingi, pia aijue jamii yake inaitaji nini hasa upendo na amani kwani ukiwa na upendo na amani utakubalika na jamii yako na pia siraha kubwa ya mafanikio kimaisha ni uaminifu sasa hivi vitu vinawezekana kujifunza na kuvisimamia na kukuwezesha ukaishi kwa furaha kabisa katika jamii yako ila siyo utajiri bro utajiri si wa kila mtu

Utajiri sawa na mafanikio ya kipaji siyo kila mwenye kipaji anafanikiwa wanaofanikiwa ni wale wateule ambao Mungu kamua ikiwa Mungu ajamua pambana uwezavyo utakuwa daraja tu kwa wengine kwaiyo ni vizuri tukajitathimi je wewe wa fungu gani siyo kulishana matango pori kuwa ukifanya hivi utakuwa tajiri wewe acha ndio maana umesema hapo kuwa mbona wanaoshinda bahati nasibu hawawi matajiri yes kwanini wao si wateule wa kuwa matajiri wao ni wateule wa bahati nasibu bro utajiri ni issue nyingine na kuupata ikiwa wewe mteule haitaji nguvu ngoja nikupe mfano wa uteule

Marehemu magufuli kipindi anafundisha shule uko kina marehemu Lowasa kina marehemu Membe walikuwa kwenye system walijua A to Z za jinsi na njia za kuwa Rais nchi hii kina Mzee marechela nk walipambana wawezavyo kuutaka Urais wa inchi japo kujua kila kitu na kuwa na kila kitu ila hawakuwa wateule wa Mungu ila akaja Magufuli from no where kawa Rais, haya mama yetu huyu miaka kumi iliyopita sidhani kama aliwaza kuja kuwa Rais ila kwakua naye ni mteule wa Mungu kawa Rais

Sasa utajiri nao upo hivyo ila mafanikio ya maisha hayapo hivyo mafanikio yenyewe ndio yanaitaji ujitume siyo utajiri bro, nakupa mfano mwingine kuna watu leo hii wapo machimboni wanatafuta madini wawe matajiri na leo hii pale hospital amana kuna mama anajifungua mtoto baada ya miaka 20 uyu mtoto aliyezaliwa leo ataenda machimboni atamkuta yule mchimbaji ambaye yupo mgodini zaidi ya miaka 20 anachimba ila ana mafanikio tu hana utajiri ila uyu dogo anakaa mwaka mmoja tu shimo linaitika anakuwa tajiri kwanini ni mteule wa Mungu kuwa aje kuwa tajiri
Kusema utajiri ni bahati ndiyo nimeona akili yako imekorogeka.
Ni kweli nilichoshirikisha hapa chaweza kuwa nadharia, ambayo haiwezi kufanya kazi kwa watu wote.
Lakini kwamba utajiri ni bahati, mbona wanaoshinda bahati nasibu au kurithi mali wanapoteza zote?
Kuna zaidi ya bahati mkuu, usikaze shingo, jifunze na uchukue hatua sahihi.
 
Utajiri siyo wa kila mtu kiongozi, ila maisha bora ndio yanawezekana kwa kila mtu endapo atajituma na kuwa na nidhamu ya maisha, naposema maisha naimanisha jinsi tunavyotakiwa tuishi kila siku nikiwa na maana ili tuishi yapaswa tufanye kazi yoyote ile harari yenye kuweza kukupatia kipato cha kukidhi mahitaji yako ya kila siku yani chakula, maradhi, na mavazi, mtu yoyote anayejituma kufanya kazi basi huweza kukizi hayo mahitaji ya msingi, pia aijue jamii yake inaitaji nini hasa upendo na amani kwani ukiwa na upendo na amani utakubalika na jamii yako na pia siraha kubwa ya mafanikio kimaisha ni uaminifu sasa hivi vitu vinawezekana kujifunza na kuvisimamia na kukuwezesha ukaishi kwa furaha kabisa katika jamii yako ila siyo utajiri bro utajiri si wa kila mtu

