Elections 2010 Kanuni za Uchaguzi 2010 na mgogoro wa Sheria ya Gharama

Elections 2010 Kanuni za Uchaguzi 2010 na mgogoro wa Sheria ya Gharama

Status
Not open for further replies.
mkuu ikulu yetu na watendaji wake wengi hawako makini na kazi zao zilizowapeleka pale wanachofanya ni hicho tu(kamuhogo)lakini pia hakuna wa kuwasahisha make wengi wao ni haohao

Sio Watendaji tu hata huyo Rais mwenyewe hayuko makini maana inaelekea hakusoma alichokuwa anasaini vinginevyo angeshtuka kabla ya kuweka wino.
 
Ikulu kuna matatizo ya banyamulenge na mkolomi Roastum Aziz.
 
Labda tu tuseme kwamba Rais hakusoma huo mswada; lakini kusema kwamba watu wa ikulu hawana umakini mimi kwa hili siamini. Yawezekana watu wa ikulu haohao wakishirikiana na baadhi ya vigogo ndio waliochomeka hayo mambo mageni. Wachomekaji lazima wawe ni watu wajanja, walijua fika wanachokifanya. Kumbe kuwalaumu watu wa ikulu kwamba hawakuwa makini si sawa vinginevo tuna uhakika hao wana-ikulu si washiriki wa hiyo mbinu chafu, tukimtoa Rais.
 
Wa TZ huwa tunafanya kazi kimazoea kuanzia ngazi ya chini mpaka ngazi za juu hapa inatakiwa mkoloni arudi alekebishe.
 
Uvumbuzi huu wa haya makosa umemwongezea Credit Dr. Slaa kuwa ni mtu makini na anayesoma nyaraka mstari kwa mstari na kupambanua. Wale wanaosaini mikataba kwa niaba ya nchi wangekuwa wana umakini wa walao 25% ya Dr Slaa mnadhani nchi hii ingekuwa na mikataba ya kijinga kama tuliyonayo sasa hivi.
Tumpe haki yake Dr kwa kumpongeza na kutambua utayari wake. HUYU NDIO MFANO WA WABUNGE WANAOTAKIWA KUWEPO BILA KUJALI ANATOKA CHAMA GANI.
 
Naomba kuuliza, hivi muswada ukishapitishwa na bunge, nani anachukua wajibu wa kuuchapa na kumpelekea rais kuweka sahihi?

Nini wajibu wa spika na team yake kwenye hili? Nilikuwa nategemea bunge likipitisha basi ofisi ya spika ichukue madaraka ya kuchapa na kuufikisha kwa rais.
 
Labda tu tuseme kwamba Rais hakusoma huo mswada; lakini kusema kwamba watu wa ikulu hawana umakini mimi kwa hili siamini. Yawezekana watu wa ikulu haohao wakishirikiana na baadhi ya vigogo ndio waliochomeka hayo mambo mageni. Wachomekaji lazima wawe ni watu wajanja, walijua fika wanachokifanya. Kumbe kuwalaumu watu wa ikulu kwamba hawakuwa makini si sawa vinginevo tuna uhakika hao wana-ikulu si washiriki wa hiyo mbinu chafu, tukimtoa Rais.

mkuu hivi unafikiri rais atapitia kiukamilifu mambo mangapi?? tena ya nchi nzima na mengine ya kimataifa?? usifanye mchezo mkuu!! ndio maana akawekewa wasaidizi ... laiti kama kila kitu angekuwa anafanya yeye basi nadhani angeshakuwa chizi!!
 
Sio Watendaji tu hata huyo Rais mwenyewe hayuko makini maana inaelekea hakusoma alichokuwa anasaini vinginevyo angeshtuka kabla ya kuweka wino.
BAK,

Unataka rais asome sheria zote zinazopitishwa na bunge? Hilo haliwezekani, muda atautoa wapi? Ndio maana ana wasaidizi kibao wanaolipwa na serikali.

Hao ndio wanatakiwa kusoma na kumpa briefing rais. Wakichemsha na rais anakuwa amechemsha maana yeye ndiye kawachagua ili wamsaidie kazi.

