Niupumbavu sana watawala kutaka wote tuipe pambio zaoAsipangie watu cha kuongea kwenye kampeni. Kila siku tunasikia rais wetu akibeza mambo ya hovyo yaliyofanyika awamu zilizopita, ni kwanini yeye awazuie watu wengine kuyasema ya hovyo ya awamu hii? Inaonekana awamu hii inataka kampeni zifanyike kwa utashi wa rais aliye madarakani.
Kichwa ni chake Ila ubongo ni jiweMajaliwa ninayemfahamu hawezi kuongea utumbo kama huu.
Hapo sasaHao anaodai watafanya vurugu ni kina nani? Je amesahau huyuhuyu aliyeshiriki kuiua EAMW ndiye huyohuyo aliyejitakasa... aaah nikomee hapo
mmechota hela za umma mmenda kununua korosho,،halafu mkala hasara ,hizo bilioni 600,zingetosha kupeleka MADAWA nchi nzima,mmezitupa kwenye korosho nyinyiiiiiiiiiWaziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wanasiasa kufanya kampeni za kistaarabu mara kampeni za uchaguzi mkuu zitakapofunguliwa ili kuepuka vurugu zinazoweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini.
Akizungumza katika ibada ya siku kuu Eid Al Adha Jijini Dar es Salaam, Majaliwa amesema kuwa ni muhimu kwa wanasiasa kueleza yale waliyopanga kuwasaidia wananchi kuliko kubeza yale yaliyofanywa na wengine na kukashfu.
“Tujiepushe na lugha za uchochezi, tujiepushe na lugha za bezo, tujiepushe na lugha za kashfa kazungumze kile ambacho utawatendea wananchi” amesema Majaliwa
Waziri Mkuu pia amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuimarisha amani na mshikamano nchini kwa kutoa mawaidha mazuri yenye lengo la kujenga jambo ambalo limekuwa msaada mkubwa kwa Taifa.
Akielezea kuhusu hayati Benjamini Mkapa ,amesema kuwa waislamu watamkumbuka kwa kuanzisha Chuo Kikuu cha waislamu kwa kutoa majengo ya Serikali na kukabidhi kwa waislamu na hivyo kuanzishwa kwa Chuo Kikuu hicho kilichopo mjini Morogoro.
Ippmedia.com
safii mkuu,corona inaweza kutusaidia kumvugumisha apotele mbaliMatumaini pekee kwa watanzania yamebaki kwenye corona kufanya kama kwa NKRUNZINZA
Mheshimiwa tunaelekea kubaya,nasema kubaya iwapo mwanasiasa mpinzani anachaguliwa jambo la kusema na mtawala,kusema azungumzie atakayofanya bila kubeza yaliyofanyika imekaakaaje hii?nitasemaje nitaboresha shirika bila kueleza kasoro kwa aliyetangulia kujenga shirika?nitajengaje SGR vizuri bila kuonyesha kasoro kwa huyu aliyejenga hii SGR?au si ndio kubeza huko?Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wanasiasa kufanya kampeni za kistaarabu mara kampeni za uchaguzi mkuu zitakapofunguliwa ili kuepuka vurugu zinazoweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini.
Akizungumza katika ibada ya siku kuu Eid Al Adha Jijini Dar es Salaam, Majaliwa amesema kuwa ni muhimu kwa wanasiasa kueleza yale waliyopanga kuwasaidia wananchi kuliko kubeza yale yaliyofanywa na wengine na kukashfu.
“Tujiepushe na lugha za uchochezi, tujiepushe na lugha za bezo, tujiepushe na lugha za kashfa kazungumze kile ambacho utawatendea wananchi” amesema Majaliwa
Waziri Mkuu pia amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuimarisha amani na mshikamano nchini kwa kutoa mawaidha mazuri yenye lengo la kujenga jambo ambalo limekuwa msaada mkubwa kwa Taifa.
Akielezea kuhusu hayati Benjamini Mkapa ,amesema kuwa waislamu watamkumbuka kwa kuanzisha Chuo Kikuu cha waislamu kwa kutoa majengo ya Serikali na kukabidhi kwa waislamu na hivyo kuanzishwa kwa Chuo Kikuu hicho kilichopo mjini Morogoro.
Ippmedia.com