Kashfa ya Richmond: Lowassa, Karamagi na Dkt. Msabaha Wajiuzulu

Kashfa ya Richmond: Lowassa, Karamagi na Dkt. Msabaha Wajiuzulu

Jamani wacheni maneno ya kitoto msiwafanaye Watanzania kuwa ni taahira. Kama Lowassa - Mzee wa maamuzi magumu - angeona kuwa huu mkataba ni mbovu, angeuvunja. Alipokataliwa na "Mamlaka ya Juu" - kama kweli alikataliwa - basi angejiuzulu hapo hapo. Mbona ni juzi tu "Mamlaka ya Juu" imemuengua Lowassa kwenye kinyanganyiro cha Urais: kama kweli anatii Mamlaka ya Juu au analazimishwa nayo, mbona amejiuzulu na kwenda CHADEMA? Kwa nini hakuenda CHADEMA wakati huo huo wanamwita fisadi?

Sitegemei kama Kikwete kama mtu binafsi angeweza kuamuru Mkataba ufanyike, alisema "alishauriwa na Makatibu wakuu" kuwa uendelee. Lowassa anaposema Mamlaka ya Juu ilisema "mkataba uendelee" hatuambii kila kitu. What were the exact words and what was the context? Je, Mamlaka labda ilisema "kama ni shida ya kampuni kutoonekana, watafuteni zaidi" (maana Mwakyembe alisema walienda Texas wakakosa ofisi yao); au kama ni shida ya gharama basi "tafuteni uwezekano wa kupunguza". Au kitu kama hicho.

Rais ni mtu mmoja hawezi kusema "mkataba uendelee' hivi hivi. Au labda Lowassa anasema kuwa Rais "alijua kuwa najua kuwa anajua"? Yaani ulikuwa na "mradi" wao wote wawili? In that case wote ni majambazi, washitakiwe; haimaanishi kuwa kama Rai anajua kwa hiyo Lowassa ndiyo awe msafi.

Kumhusisha Rais na ufisadi wake haiamaanishi yeye ni msafi. Kumbuka kuwa Lowassa ana tabia ya kujificha mgongoni mwa watu wengine. Nani asiyejua kuwa ni majuzi tu alimhusisha Makamu wa Rais na ufisadi wake. Alienda Arusha kuhonga Msikitini akidai "amesaidiwa na marafiki zake". Marafiki hawo hajawataja hata siku moja, lakini siku hiyo haraka haraka akasema "marafiki wangu kama Makamu wa Rais" kwa vile alimtuma akamuwakilishe.

Hapo si anatumia vibaya jina la Dr Bilal ambaye hata siku moja hajafuatana na Lowassa kwenda kwenye hizi hongahonga zake Makanisani na kwenye kwaya na Misikitini?

Simtetei Rais lakini naona wazi kuwa Lowassa anatafuta pa kujificha - sasa anataka kuhusisha na Rais kwa jambo ambalo hatuambii ukweli wote. Hii huitwa MONEY LAUNDERING, yaani anamtumia Makamu wa Rais kufua nguzo zake chafu. Unaweza ukaenda mahakama yoyote utaambiwa kuwa "ushahidi" wa fisadi dhidi ya mafisadi wenziye huwa haupewi uzito wowote.

Lowassa hawezi kujitoa kwenye ufisadi hata iweje. Hata hii Richmond si ufisadi pekee anaohusishwa nao, wala si ufisadi mkubwa zaidi, ZIPO FISADI NYINGI. Wananchi wanamjua vizuri na watamjua zaidi; watamtosa asiweze kurudi tena. RM
 
Mnahangaika na ushahidi wa EL kuhusika na Richmond ambao miaka zaidi ya 7 sasa haujapatikana. Lakini mnakwepa ushahidi wa wazi unaomhusu aliyekuwa "Waziri wa ujenzi" ambao uko wazi kabisa: Kuuza nyumba za umma kwa bei poa na kuisababishia nchi hasara ya mabilioni. Ni nani anapaswa kuhukumiwa kwanza hapa?
 