Kwenye hili kuna watu wengi sana wamechemsha, kuanzia kule kwa Spika mpaka Ikulu kwenyewe.
 
Mheshimiwa Dr. Slaa, wewe ni kiongozi, Mbunge wetu, huwezi kututamkia "Watanzania hawaelewi issues"!

Kisiasa inaonyesha hujali hata kutuonyesha unanyenyekea kwa tuliokupa taadhima ya kutuongoza, na ulivyo mwepesi kutumia lugha za kujumuisha watu jumla jumla na kuwashusha. Tafadhali Mheshimiwa.

Baadhi ya Wananchi tunadai kutodharauliwa na Waheshimiwa.

Ulitaka utamkiwe kitu gani?Unapenda kunyenyekewa ili iweje?Issue hapa ni kutokuwa makini kwa bunge zima pamoja na ikulu....Hivi ngoja nikuulize swali,kuna dharau kwa mtanzania kama kusaini mikataba mibovu na sheria bila kuwa waangalifu ama kujali maslahi ya Taifa?

Licha ya kwamba sijaona pahala Dr Slaa alipoonyesha dharau,bado unatakiwa uelewe kuna tofauti kati ya watu wanaoona situations first hand on the ground,na sisi tulioko mtandaoni,mwananchi anasema anapewa rushwa kwasababu anapendwa na kiongozi anayempa rushwa,mwananchi hajali kinachofanywa na viongozi wakati wa utekelezaji ama maamuzi muhimu ya Taifa, mwananchi ana assume kiongozi ana nia nzuri wakati wote na anaamini kabisa kuwa rushwa ni ishara ya upendo! Na hivyo hana haja ya kufuatilia mikataba wala sheria mbovu zinazopitishwa na kusainiwa kwa mbwembwe kwasababu mtu anayekupenda na kuongea kwa unyenyekevu hawezi kuwa mtu mbaya ama fisadi....!

Kama tuna kiongozi anayeangalia na kufuatilia hayo kwa niaba yetu sisi wananchi kama anavyofanya Dr Slaa,basi huyo ndiye kiongozi anayetuheshimu sisi wananchi na hivyo ndo kiongozi tunayemuhitaji.

Hongera Mh Dr Slaa kwa kufanya yale wananchi waliyokutuma kuyafanya,na pia hongera kwa kujali maslahi ya wananchi wote licha ya uelewa wetu "mbovu"

Tunahitaji viongozi makini wa caliber yako ili tuweze kuumaliza ufisadi kwa maslahi ya Taifa letu na kizazi kijacho....May God bless you indeed!
 
Hivi haya mapungufu mbona yanatokea sana katika kipindi hiki cha huyu mkulu?
Binti Sayuni, ktk familia yeyote, baba akiwa kalewa wakati wote na mama anapiga ukahaba saa zote unategemea watoto watafanya nini? Ndivyo ilivyo wa wasaidizi wa jumba kuu.
 
mkuu hivi unafikiri rais atapitia kiukamilifu mambo mangapi?? tena ya nchi nzima na mengine ya kimataifa?? usifanye mchezo mkuu!! ndio maana akawekewa wasaidizi ... laiti kama kila kitu angekuwa anafanya yeye basi nadhani angeshakuwa chizi!!
...acha kutoa excuse ya kijinga na rojo rojo wewe,huwezi kuongoza nchi kwa kubase kwenye ushauri na briefings!! yeye mwenyewe rais lazima ajue mambo yote kama yeye!!! asome miswaada ya sheria kikamilifu na kufuatilia mijadala ya bunge na kile wanachoamua yeye mwenyewe!! ndio maana watz tunarahisisha mambo holela holela tu, URAIS siyo briefings!!!! nchi nyingine kiongozi lazima athibitishe kwa dhati kwamba anafaa kwa kazi hiyo anayotaka!!!
RAIS NDIO ANA MAKOSA!!!!!!!!siku nyingine basi atavaa sketi atoke kwa public appearance kwa vile tu washauri wake wamwemshauri avae hivyo siku hiyo!
 
