Karne 21 bado ni sahihi DC & RC kuteuliwa na Rais?

Karne 21 bado ni sahihi DC & RC kuteuliwa na Rais?

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Heshima sana wanajamvi,

Tanzania ilipata uhuru wake zaidi ya miaka 60 iliyopita.Tumepitia awamu mbali mbali kuanzia awamu ya kwanza ya Mwl Nyerere hadi sasa awamu ya sita ya Mama Samia Suluhu.

Nimekuwa nikitatizwa na namna tunavyojitawala,hasa katika suala la zima la mamlaka ya uteuzi wa nafasi mbali mbali kama RC au DC.

Hizi nafasi za RC or DC zinahusika moja kwa moja na maisha ya wananchi wengi.Nimejaribu kufuatilia mamlaka ya Wakuu wa Mikoa au Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao ya kazi nikaona wamekuwa na nguvu kuliko viongozi wanaochaguliwa na wananchi kama Wabunge au Madiwani.

Wakuu wa Wilaya na Mikoa wana uwezo wa kuwaweka ndani wananchi pia ni wenyeviti wa ulinzi na usalama katika maeneo yao ya kazi.

Wakuu hawa wapo katika maeneo ya kazi kwa maana ya Wilaya na Mikoa kwa ridhaa ya Rais na si wananchi !.

Hapa ndio mgogoro unapoanza,mfano mzuri ni Mkuu wa Wilaya ya Hai kama wananchi wangekuwa na uwezo wa kumwadhibu wengefanya hivyo siku nyingi.Matokeo yake Wakubwa hawa wanajitahidi kwa kadri ya uwezo wote kimfurahisha Rais au kutenda mambo ambayo yatampendeza Rais na si wananchi.

Utaratibu huu uliopitwa na wakati unasababisha wananchi wa maeneo mbali mbali kuongozwa na viongozi ambao hawana ridhaa nao.

Leo hii wananchi wa Mkoa wa Manyara wameletewa Makongoro Nyerere kuongoza Mkoa wao pasipo kuhusika kwa namna yoyote katika uteuzi wake.Mambo ni hayo hayo katika Mikoa yote na Wilaya zote.

Naomba kuwasilisha,

Ngongo Safarini Zanzibar kwa mapumziko mafupi na kusheherekea sikukuu ya Idd.
 
Heshima sana wanajamvi,

Tanzania ilipata uhuru wake zaidi ya miaka 60 iliyopita.Tumepitia awamu mbali mbali kuanzia awamu ya kwanza ya Mwl Nyerere hadi sasa awamu ya sita ya Mama Samia Suluhu.

Nimekuwa nikitatizwa na namna tunavyojitawala,hasa katika suala la zima la mamlaka ya uteuzi wa nafasi mbali mbali kama RC au DC.

Hizi nafasi za RC or DC zinahusika moja kwa moja na maisha ya wananchi wengi.Nimejaribu kufuatilia mamlaka ya Wakuu wa Mikoa au Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao ya kazi nikaona wamekuwa na nguvu kuliko viongozi wanaochaguliwa na wananchi kama Wabunge au Madiwani.

Wakuu wa Wilaya na Mikoa wana uwezo wa kuwaweka ndani wananchi pia ni wenyeviti wa ulinzi na usalama katika maeneo yao ya kazi.

Wakuu hawa wapo katika maeneo ya kazi kwa maana ya Wilaya na Mikoa kwa ridhaa ya Rais na si wananchi !.

Hapa ndio mgogoro unapoanza,mfano mzuri ni Mkuu wa Wilaya ya Hai kama wananchi wangekuwa na uwezo wa kumwadhibu wengefanya hivyo siku nyingi.Matokeo yake Wakubwa hawa wanajitahidi kwa kadri ya uwezo wote kimfurahisha Rais au kutenda mambo ambayo yatampendeza Rais na si wananchi.

Utaratibu huu uliopitwa na wakati unasababisha wananchi wa maeneo mbali mbali kuongozwa na viongozi ambao hawana ridhaa nao.

Leo hii wananchi wa Mkoa wa Manyara wameletewa Makongoro Nyerere kuongoza Mkoa wao pasipo kuhusika kwa namna yoyote katika uteuzi wake.Mambo ni hayo hayo katika Mikoa yote na Wilaya zote.

Naomba kuwasilisha,

Ngongo Safarini Zanzibar kwa mapumziko mafupi na kusheherekea sikukuu ya Idd.
Kwa kuwa utafiti wako au ushauri,mawazo yako yameweza kuona,sii mbaya tukafahamu matamanio yako ni yapi ili mapungufu hayo,yaweze kurekebishwa,Binafsi naamini wateuliwa huwa wanatekeleza matakwa ya mamlaka ya uteuzi,ni vipi tunaweza kuboresha ili kuepukana na shida kama hizi siku zijazo.
 
Ndio maana hawataki Katiba Mpya hivyo vyeo kwa ujumla wake havina maana vya kufutwa tu, hao wote ni wafanyakazi wa CCM.

Ebu tufikiri kidogo nje ya box.Mkuu wa Wilaya ya Hai Sabaya Ole Lengai kaumiza watu wengi sana wakati akitumikia nafasi ya ukuu wa Wilaya.