Hata escrow kikwete ndie muhusika mkuu, epa pia yumo, watu wanaogopoa kusema ukweli watakosa ulaji.
Na haya ndo yanawafanya wanang'ang'anie madaraka na si kuipenda Tanzania.shame on them
 
Mnahangaika na ushahidi wa EL kuhusika na Richmond ambao miaka zaidi ya 7 sasa haujapatikana. Lakini mnakwepa ushahidi wa wazi unaomhusu aliyekuwa "Waziri wa ujenzi" ambao uko wazi kabisa: Kuuza nyumba za umma kwa bei poa na kuisababishia nchi hasara ya mabilioni. Ni nani anapaswa kuhukumiwa kwanza hapa?
Mkuu magufuli bado amejificha kichakani(ccm) hatumuoni ndo maana hatuhangaiki nae.Lowasa yupo nchi ya kichaka tunamuona na lazima tumthibiti ili asichome kichaka chetu
 
Perfect, ndio maana viongozi wa dini huwa sina imani nao, wanashindwa kukemea pale ukweli ulipo wazi. Wanaogopa kutaja bila kificho kuwa JK naye aulizwe, maana maamuzi makubwa kama hayo hayawezi kupita bila yeye kuwa nataarifa.
siku watanzania wakiamua kuacha unafiki nchi yetu itakuwa imepona.viongozi wetu wa dini chief wangu most of them nao ni wanafiki tu
 
EL ni fisadi sio tu kwenye Richmond mnayohangaika nayo kumsafisha. leo anadanganya watu eti hela ni za rafiki zangu, kuna rafiki gani anakupa hela bila wewe kumsaidia chochote?

Mwambie Kikwete akatae au ampeleke Lowasa mahakamani.

Sema nani mhusika was Escrow, EPs meremeta...etc

Taja kashfa nyingine ya Lowasa.

Ferry ya Dar - Bagamoyo, uuzaji was nyumba za serikali,..... Nani kahusika?
 
JK atoke mbele kujisafisha.
Nyumba inamuangukia rasmi.
 
Na hao marsfiki zake wanataraji nini kutoka kwake? Hapa Lowasa ni fisadi na anasaidiwa na marsfiki zake ambao ni mafisadi
ashamtaja sasa povu jingi la nini, mamlka ya juu ni Rais baada ya waziri mkuu au usikiii umeweka pamba???????/
 
EL ni fisadi sio tu kwenye Richmond mnayohangaika nayo kumsafisha. leo anadanganya watu eti hela ni za rafiki zangu, kuna rafiki gani anakupa hela bila wewe kumsaidia chochote?

Taja ufisadi mwingine unaoujua kutoka kwa EL.
 
Lowasa amehusika wanaokataa waangalie Barua ya Lowa akiagiza mkataba usainie aache ubabaishaji,ata aibika mwaka huu.
 
Lowasa amehusika wanaokataa waangalie Barua ya Lowa akiagiza mkataba usainie aache ubabaishaji,ata aibika mwaka huu.

Barua haina tarehe signature ni barua bubu mbona hiyo nyingine inavyo, akili ya kuambiwa changanya na zako ukiona haina hata muhuri ujue alikataa mpango huo.Ndo mana iko hivyo
 
Napata shida kuelewa kwa kweli why EL alijiuzulu UPM kwa kutuhumiwa tuu.In other words todate he has not been proven guilt but why did he resign.
Nadhani kuna kitu nyuma ya pazia maana kunakauli pia aliwai sema EL kama tatizo ni uwaziri mkuu.....
 
Pamoja na Kuchanganya English yako mbovu na Kiswahili Kama Muhaya, Nitakusaidia Kama Ifuatavyo; Kujiuzulu yeye Alifanya Hivyo Ili

Kuiokoa serikali Isidondoke. Alisema Juzi Ofisi Kuu Ilitoa Order Wakati Yeye Alishasema Mkataba Uvunjwe.Pia Kasema Kama Una Ushahidi

Peleka Mahakamani.
 
Ministerial Responciblity this means that if waste, corruption, or any other misbehaviour is found to have occurred within a ministry, the minister is responsible even if the minister had no knowledge of the actions. A minister is ultimately responsible for all actions by a ministry because, even without knowledge of an infraction by subordinates, the minister approved the hiring and continued employment of those civil servants. If misdeeds are found to have occurred in a ministry, the minister is expected to resign. It is also possible for a minister to face criminal charges for malfeasance under their watch.
Lakini why aseme tatizo ni uwaziri mku u wkati point ya ministerial responciblity iko wazi ndg Lincoln
 
Ministerial Responciblity this means that if waste, corruption, or any other misbehaviour is found to have occurred within a ministry, the minister is responsible even if the minister had no knowledge of the actions. A minister is ultimately responsible for all actions by a ministry because, even without knowledge of an infraction by subordinates, the minister approved the hiring and continued employment of those civil servants. If misdeeds are found to have occurred in a ministry, the minister is expected to resign. It is also possible for a minister to face criminal charges for malfeasance under their watch.
Lakini why aseme tatizo ni uwaziri mku u wkati point ya ministerial responciblity iko wazi ndg Lincoln

Wewe umejiandaa kubisha.
 
Back
Top Bottom