Karne 21 bado ni sahihi DC & RC kuteuliwa na Rais?

Karne 21 bado ni sahihi DC & RC kuteuliwa na Rais?

Kile kiti sijui huwa kina nini! Wimbo ni huo huo toka enzi za Nyerere!
Jk aliuanzisha mchakato wa katiba mpya,ila shida naona ilikuwa ni wazalendo maslahi ndio waliouteka mchakato ule na kuuchelewesha

Hadi muda wake haukutosha kuukamilisha,na mtazamo wangu ni kuwa wenye maslahi yao walihakikisha aliyefuata ni mtu siyetayari kuuendeleza mchakato ile malengo yao yatimie,japo hali haikuwa kama matarajio yao.
 
Kwa mamlaka aliyopewa Rais kwa mujibu wa katika hakuna tatizo...
 
Heshima sana wanajamvi,

Tanzania ilipata uhuru wake zaidi ya miaka 60 iliyopita.Tumepitia awamu mbali mbali kuanzia awamu ya kwanza ya Mwl Nyerere hadi sasa awamu ya sita ya Mama Samia Suluhu.

Nimekuwa nikitatizwa na namna tunavyojitawala,hasa katika suala la zima la mamlaka ya uteuzi wa nafasi mbali mbali kama RC au DC.

Hizi nafasi za RC or DC zinahusika moja kwa moja na maisha ya wananchi wengi.Nimejaribu kufuatilia mamlaka ya Wakuu wa Mikoa au Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao ya kazi nikaona wamekuwa na nguvu kuliko viongozi wanaochaguliwa na wananchi kama Wabunge au Madiwani.

Wakuu wa Wilaya na Mikoa wana uwezo wa kuwaweka ndani wananchi pia ni wenyeviti wa ulinzi na usalama katika maeneo yao ya kazi.

Wakuu hawa wapo katika maeneo ya kazi kwa maana ya Wilaya na Mikoa kwa ridhaa ya Rais na si wananchi !.

Hapa ndio mgogoro unapoanza,mfano mzuri ni Mkuu wa Wilaya ya Hai kama wananchi wangekuwa na uwezo wa kumwadhibu wengefanya hivyo siku nyingi.Matokeo yake Wakubwa hawa wanajitahidi kwa kadri ya uwezo wote kimfurahisha Rais au kutenda mambo ambayo yatampendeza Rais na si wananchi.

Utaratibu huu uliopitwa na wakati unasababisha wananchi wa maeneo mbali mbali kuongozwa na viongozi ambao hawana ridhaa nao.

Leo hii wananchi wa Mkoa wa Manyara wameletewa Makongoro Nyerere kuongoza Mkoa wao pasipo kuhusika kwa namna yoyote katika uteuzi wake.Mambo ni hayo hayo katika Mikoa yote na Wilaya zote.

Naomba kuwasilisha,

Ngongo Safarini Zanzibar kwa mapumziko mafupi na kusheherekea sikukuu ya Idd.
Pengine swali lingekuwa...upo umuhimu was kuwa na maRC na maDC??
 
Kama bado wakuu wa wilaya na mikoa hawawajibiki kwa wapiga kura, tuna kazi ngumu ya kupata maendeleo!!

Kama tunavowashutumu wabunge kwa kutoleta maendeleo, wakuu wa mikoa wawe na wajibu pia. Kama vipi watoke tu. Maendeleo hayajawahi kuwa jambo la level ya mkoa. Ni jimbo!!!
 
Pengine swali lingekuwa...upo umuhimu was kuwa na maRC na maDC??
Heshima sana wanajamvi,

Tanzania ilipata uhuru wake zaidi ya miaka 60 iliyopita.Tumepitia awamu mbali mbali kuanzia awamu ya kwanza ya Mwl Nyerere hadi sasa awamu ya sita ya Mama Samia Suluhu.

Nimekuwa nikitatizwa na namna tunavyojitawala,hasa katika suala la zima la mamlaka ya uteuzi wa nafasi mbali mbali kama RC au DC.

Hizi nafasi za RC or DC zinahusika moja kwa moja na maisha ya wananchi wengi.Nimejaribu kufuatilia mamlaka ya Wakuu wa Mikoa au Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao ya kazi nikaona wamekuwa na nguvu kuliko viongozi wanaochaguliwa na wananchi kama Wabunge au Madiwani.

Wakuu wa Wilaya na Mikoa wana uwezo wa kuwaweka ndani wananchi pia ni wenyeviti wa ulinzi na usalama katika maeneo yao ya kazi.

Wakuu hawa wapo katika maeneo ya kazi kwa maana ya Wilaya na Mikoa kwa ridhaa ya Rais na si wananchi !.

Hapa ndio mgogoro unapoanza,mfano mzuri ni Mkuu wa Wilaya ya Hai kama wananchi wangekuwa na uwezo wa kumwadhibu wengefanya hivyo siku nyingi.Matokeo yake Wakubwa hawa wanajitahidi kwa kadri ya uwezo wote kimfurahisha Rais au kutenda mambo ambayo yatampendeza Rais na si wananchi.

Utaratibu huu uliopitwa na wakati unasababisha wananchi wa maeneo mbali mbali kuongozwa na viongozi ambao hawana ridhaa nao.

Leo hii wananchi wa Mkoa wa Manyara wameletewa Makongoro Nyerere kuongoza Mkoa wao pasipo kuhusika kwa namna yoyote katika uteuzi wake.Mambo ni hayo hayo katika Mikoa yote na Wilaya zote.

Naomba kuwasilisha,

Ngongo Safarini Zanzibar kwa mapumziko mafupi na kusheherekea sikukuu ya Idd.
Kamanda: mbona mambo unaishia nusunusu? Askofu wako anateuliwa Roma, Headmaster anateuliwa na Ndalichako Dodoma, na Mkurugenzi wa Fedha anatokea NBAA Dar es Salaam? Kweli bwana, sasa tumesoma vya kutosha kila Kijiji tuwe na Mganga wetu, Mufti wetu, RPC (sorry, VPC) wetu, Askofu wetu, TAKUKURU wetu, Supika wetu. Vipi, mpe tundulissu aongeze kwenye Ilani yake, last time aliishia majimboni sasa twende vijijini kabisa, eh?
 
Back
Top Bottom