Mamlaka ya uteuzi ilichukua muda mrefu sana kumwondosha katika nafasi wakati tuhuma zake zipo wazi muda mrefu sana.Ushahidi upo wazi sasa jiulize ni kwanini mamlaka hazikuchukua hatua !.Nafiki sababu kubwa ni maumivu,hasara na Mambo yote ya hovyo yakikuwa yakiwagusa wananchi moja kwa moja na si viongozi waliofanya uteuzi.
 
Heshima sana wanajamvi,

Tanzania ilipata uhuru wake zaidi ya miaka 60 iliyopita.Tumepitia awamu mbali mbali kuanzia awamu ya kwanza ya Mwl Nyerere hadi sasa awamu ya sita ya Mama Samia Suluhu.

Nimekuwa nikitatizwa na namna tunavyojitawala,hasa katika suala la zima la mamlaka ya uteuzi wa nafasi mbali mbali kama RC au DC.

Hizi nafasi za RC or DC zinahusika moja kwa moja na maisha ya wananchi wengi.Nimejaribu kufuatilia mamlaka ya Wakuu wa Mikoa au Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao ya kazi nikaona wamekuwa na nguvu kuliko viongozi wanaochaguliwa na wananchi kama Wabunge au Madiwani.

Wakuu wa Wilaya na Mikoa wana uwezo wa kuwaweka ndani wananchi pia ni wenyeviti wa ulinzi na usalama katika maeneo yao ya kazi.

Wakuu hawa wapo katika maeneo ya kazi kwa maana ya Wilaya na Mikoa kwa ridhaa ya Rais na si wananchi !.

Hapa ndio mgogoro unapoanza,mfano mzuri ni Mkuu wa Wilaya ya Hai kama wananchi wangekuwa na uwezo wa kumwadhibu wengefanya hivyo siku nyingi.Matokeo yake Wakubwa hawa wanajitahidi kwa kadri ya uwezo wote kimfurahisha Rais au kutenda mambo ambayo yatampendeza Rais na si wananchi.

Utaratibu huu uliopitwa na wakati unasababisha wananchi wa maeneo mbali mbali kuongozwa na viongozi ambao hawana ridhaa nao.

Leo hii wananchi wa Mkoa wa Manyara wameletewa Makongoro Nyerere kuongoza Mkoa wao pasipo kuhusika kwa namna yoyote katika uteuzi wake.Mambo ni hayo hayo katika Mikoa yote na Wilaya zote.

Naomba kuwasilisha,

Ngongo Safarini Zanzibar kwa mapumziko mafupi na kusheherekea sikukuu ya Idd.
Nilicho gundua toka kwako ni mawivu tu.
 
Kwa kuwa utafiti wako au ushauri,mawazo yako yameweza kuona,sii mbaya tukafahamu matamanio yako ni yapi ili mapungufu hayo,yaweze kurekebishwa,Binafsi naamini wateuliwa huwa wanatekeleza matakwa ya mamlaka ya uteuzi,ni vipi tunaweza kuboresha ili kuepukana na shida kama hizi siku zijazo.

Ahsante sana kwa angalizo lako.

Mosi ningependa wananchi wote katika katika maeneo yao wapate fursa ya kuhusika moja kwa moja au kupitia wawakilishi wao katika uteuzi wa Mkuu wa Mkoa.

Pili nafasi ya Mkuu wa Wilaya nafikiri imepitwa na wakati.Hakuna sababu za msingi nafasi hizi zitaendelea kuwepo.Kazi za Mkuu wa Wilaya zaweza kufanywa na DED,Meya au Wenyeviti wa maeneo husika.

Mwisho tukifuta nafasi za Wakuu wa Wilaya ambazo nafikiri sasa zimefika 120... taifa litaokoa mabilioni ya fedha za walipa kodi.Fikiria 3,000,000 x 100= 300,000,000 huu mshahara pekee bado magari,nyumba .....

Kwa mwezi mmoja taifa lingeweza kuokoa zaidi ya Tsh 1 billion ambazo zingeweza kuelekezwa katika maeneo mengi ya maendeleo.Chukua Wilaya moja wapo viongozi wengi kupita kazi zilizopo
1.Mkuu wa Wilaya
2.Katibu Tawala wa Wilaya
3.Meya au Mwenyeki wa Halmashauri
4.Mkurugenzi wa Mji au Jiji
5.Mbunge
Hata tukilipa kodi kiasi gani ni vigumu sana kuendelea badala yake fedha nyingi zitakwenda kulipa mishahara na marupurupu kibao Viongozi waliopungukiwa kazi badala yake majungu yatazidi kuchukua nafasi kubwa.
 
Vyeo vya kurithi kutoka kwa Wakoloni hivyo. Havijawahi kuwa na tija yoyote ile kwa Taifa, zaidi tu ya hao wateule kutafuna kodi zetu huku wakikinufaisha chama chao cha ccm ili kiendelee kuitawala nchi yetu kimabavu.