Walijua haya:
1)Kwamba muswada una mushkeli...
2)Rais hayuko makini
Kwa hiyo wakamsainisha mbele ya waandishi asije kukana saini yake baadae...HAIJAWAHI TOKEA katika nchi hii rais kusaini muswada kwa mbwembwe


Mpwa wataka kuniambia Mkulu huwa hapitii hayo makablasha kabla ya kusaini? au ndio kamtindo kake na ndio maana wana mwingiza mkenge? na walisha msoma kwa hilo?

Je sasa nani anatakiwa kuhakiki hayo makablasha kabla ya mkulu kumwaga wino wake?

Enzi za mwalimu JKN ukimleteaa issue tu kuhusu kitu fulani anakuambia nisha ipata 2hours ago unajiuliza vipi huyu mtu sasa mkulu tulie nae ni mpaka ameisha mwaga wino ndio anakuja shtuliwa tena na watu walioko nje ya IKULU hii si aibu kwa kiongozi mkubwa kama yeye na inaashiria si makini katika kuperuuuzii na kudadisi makablasha ya IKULU
 
Labda tu tuseme kwamba Rais hakusoma huo mswada; lakini kusema kwamba watu wa ikulu hawana umakini mimi kwa hili siamini. Yawezekana watu wa ikulu haohao wakishirikiana na baadhi ya vigogo ndio waliochomeka hayo mambo mageni. Wachomekaji lazima wawe ni watu wajanja, walijua fika wanachokifanya. Kumbe kuwalaumu watu wa ikulu kwamba hawakuwa makini si sawa vinginevo tuna uhakika hao wana-ikulu si washiriki wa hiyo mbinu chafu, tukimtoa Rais.

Babuyao!!!!

1:Bunge huwa wanamkabidhi nani huo mswada huko IKULU?

2:Je pale Mkulu anapotaka kuusaini mswada wowote ule hakuni mtu wa kutoka bunge na kufanya last cross check na kuhakiki kuwa ni kweli ndio ule mswada aliouwakilisha?
 
Nadhani, haya yote yamekuwa yakitokea. the difference is only that..this time CHADEMA as opposition has a stake in it and akina Dr. Slaa were reading it carefully between the lines and were able to interpret each and every line on the adverse effect it will during the coming elections.
For sure if you go through all other muswadas there must be some changes which they may call it minor but have been changed after the parliament meeting. We don't have legislators eager to do proof reading of what has been enacted as the law compared to the parliament hansard, etc.
The problem for JK is that he is becoming also too transparent compared to his predicessors and he want the public to be informed of everything for reasons ofcourse well known to him!
 


Mpwa wataka kuniambia Mkulu huwa hapitii hayo makablasha kabla ya kusaini? au ndio kamtindo kake na ndio maana wana mwingiza mkenge? na walisha msoma kwa hilo?

Je sasa nani anatakiwa kuhakiki hayo makablasha kabla ya mkulu kumwaga wino wake?

Kumbuka kashfa ya kutoa ambulance hakuna aliyewajibishwa.....huu mwenendo wa kubebana




Enzi za mwalimu JKN ukimleteaa issue tu kuhusu kitu fulani anakuambia nisha ipata 2hours ago unajiuliza vipi huyu mtu sasa mkulu tulie nae ni mpaka ameisha mwaga wino ndio anakuja shtuliwa tena na watu walioko nje ya IKULU hii si aibu kwa kiongozi mkubwa kama yeye na inaashiria si makini katika kuperuuuzii na kudadisi makablasha ya IKULU

JKN alikuwa na watu ikulu ambao ni chapa kazi na alikuwa na watu wa usalama kila kona ikawa inamsaidia kujua kila kitu kiendeleacho
 
Kumbuka kashfa ya kutoa ambulance hakuna aliyewajibishwa.....huu mwenendo wa kubebana




JKN alikuwa na watu ikulu ambao ni chapa kazi na alikuwa na watu wa usalama kila kona ikawa inamsaidia kujua kila kitu kiendeleacho

Sasa hivi hakuna kubebana wala kupakatana.
 
Tahariri ya Tanzania Daima

WIKI chache zilizopita Rais Jakaya Kikwete alisaini Sheria ya Matumizi ya Gharama za Uchaguzi katika viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam. Sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali, wakiwamo mawaziri, mabalozi, viongozi wa dini na viongozi wa vyama vya siasa.