Utajiri sawa na mafanikio ya kipaji siyo kila mwenye kipaji anafanikiwa wanaofanikiwa ni wale wateule ambao Mungu kamua ikiwa Mungu ajamua pambana uwezavyo utakuwa daraja tu kwa wengine kwaiyo ni vizuri tukajitathimi je wewe wa fungu gani siyo kulishana matango pori kuwa ukifanya hivi utakuwa tajiri wewe acha ndio maana umesema hapo kuwa mbona wanaoshinda bahati nasibu hawawi matajiri yes kwanini wao si wateule wa kuwa matajiri wao ni wateule wa bahati nasibu bro utajiri ni issue nyingine na kuupata ikiwa wewe mteule haitaji nguvu ngoja nikupe mfano wa uteule

Marehemu magufuli kipindi anafundisha shule uko kina marehemu Lowasa kina marehemu Membe walikuwa kwenye system walijua A to Z za jinsi na njia za kuwa Rais nchi hii kina Mzee marechela nk walipambana wawezavyo kuutaka Urais wa inchi japo kujua kila kitu na kuwa na kila kitu ila hawakuwa wateule wa Mungu ila akaja Magufuli from no where kawa Rais, haya mama yetu huyu miaka kumi iliyopita sidhani kama aliwaza kuja kuwa Rais ila kwakua naye ni mteule wa Mungu kawa Rais

Sasa utajiri nao upo hivyo ila mafanikio ya maisha hayapo hivyo mafanikio yenyewe ndio yanaitaji ujitume siyo utajiri bro, nakupa mfano mwingine kuna watu leo hii wapo machimboni wanatafuta madini wawe matajiri na leo hii pale hospital amana kuna mama anajifungua mtoto baada ya miaka 20 uyu mtoto aliyezaliwa leo ataenda machimboni atamkuta yule mchimbaji ambaye yupo mgodini zaidi ya miaka 20 anachimba ila ana mafanikio tu hana utajiri ila uyu dogo anakaa mwaka mmoja tu shimo linaitika anakuwa tajiri kwanini ni mteule wa Mungu kuwa aje kuwa tajiri
Nadhani amekuelewa
 
Utajiri siyo wa kila mtu kiongozi, ila maisha bora ndio yanawezekana kwa kila mtu endapo atajituma na kuwa na nidhamu ya maisha, naposema maisha naimanisha jinsi tunavyotakiwa tuishi kila siku nikiwa na maana ili tuishi yapaswa tufanye kazi yoyote ile harari yenye kuweza kukupatia kipato cha kukidhi mahitaji yako ya kila siku yani chakula, maradhi, na mavazi, mtu yoyote anayejituma kufanya kazi basi huweza kukizi hayo mahitaji ya msingi, pia aijue jamii yake inaitaji nini hasa upendo na amani kwani ukiwa na upendo na amani utakubalika na jamii yako na pia siraha kubwa ya mafanikio kimaisha ni uaminifu sasa hivi vitu vinawezekana kujifunza na kuvisimamia na kukuwezesha ukaishi kwa furaha kabisa katika jamii yako ila siyo utajiri bro utajiri si wa kila mtu
Huu sasa ndiyo utajiri ninaouzungumzia mimi, siyo wa kuwa kwenye orodha au kuwashinda wengine.
Utajiri ninaofundisha mimi na ambao nataka kila mtu aupate maana yake ni hii; KUWEZA KUISHI MAISHA YAKO KWA NAMNA UNAVYOTAKA WEWE BILA YA KULAZIMIKA KUFANYA AMBACHO HUTAKI KUFANYA.
Ni hivyo tu, mengine ni mbwembwe.
Kwa hiyo narudia kusema Utajiri siyo tu unawezekana kwa kila mtu, bali ni haki ya kila mtu.
Tukirudi kwenye kanuni niliyoshirikisha, ili uweze kuishi maisha yako kwa uhuru bila kulazimika kufanya kitu usichopenda, unapaswa kuwa na uwekezaji ambao unaweza kukuingizia kipato cha kutosha kuendesha maisha yako hata kama hufanyi kazi moja kwa moja.
Hivyo basi, kwa kipato chako na umri wako, unapaswa kuwa unafanya uwekezaji ambao thamani yake inaendana kwa kanuni hiyo.
 
