Kariakoo baba lao.
Nilikua nimeenda kununua Tende pale Msimbazi msikiti wa Idrisa kwa ajili ya iftar (kufuturisha Waislamu wenzangu nipate thawabu kwa Mola wangu. Yaani pamoja na kuwa na tabia chafu ya kutembea na wake za watu lakin najivunia kuwa Muislamu aisee. Inshallah mwaka huu nikioa nitatulia).
Sasa wakat naondoka nikapita mitaa ya katikati mule, nikaona meza moja Raba kali kinoma, zile wanaziiitaga Air Jordan, Nike, NBA snickers. Kuulizia bei zake akaanzia 20,000!
Daaah nikavikagua na kuanza kujisemea moyoni hivi si naonaga akina David Sportswear, Robyone, NjooKariakoo2020 wanauza kuanzia 65,000 mpaka 70, 0000!!!
Nikamwambia mshikaji mie nina 14,000 akanitolea nje. Nikasepa, akaniita akasema ongeza buku. Nikampa 15,000 nikabeba.
Wakuu, kumbe madukani huwa mnaibiwa. Vitu vya kijanja kwa bei za kijanja vyote vipo Kariakoo.
View attachment 1764016