Katakata ya umeme imeanza upya kuelekea uchaguzi mkuu, hapa kirumba Mwanza umekatwa.

tripof

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2024
Posts
829
Reaction score
1,120
Hili suala la kukatika umeme limeanza upya mbali na kuaminishwa na Naibu Waziri Mkuu kuwa limekwisha baada ya Mitambo kuanza kufanya kazi Rufiji. je kulikoni leo huku Kabuhoro wamekata muda mrefu tu bila taarifa.TANESCO iko shida kubwa, Watamharibia mama.
 
Kabuhoro milimani huko kwa walevi wa wanzuki na gongo? Kuna wavuta bangi wengi sana, walau ungesema ibanda ningekuelewa
 
Nahisi kuna watoto wameachiwa swichi hapo tanesco maana siku za mechi lazima umeme utakatika tu haswa timu ya Bongo ikiwa inafanya vizuri hizi za watani, hua najiuliza profesionalizm iko wapi.. Nchi zingine umeme ukikatika watu wanaandika ripoti za maana na ikionekana kuna uzembe, wanawajibishwa ila huku kwetu ukisikia kuna Mechi ya Watani basi hakikisha simu yako imejaa chaji maana siku iyo lazima umeme ukatike, Siku nikipewa cheo hata cha Unaibu waziri kumaanisha! Kuna watu wataonja joto ya jiwe.. upumbavu kama huu siwezi kuuvumilia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…