Katavi: Wavuvi Nsimbo wameomba kurudishiwa pesa zao kukatiwa vibali vya uvuvi

Katavi: Wavuvi Nsimbo wameomba kurudishiwa pesa zao kukatiwa vibali vya uvuvi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Wananchi waliokuwa wakifanya shughuli zao katika Mto Katuma ulioko Kata ya Sitalike, Halmashauri ya Nsimbo Mkoani Katavi wameomba kurudishiwa pesa zao walizotoa kwa ajili ya kukatiwa vibali vya uvuvi ambavyo havikuainisha eneo rasmi ya kufanyia shughuli hiyo.

Meleji Mollel ambaye ni Afisa Hifadhi Katavi na Daniel Walakunga ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nsimbo wamesema shughuli za uvuvi zinazingatia maelekezo ya mipaka ambapo vibali vyote haviruhusu kuingia katika hifadhi ya Katavi.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusuf amesikitishwa na wananchi hao kutofanya shughuli hiyo ipasavyo ambapo ameagiza pesa walizotoa kwa ajili ya kupewa vibali zirudishwe kwa wananchi haraka.
 
Back
Top Bottom