Kwa mara ya kwanza, Tanzania iliandika historia katika nchi za Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kusaini sheria hiyo ambayo imelenga kudhibiti vitendo viovu wakati wa uchaguzi.

Tulifurahishwa na uamuzi wa ujio wa sheria hii, tukiamini itapunguza mianya ya rushwa, hasa kwa kurubuni wapiga kura katika maeneo ya vijijini, ambako wananchi wengi haki zao hununuliwa.

Jambo la kusikitisha ambalo sasa limeanza kuibua hisia miongoni mwa jamii ni hatua ya Rais Kikwete kusaini sheria ambayo baadhi ya vipengele vyake havikupitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano.

Tunaamini kitu chochote ambacho kinafikia hatua ya kusainiwa na rais huwa kimekamilika, sasa tumeshtushwa kusikia kuna baadhi ya vipengele vimechomekwa kinyamela.

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, alibaini kuchomekwa kipengele kinyamela katika mjadala uliopelekwa bungeni na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, aliyetaka mabadiliko ya pendekezo la serikali kwa kifungu 7 (2).

Alisema katika kifungu hicho, Chenge alitaka makundi ya sanaa yaingizwe badala ya neno ‘voters'.

Tunasema kilio cha Dk. Slaa kinaweza kuwa na ukweli kama wahusika wataamua kuchukua uamuzi wa kina wa kupitia kipengele kimoja baada ya kingine.

Kipengele kinachodaiwa kuchomekwa kwenye sheria iliyosainiwa na Rais Kikwete ni cha 7 (3), ambacho hakikuwamo kabisa kwenye muswada huo bungeni.

Tukiwa chombo huru, tunasema kama kweli kuna watu waliojaribu kuchomeka kipengele hicho kwa manufaa yao binafsi wanapaswa kusakwa kwa udi na uvumba ili kufuta aibu hii.

Aibu hii ya kumgeuza mkuu wa nchi kuwa mtoto, haikubaliki. Tunatoa wito kwa mamlaka zinazohusika kuwawajibisha wale ambao wametia mikono yao kwenye kipengele hicho.

Tunachukua fursa hii kuwataka Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Spika wa Bunge kuwaomba radhi rais na umma wa Watanzania kutokana na aibu hii ambayo haikubaliki.

Tunatumia fursa hii kuzitaka ofisi hizo mbili kurudisha sheria hiyo bungeni itenguliwe, ili iweze kujadiliwa upya kwa manufaa ya taifa na si kikundi cha watu wachache.

Kama imefikia hatua rais kuchomekewa vipengele kama hivi, Watanzania tutegemee nini katika sheria nyingine ambazo husaini ndani ya ofisi yake?

Sisi Tanzania Daima tunasema umefika wakati sasa wa kuhakikisha wale wote waliohusika kumdanganya rais wanaondolewa kwenye nafasi za kazi wanazoshikilia ili kujenga nidhamu kwa watu wengine.

Tunamalizia kwa kusema rais ana majukumu mengi, lakini wasaidizi wake wanapofikia hatua ya kumdangaya, inatia shaka na kuondoa imani mbele ya jamii.
 
Hemed Kivuyo, Arusha

MBUNGE wa Karatu Dk Wilbrod Slaa, amewashukia spika wa bunge, Samuel Sitta na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Warema kuhusu rais kudanganywa katika sheria ya matumizi ya fedha katika uchaguzi.

Kutokana na hali hiyo,amewataka waache kutoa majibu mepesi kwenye hoja nzito tena bila kufanya utafiti.

Dk Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ametaka sheria hiyo irudishwe bungeni katika kikao cha 19 kinachotarajiwa kuanza Aprili ili kifungu ambacho rais Jakaya Kikwete amekisaini bila kujadiliwa bungeni, kiondolewe.

Katika barua yake aliyomwandikia spika wa bunge kulalamikia kauli hizo, Dk Slaa alisema kifungu hicho namba 7(3) cha sheria ya uchaguzi kimemhadaa rais Kikwete na hivyo kwenda kinyume na demokrasia.


Kwa habari zaidi, soma MWANANCHI.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom