Kashfa ya Richmond: Lowassa, Karamagi na Dkt. Msabaha Wajiuzulu

Kashfa ya Richmond: Lowassa, Karamagi na Dkt. Msabaha Wajiuzulu

Hivyo kwa maoni yangu tunachotaka kuona wana JF na watz wenye mapenzi mema, ni kwamba mapendekezo yote kwenye repoti ya Mwakyembe yamefanyiwa kazi!! HAPO NDIPO TUTAHEMA KWA FURAHA KIDOGO

Mambo taratibu mzee, hujui hayo unayosema yatawagusa wangapi, one thing at a time. Ya kwanza ilikuwa ni kukata njia zinazotumiwa kutuibia, halafu tukiwa na ukakika wa hilo the next step will follow.

Si unajua tena yaliyosemwa na tume ya Mwakyembe ni mapendekezo, sio sheria kuwa ni lazima yatekelezwe, na bunge halina uwezo wa kutekeleza yote, kwanza inategemea kupenda kwa Sitta, Kikwete na wengine.

Kwa maoni yangu Lowassa anatakiwa kufikishwa mahakamani, lakini i do not see that coming, sioni mahaka yenye jeuri hiyo! mambo taratibu!
 

Yes...Baraza linavunjika Automatically kwa mujibu wa Ibara ya 57 (2)(e)

Nanukuu...



Well done Yebo2,
Hivyo automatically Rais akikubaliana na Barua ya EL basi baraza limevunjika, na ndipo kitakuja kimbembe cha nani awe nani tena!!

Any where tuzidi kumwomba Mungu maana anaweza akachaguliwa mwingine fisadi kuliko wote!!!
 
Sishangai kwa nini PM kajiuzulu kwa sababu kwa kila aliye na akili timamu alitegemea! mimi nafurahi tu!
Lakini nina wasiwasi kujiuzulu kwake kusije kukawa ni changa la macho kwa wa tz, tukasikie eti rais amekataa au hajajibu barua hiyo na kumlazimu huyu bwana kutengua uamuzi wake huku anajua ilikuwa geresha tu!!

Pili, sijui kama tunatakiwa kufurahi tu kwa kuambia PM kajiuzulu au baada ya kusikia kachukuliwa hatua zipi za kinidhamu na kisheria kwa kusaidia kuliingiza taifa kwenye matatizo makubwa, sijui sheria lakini naona kama hili linafanana sana na kosa la jinai!! Wenzetu kule ASIA kama China na Japan tumesikia tu mtu hasa viongozi akidhibitishwa kuhusika na rushwa ni kunyogwa!!

Naomba wa tz tusichekelee hatua hii pekee, bali tuangalia huyu bwana atachukuliwa hatua zipi ili liwe fundisho na kwa yeyote atakaye fuata hapo na viongozi wote kwa ujumla! Pia ripoti ya Mwakyembe imetoa mapendekezo ya kufanya mabadiliko kwenye taasisi kama TAKUKURU, Wizara ya Nishati, wizara ya fedha na kuwachukulia hatua kali za kinidhamu na kisheria wote walio husika kwa namna moja au nyingine kwenye mchakato wa kuipata RICHMONDULI!! Watu kama akina Arthur Mwakapugi, D.Yona, Karamagi na Msabaha na wote walio toa ushahidi wa wongo kwa kamati teule wachukile hatua kali kwa kukosa maadlili na uzalendo!!

Hivyo kwa maoni yangu tunacho taka kuona wana JF na watz wenye mapenzi mema, ni kwamba mapendekezo yote kwenye repoti ya Mwakyembe yamefanyiwa kazi!! HAPO NDIPO TUTAHEMA KWA FURAHA KIDOGO

festog
 
Tanzania PM tenders resignation

Dar es Salaam, Tanzania 07 February 2008 01:19

Tanzania Prime Minister Edward Lowassa told Parliament Thursday he had tendered his resignation to the president after being implicated in a corruption scandal over an energy deal.

"Because I have been linked to this scandal, I have decided to write to the president asking to be relieved of my duties," the premier told lawmakers during a session of the Dodoma-based Parliament broadcast live on television.

The speaker adjourned the session and explained he was awaiting a decision by President Jakaya Kikwete on Lowassa's resignation letter.

The premier's decision came after a report was submitted to Parliament over a deal signed between the government and Texas-based firm Richmond for emergency power supply.

According to a probe into the contract, the prime minister, as well as two other government ministers and several other officials, allegedly meddled in the tender to favour the United States company.

The emergency power-supply deal aims at providing electricity to the East African nation in case of drought.

According to the report, the deal contravened laws and rules on procurement and costs the country $140 000 a day
. --

AFP
 
Wakuu, kwa mujibu wa taarifa za moto moto,

Karamagi na Msabaha tayari wamejiuzulu..wameandika barua kuomba kujiuzulu!

KARAMAGI NAYE AOMBA KUACHIA NGAZI.

MH. NAZIR KARAMAGI AMEMALIZA KUJIELEZA NA AMELIAMBIA BUNGE KWAMBA NA YEYE LEO ASUBUHI AMEPELEKA BARUA KWA JK KUOMBA KUJIUZURU WADHIFA WAKE WA UWAZIRI WA NISHATI NA MADINI. YEYE PIA AMEJITETEA KWAMBA HANA HATIA KATIKA SAKATA HILI.
 
Lakini JK itabidi vilevile awachukulie hatua za kisheria, especially kwa wale ambao wako directly involved kulitia taifa hasara. Kujiuzulu pekee hakutasaidia, wawe prosecuted!!!!
 
Tunasubiri wengine ambao bado wamekaa kimya; au wanasubiri JK awafukuze mwenyewe?
 
Steve,
Kama alivyosema EL mwenyewe, naungana naye kuwa hajatendewa haki na Kamati ya Mwakyembe maana hawakumuhoji (naamini asingewakwepa kama Mshirika wake wa Kibiashara- Rostam Azizi) maana Msabaha na wengineo walimtaja Waziri Mkuu kama ndiye Mshinikizaji; kwa nini hawakumhoji? LAbda naye angewataja wengine naamini kabisa kuwa angemtaja bosi wake maana vyanzo vyangu vinadai kuwa Richmonduli ulikuwa Mradi wa EL na Bosi wake! HAKI HAIJATENDEKA

Hakuna cha kutotendeka haki wala nini.Mie nafikiri alionyesha dharau kwa hii kamati, kama wahusika wenzake. Kamati kwa ustaarabu nadhani walimwita kistaarabu,bila order na hakutaka kuja.

Mimi siamini kwa namna ripoti ilvyoandaliwa kitaalam na Mwakembe kwamba hakuona umuhimu wa kumwita EL baada ya kuonekana kuhusishwa kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Kamati kwa ustaarabu mwingine nadhani wakaamua kumstiri kwa kutosema kuwa alikataa na kwa kuwa hakuitwa kwa order then hakuna ushahidi.

ASitufanye Watanzania wajinga saana.Ni mwizi na aende kuzimu kama siyo jela.
 
Hii imeingia sasa hivi ...

Msabaha naye aachia ngazi!
 
Bado tuko naye sambamba. next step katika uwajibikaji ni kufunguliwa mashtaka ya uzembe, ulaghai, kujinufaisha isivyo halali na na kulingizia taifa hasara ya mabilioni. it is not over yet!
 
Lakini JK itabidi vilevile awachukulie hatua za kisheria, especially kwa wale ambao wako directly involved kulitia taifa hasara. Kujiuzulu pekee hakutasaidia, wawe prosecuted!!!!

Watanzania jamani wakati ni huu, kwa nini kila kitu tunataka tufanyiwe? JK yeye ni Raisi wala si mahakama wala polisi walanini, kama watu wamekutwa na makosa wahusika wafanye kazi yao mara moja na si kumsubiri JK otherwise na wao tuwanyanganye kazi.

Tabia hii hii ya kufanyiwa vitu ndio iliyofanya Tanesco iingiliwe kazi yake, siku nyingine hakuna umeme watu watamlilia JK awaletee umeme wakati kuna taasisi zinazotakiwa kuleta umeme.

Siku nyingine mtu anaumwa homa ataomba JK akampime homa.

Jamani tujifunzeni kutowasubiri wengine watufanyie kazi.
 
Asante mungu kwa kusikiliza maombi yetu.Tunaomba mungu endelea kuwa nasi katika mapambano haya.Tumedhulumiwa vya kutosha sasa tunataka haki.

Hongera wana JF kwa kuendeleza mapambano haya mpaka sauti yetu imesikilizwa.

Hongera Dr.Mwakyembe...

Hongera watanzania wote huu ni ushindi kwenu.

Wembe
 
Sasa huyu nayeanajiuzulu nini wakati nafasi yake tayari ni badili...asijifanye alikuwa na nia ya kujiuzulu maana Waziri Mkuu akijiuzulu Mawaziri Wote moja kwa moja wanakuwa hawana kazi (Katiba ya Jamhuri Ibara ya 57(2) kifungu kidogo (e)).

Katiba pia kama nimesoma na kuielewa vizuri haisemi kuwa kujiuzuru kwa Waziri Mkuu ni LAZIMA kuthibitishwe na Rais wa Jamhuri, kwa mujibu wa Ibara ya 51 (3) kifungu kidogo (C).

Hivyo hao wakina Karamagi na Msabaha wanacheza mchezo wa ukuti hapo bungeni...kazi hawana tangu asubuhi.
 
Kufunguliwa Mashtaka- je Mahakama nayo Tanzania tunaiamini?

Haitakuwa kama yale ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Tabora?
 
Tusidanganyane

Hivi kwa nini serikali nzima isijiuzulu tuu tukajua moja?

Hivi nani anaamini kuwa wafisadi ni hao tuu?
 
Nafikiri nchi nzima ina matatizo, yaani kila kitu kinakwenda hovyo hovyo.

Nafikiri wizara zinaongozwa kjinga kijinga na hiyo ni mbali ya matatizo ya rushwa.

Hawa viongozi hawatakiwi kujiuzulu wanatakiwa kuwa sacked.
 
Back
Top Bottom