nzagambadume
JF-Expert Member
- Apr 9, 2018
- 2,430
- 5,779
- Thread starter
-
- #41
Upuuzi wa mtoa mada. .. Unaonyesha ujinga wake.
Kama unakumbuka wiki iliyopita, tuliishia
pale ambapo mtu mmoja raia wa Misri,
anayedaiwa kuwa na ukaribu na Kocha
Amunike alifika katika kambi ya Stars katika
eneo la New Cairo katika Hoteli ya
LandaMark Helnan na kutamka mambo
yaliyoonyesha kutaka upangaji wa matokeo.
Raia huyo wa Misri amewahi kufika kambini
hapo kumjulia hali Kocha Amunike na
inaelezwa ni wakala wake. Alikuwa akijua
kama inawezekana Stars kufungwa mabao
mengi zaidi.
“Alisema kwamba dhidi ya Algeria, Stars
itafungwa lakini angetamani kuona mabao
mengi. Hivyo alikuwa akiuliza ili iwe hivyo
yeye afanye nini,
” kinaeleza chanzo.
Mmoja wa madereva waliokuwa
wanawaendesha viongozi wa TFF ndiye
aliyeanza kunitonya kuhusiana na hilo,
akisisitiza niwaeleze viongozi kwamba yule
si mtu mzuri kwa kuwa amemsikia
akizungumza maneno hayo Kiarabu.
Mimi niliwafikia baadhi ya viongozi wa TFF
na kuewaeleza hali hiyo, tayari walikuwa
wametangulia mbele yangu baada ya
kunieleza walikuwa wamemrekodi.
Walikiri kweli alifika na kuuliza hivyo,
akitaka msaada wa kuona Stars inafungwa
mabao mengi, nao wakamuwekea mtego na
kumrekodi. Juhudi zangu za kupata sauti
hiyo zilifeli baada ya wao kugoma kunipa.
Hata hivyo, walionyesha kuwa kwenye
taharuki kama mtu huyo alishirikiana na
Amunike au alikuwa na nia yake tofauti
wakidhani, huenda alitaka, kufanya hivyo
kwa mambo mawili.
Kwanza huenda ni mcheza kamari na
anashirikiana na kocha, lakini wakataka
kujiridhisha. Au pili, ni mhuni tu ambaye
alitaka Stars ifungwe mabao mengi zaidi,
TFF wachukizwe na hiyo hali na baada ya
hapo wamtimue Amunike ili alipwe rundo la
fedha ili naye afaidike.
Wakati naanza kuandika makala haya
nilielezea kuhusiana na Watanzania
tunavyoamini siri, tunaona kutosema
mambo yanayotukera ndiyo uungwana.