Cha kushangaza hao Wazungu wenyewe kwa sasa huwezi kuwasikia wakikumbatia aina hii ya watu! Ila sisi ndiyo tumekaza shingo, mwanzo mwisho.
 
Ebu tufikiri kidogo nje ya box.Mkuu wa Wilaya ya Hai Sabaya Ole Lengai kaumiza watu wengi sana wakati akitumikia nafasi ya ukuu wa Wilaya.

Mamlaka ya uteuzi ilichukua muda mrefu sana kumwondosha katika nafasi wakati tuhuma zake zipo wazi muda mrefu sana.Ushahidi upo wazi sasa jiulize ni kwanini mamlaka hazikuchukua hatua !.Nafiki sababu kubwa ni maumivu,hasara na Mambo yote ya hovyo yakikuwa yakiwagusa wananchi moja kwa moja na si viongozi waliofanya uteuzi.
Ni kweli mkuu, viongozi hawa wanaoteuliwa na Rais wanatuumiza sana wananchi wanaotuongoza. Lakini kwa Katiba iliyopo hata hao tuliowachagua (wabunge na madiwani) tuna namna au uwezo wowote wa kuwawajibisha pale wanapokuwa hawafanyi kile tulichowatuma? Jibu ni HAPANA, hatuna uwezo wala namna ya kuwafanya chochote, sasa hapa ndio maana kila siku tunalia tupate katiba mpya. Tusichoke kudai, tuendelee mpaka kieleweke tupate Katiba mpya itayotupa uwezo wa kuwawajibisha na hata kuwatoa madarakani wakizingua.
 
Ni kweli mkuu, viongozi hawa wanaoteuliwa na Rais wanatuumiza sana wananchi wanaotuongoza. Lakini kwa Katiba iliyopo hata hao tuliowachagua (wabunge na madiwani) tuna namna au uwezo wowote wa kuwawajibisha pale wanapokuwa hawafanyi kile tulichowatuma? Jibu ni HAPANA, hatuna uwezo wala namna ya kuwafanya chochote, sasa hapa ndio maana kila siku tunalia tupate katiba mpya. Tusichoke kudai, tuendelee mpaka kieleweke tupate Katiba mpya itayotupa uwezo wa kuwawajibisha na hata kuwatoa madarakani wakizingua.

Katiba mpya ni muhimu sana wakati huu kuliko kipindi chochote.
 
Kwa nyakati hizi hatuwahitaji kabisa. Ras na Das wanatosha kulink tawala za mikoa na serikali kuu.
 
Sio sahihi ila ndio hivyo jamii kubwa wanashangali watu kupewa "ulaji" na yupi mtu poa na asiye poa!
 
Kile kiti sijui huwa kina nini! Wimbo ni huo huo toka enzi za Nyerere!
Kikwete:Rais ana madaraka makubwa Tanzania alisikika kwenye mazishi ya Magufuli.

Cha ajabu uwa wanaongea wakiwa nje ya office
 
Ahsante sana kwa angalizo lako.

Mosi ningependa wananchi wote katika katika maeneo yao wapate fursa ya kuhusika moja kwa moja au kupitia wawakilishi wao katika uteuzi wa Mkuu wa Mkoa.

Pili nafasi ya Mkuu wa Wilaya nafikiri imepitwa na wakati.Hakuna sababu za msingi nafasi hizi zitaendelea kuwepo.Kazi za Mkuu wa Wilaya zaweza kufanywa na DED,Meya au Wenyeviti wa maeneo husika.

Mwisho tukifuta nafasi za Wakuu wa Wilaya ambazo nafikiri sasa zimefika 120... taifa litaokoa mabilioni ya fedha za walipa kodi.Fikiria 3,000,000 x 100= 300,000,000 huu mshahara pekee bado magari,nyumba .....

Kwa mwezi mmoja taifa lingeweza kuokoa zaidi ya Tsh 1 billion ambazo zingeweza kuelekezwa katika maeneo mengi ya maendeleo.Chukua Wilaya moja wapo viongozi wengi kupita kazi zilizopo
1.Mkuu wa Wilaya
2.Katibu Tawala wa Wilaya
3.Meya au Mwenyeki wa Halmashauri
4.Mkurugenzi wa Mji au Jiji
5.Mbunge
Hata tukilipa kodi kiasi gani ni vigumu sana kuendelea badala yake fedha nyingi zitakwenda kulipa mishahara na marupurupu kibao Viongozi waliopungukiwa kazi badala yake majungu yatazidi kuchukua nafasi kubwa.
Sasa hapa,suluhu ni katiba pendekezwa ya jaji warioba.
 
Mimi linalonisononesha kuliko yote ni ile nguvu waliyo nayo hawa wahuni (wakuu) wa mikoa na wilaya kiasi kwamba wanathubutu kuwaweka ndani wabunge (wawakilishi) waliochaguliwa na wananchi wa eneo husika.

Katika karne hii? Hapana, hiki ni kiwango cha upumbavu, ushenzi na uzandiki usiostahimilika katika karne hii! Maskini Tanzania, unaweza kudhani bado tuko katika ile karne ya mawe! Hakika CCM imeiharibu sana hii nchi.
 
Back
Top Bottom