Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,176
Lowasa hawezi kukwepa kashifa hii hata akiogamaji ya baarini.
Mlitaka aseme alihusika ili akatwe tena? kashfa aliyotuhumiwa sio ya siasa ya chama bali ni maslahi ya umma na alipaswa kuulizwa na mamlaka ya serikali(mahakama) ikizingatiwa kuwa wanaomuuliza ndio waliomtuhumu kuhusika! au chadema wamekuwa mahakama?
NILIWAITA MAKATIBU WAKUU kutaka kuvunja mkataba wa Richmond lakini Mwanasheria Mkuu Ndugu Mwanyika aliporudi kutoka nje alisema kuwa nimepokea simu kutoka mamlaka ya juu kuwa mkataba usainiwe. Mwisho wa kunukuu. Sisi kama waumini wa CCM tumefadhaishwa na maneno haya na hivyo tunaomba maneno haya yakanushwe katika vyombo vya habari, magazeti na hata kwenye redio vinginevyo huku mitaani hakukaliki.
Good question.
Angeteuliwa kuwa mgombea wa CCM angetoka na kusifia kila kitu.
Sijui humu ndani kuna mataahira wangapi., lakini siwezi kuwa mmoja wa machizi wanaoweza kuamini dhamira ya Lowassa ni njema, baada ya kukaa kimya kwa miaka 8 kuhusu kitu alichojua ni kosa,au kuhusu ushiriki wake.
lakin kwa kuwa shake before use wako wengi,kuna watu watakunywa hii kool aid bila hata ku-shake well before drinking.
Mzee Ngoyai kawaambia kwamba yeye ni Mkristo, na Neno la Mungu linanena waziwazi kuhusu kutii mamlaka iliyojuu:
Warumi 13: 13
Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu.
mngekalia kumpigia debe mgombea wenu mngemsaidia sana,kwani ana wakati mgumu sana kupambana na tingatinga
Mlitaka aseme alihusika ili akatwe tena? kashfa aliyotuhumiwa sio ya siasa ya chama bali ni maslahi ya umma na alipaswa kuulizwa na mamlaka ya serikali(mahakama) ikizingatiwa kuwa wanaomuuliza ndio waliomtuhumu kuhusika! au chadema wamekuwa mahakama?
Kwenye siasa watu hawazungumzizungumzi tu. Kila kauli ina sababu na maana kubwa.
Ukiangalia jitihada za Lowassa kutaka kuzungumzia sakata la Richmond kupitia TBC lilivyozuiwa kabla, yaliyomkuta Tido Mhando, ukifautilia kauli na mashaka ya viongozi wengi wa CCM dhidi ya mwanachama 'mwenzao' wa zamani Lowassa na hali ya hofu ya watu kusema atalipiza kisasi, mtu mwenye akili ata-conclude kuwa kuna kitu chini ya kapeti hatukijui kuhusiana na ufisadi au usafi wa Lowassa.
Hivi mamlaka ya juu iko karibu na waziri mkuu au au na mwanasheria wa serikali.? Inauhakika gani kama mwanasheria hakupiga simu kwa mamlaka ya juu kisha kumuongopea.au kushauriwa vibaya na mwanasheria.ili hali yeye lowasa alikuwa karibu sana na mamlaka za juu za maamuzi kwa nini hakuongea yeye na mamlaka ya juu
Hivi dereva wa hilo tinga tinga ni nani?
Save that bullcrap to some CDM kid not me please.
Yani unataka mtu aliyeficha uovu wa CCM kwa miaka 8 baada ya kufahamu,if that was the case anyways,ndio apewe nchi?do u even listen to yourself?
Wakati slaa anamwita Lowassa Fisadi hakujua haya unayobwabwaja hapa?wakati viongozi wenu wakuu wooote walipotumia kodi zetu kuzubguka jukwaa baada ya jukwaa kumuambia Lowassa na marafiki zake hamkuyajua hayo?what changed?
Msifanye watu hatunazo.
Huyo Ng'wamalalala ni kada wa CCM kindakindaki, humuwezi mkuu!
Kuna watu katika serikali ya JK walishasema kufanya kazi na huyo jamaa inahitaji moyo.
Na hata Pinda Mizengo hapo alipo anatamani ikiwezekana uchaguzi ufanyike hata kesho tu ili mzee wa watu ajipatie mafao yake akapumzike hukooo kijijini kwake ili aendelee na ufugaji wa nyuki wake kwa sbb kufanya kazi na Mkwere yahitaji moyo.
Unakumbuka sakata la Jairo Pinda alivyopata taabu bungeni wakati jamaa (JK) yuko ughaibuni anakula good time tu na kuagiza kwa simu tu kwamba baadhi ya maafisa wa wizara ya nishati na madini wasimamishwe, isipokuwaJairo asubiriwe yeye hadi atakaporudi?
Mtu mwadilifu siku zote husimama katika ukweli na haki.Kama aliona mkataba wa Richmond una matatizo kwa nini hakugoma kusaini? Na hata kujiuzulu kama aliona watu wanataka asaini ili kulinda hadhi yake ya uadilifu na kulinda mali za umma?
Kusema alishinikizwa kusaini alishinikizwaje? Alishikiwa bastola au? Madhara ya kusaini kisheria si anayajua? Aliyesaini ndiye mhusika mwenyewe au hilo halijui.Kwa taratibu za kikazi hakuna kitu kinachoitwa kushinikizwa kusaini.Mtu anayesaini ana uhuru wa kukubali kusaini au kukataa na hata kujiuzulu akiona kutia sahihi huko kutampa matatizo huyo aliyesaini.
Kama aliidhinisha RICHMOND kusikizia kuwa alipata shinikizo toka juu ni uongo na utapeli mkubwa angegoma kusaini na angejiuzulu na akaeleza sababu za kugoma kusaini na kujiuzulu kuwa ni kwa sababu hataki Richmond leo hii angekuwa shujaa wa kimaadili.Kusaini kunaonyesha mzee mzima alikula pesa aache uongo.Zigo la Richmond analo.