Bongo ishu ni channel sio umri😂, ukiwa kwenye line sahihi hauhitaji hata formula yeyote. Hata ukiwa 65 miaka 5 tu inatosha kusomba lumbesa za dollar.
Kwanza kwanini amegawanya kwa kumi ??kumi inawakilisha nini???atupe validation ya hiyo formulae

Motivesheno spika miyayusho sana.
 
Asante kwa mrejesho mkuu.
10 ni factor tu kwenye formula.
Formula hii sijaitunga mwenyewe, bali imetoka kwenye kitabu cha THE MILLIONAIRE NEXT DOOR, kilichoandikwa na Thomas J. Stanley na William D. Danko.
Karibu.

Sasa kwanini hauweki hizo acknowledgment kwenye Uzi?

Pia ni USD, GBP au TZS?
Na hiyo 12 unayozidisha na umri wako ni kitu Gani, kwamba makadirio ya kipato Cha 1M Kwa mwezi?
 
Huenda hujakokotoa kwa usahihi.
Unaweza kutushirikisha namba zako hapa tuone? Kwa jumla tu, hatutaki kujua kuhusu wewe. Tupe umri, pato la mwaka na thamani ya utajiri wako kwa kuainisha mali na madeni.

Kwanini wewe usiweke hapo kama mfano wa utajiri wako?

Pia hii inaongelea utajiri wa upande mmoja, kipato.

Kuna mambo mengine kama afya, utulivu wa akili, mahusiano n.k yanathamani kubwa pia.
 
Asante kwa mrejesho mkuu.
10 ni factor tu kwenye formula.
Formula hii sijaitunga mwenyewe, bali imetoka kwenye kitabu cha THE MILLIONAIRE NEXT DOOR, kilichoandikwa na Thomas J. Stanley na William D. Danko.
Karibu.
Mwandishi wa kitabu Thomas J. Stanley yeye aliwaza vipi kutumia 10 na si 15, 20, 30, n.k.
Je, hiyo formula ni universal?

"Maisha hayana formula". "Utajili ni kitu uncertain"
 
Kwanza kwanini amegawanya kwa kumi ??kumi inawakilisha nini???atupe validation ya hiyo formulae

Motivesheno spika miyayusho sana.
Ndio maana ukisoma sana unakuwa mjinga uko tranquility kama nyumbani ujakuta mali basi jitoe shiriki sana shughuli za wenzako ila utakapokuwa na jambo lako wenzako waje kwaiyo unajitoa uku u afanya kazi kupata pesa ukodi shamba ukupata pesa unakodi shamba kubwa msimu wa kilimo ukifika unaita wenzako ulioenda wasaidia kulima mashamba yao zamani wanakuja wanakusaidia hapo una imani kuwa msimo wa mavuno navuna mavun9 yakiwa mazuri nanunua shamba langu

Kweli kijana akivuna ananua shamba lake anaweka malengo mwakani nalima nikivuna nikiuza naoa kweli anavuna anaoa anaweka malengo mwakani nalima nikivuna naunua mifugo kweli anaunua mifugo anaweka malengo tena mwakani nikivyna nauza mifugo naongeza shamba na kweli anavuna anafanya hivyo anaweka tena malengo mwakani nikivuna najenga kwakua ana aridhi kubwa kweli anajenga anaweka tena malengo umeona sijui yani mipango tu sasa hawa wenye shule Mungu anajua yeye
 
Back
Top Bottom