Kashfa: VETA yadaiwa kudorora kwa kiwango cha kutisha

Kashfa: VETA yadaiwa kudorora kwa kiwango cha kutisha

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Taarifa zetu za Uchunguzi zinaonyesha kwamba Chuo cha Ufundi cha Taifa (VETA), kwa sasa ndio Taasisi duni kabisa miongoni mwa Taasisi kongwe za serikali ya Tanzania, zipo habari kwamba kwa sasa VETA inaweza kuahirisha mitihani kutokana na kukatika kwa umeme tu, hii ni kwa sababu hawana jenereta au hawana hela ya kununua mafuta kwa ajili ya jenereta lao la kizamani walilonalo.

Kwa mfano, VETA CHANG'OMBE wanaongoza kwa matatizo , ambapo mtoa Taarifa wetu amedokeza kwamba ukiachilia mbali UKATA wa kushindwa kununua mafuta kwa ajili ya Generetor lao la kizamani lililopitwa na wakati, HATA WAFANYAKAZI WAO WANAWEZA KUTOKULIPWA MSHAHARA MPAKA UREFU WA MIEZI 6, ikumbukwe kwamba hii ndio taasisi inayofundisha hata wale malundo ya wanafunzi wanaodaiwa kulipiwa na ofisi ya Waziri Mkuu, Sasa kwanini wafanyakazi wao hawalipwi mshahara, ni nani anakula hela hizo, ni Mkuu wa Chuo au ni vigogo wa Wizara?

Taarifa mpya kutoka VETA CHANG'OMBE inadokeza kwamba kitengo cha wakufunzi wa shule ya Madereva , shule ya madereva iliyoheshimika Duniani kinazidi kupukutika baada ya Zaidi ya wakufunzi 6 kuondoka kwa mkupuo kutokana na kudhulumiwa hela zao za mshahara kwa miezi mingi.

Tatizo la Chuo cha VETA linatokana na Mkuu wa Chuo cha Chang'ombe au linatokana na Wizara?

Timu yetu ya Uchunguzi yenye watu zaidi ya 10 imeingia rasmi ndani ya Veta na itahakikisha kila uchafu unafukuliwa na kuanikwa hadharani, kama chanzo ni chuo chenyewe au kama chanzo ni serikali, basi kila kitu kitaaanikwa bila huruma.

ITAENDELEA...
 
Sasa vyuo hivi ndiyo kwa ajili ya wananchi wanyonge wenye vijana wao waliokuwa wanaota baada ya kuhitimu ufundi stadi wajiajiri au vyeti vyao vipendelewe na serikali kwa kuwapa hati za kusafiri waende nje kutafuta maisha kupitia ujuzi wao .

TOKA MAKTABA :

Mimi nashauri vijana wote waliomaliza vyuo vya elimu juu, ufundi stadi, VETA wapewe pasipoti kubwa ya kusafiri nje bila masharti yoyote, wazewe kwenda ughaibuni.

Every United States citizen is entitled to a U.S. passport provided that they, or an adult acting on a child’s behalf, comply with all applicable requirements, and that there is no statutory or regulatory reason to deny the passport .. more : source : Fact Sheet on Passports for Judges and Lawyers

More links :
https://www.tcu.go.tz/?q=content/higher-education-statistics,


 
Sasa vyuo hivi ndiyo kwa ajili ya wananchi wanyonge wenye vijana wao waliokuwa wanaota baada ya kuhitimu ufundi stadi wajiajiri au vyeti vyao vipendelewe na serikali kwa kuwapa hati za kusafiri waende nje kutafuta maisha kupitia ujuzi wao .


TOKA MAKTABA :
Itafahamika tu
 
Mambo mengine yanasikitisha sana. Halafu tunanunua ndege kesh kwa matrilion. Sijui ngozi nyeusi tumeumbwaje utadhani bongo zetu zimesheheni Mavi.

So Sad!
Waziri Mkuu anahamisha Wamasai kwa ufanisi mkubwa sana , lakini kule anakopeleka wanafunzi wa Ofisi yake amekupuuza !
 
Back
Top Bottom