Kati ya Burhani na Hemeti nani ashinde Sudan

Kati ya Burhani na Hemeti nani ashinde Sudan

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Mapigano mengine makali ya wenyewe kwa wenyewe yameibuka nchini Sudan.Safari hii ni kati ya general Abdel Fattah al-Burhan ambaye ndiye kiongozi wa nchi hiyo kwa sasa na mkuu wa jeshi. Mpinzani wake ni general Mohamed Hamdan Dagalo maarufu kama Hemeti na ambaye ndiye naibu katika utawala wa sasa unaitwa wa mpito kuelekea utawala wa kiraia.
Majeneralji wote hawa walikuwa ni sehemu ya uongozi wa kijeshi wakati wa utawala wa rais Omar albashir.Katika maandamano yaliyopelekea kuondolewa madarakani kwa albashiri general Burhani alijionesha kama mtu aliyewaonea huruma sana wananchi na hata kutembelea maeneo waliyokuwa wamejikushanya jijini Khartoum na kutaniana nao.
Kwa upande wake general Hemet alikwishashutumiwa na taasisi za kimataifa kama mshiriki mkuu wa mauwaj yanayotajwa kutokea Darfur na yeye alitajwa kama kiongozi wa Janjaweed. Katika uongozi wa baada ya kuondoka kwa albashir ambapo Hamdoh alikuwa kiongozi wa kiraia katika serikali hiyo,majenerali hao walishirikiana vizuri jambo ambalo halikudumu kwa muda mrefu kabla ya kutokea kutofahamiana tena kila mmoja akiwa na wafuasi wake na ambapo Hamdoh aliwekwa pembeni hapo mwaka juzi 2021.
General Hemet amekuwa na jeshi lake linaloitwa RSF ambalo ni mwendelezo wa vikosi tangu enzi za Albashir vilivyotumika kuzima uasi maeneo mbali mbali ya nchi hiyo ikiwemo Darfur.General Burhani pamoja na kuwa ni kiongozi wa kijeshi tangu enzi za Albashiri kwa sasa ndiye mkuu wa jeshi la ulinzi na mkuu wa nchi kuelekea utawala wa kiraia.
Kipengele kinachotajwa kupelekea kutoelewana kwa majenerali hao kwa sasa ni namna ya kuviingiza vikosi vya RSF katika jeshi rasmi la nchi na muda wake.Wakati Hemet akitaka iwe ni kitendo kinachotakiwa kiendelee kwa muda mrefu hata miaka 10 ijayo kutoa fursa ya kuaminiana na kupata ufanisi.Kwa upande wake general Burha ametaka iwe ni jambo la kufanyika kwa haraka.
Mbali na kutajwa kuwa alihusika na mauwaji ya Darfur,general Hemeti kwa sasa anatajwa kupokea misaada ya kijeshi kutoka Urusi baada ya kuwafungulia njia katika uendeshaji wa migodi ya dhahabu ya nchi hiyo wakati mwenzake Burhani akitajwa kuwa na ushirikiano mkubwa na vyama vya kisjiasa vya mrengo wa kiislamu vilivyowahi kutawala nchini humo.
Hapo juzi kulionekana harakati kubwa za vikosi vya RSF za kuhamisha silaha kuelekea maeneo tofauti ya nchi karibu na jiji la Khartoumj kitendo kilichotajwa na ujpande wa Burhan kuwa kumefanyika bila ushirikiano wa kijeshi na jeshi lake.Siku iliyofuata hapo juzi vita kamili vilianza huku Hemeti akitangaza kushikilia ikulu na viwanja vya ndege na upande wa Burhani kukanusha huku ukitumia ndege za kuvita kushambulia maeneo kadhaa ya jiji hilo.
_129371206_239b828587d5bb938cca33d701bc2d4abca5108b0_230_5500_30921000x563.jpg

general Mohamed Dagalo (Hemeti)
15sudan-Abdel-Fattah-al-Burhan-articleLarge.jpg

general Abdulfatah AlBurahan
AP23105459336254.jpg
 
Hawa wanafanya biashara kubwa ya silaha. Kwa hiyo vita kwao ni biashara
Wewe mpuuzi unaweza taja silaha zozote za kimarekani zinazotumika kwenye vita Africa hii ,? , Kuna nchi au kikundi cha uasi kinaweza nunua silaha za kimarekani Africa hii ?,hivi ninyi vichwa vyenu huwa vina kinyesi cha wapi ? ,Mbona huwa ni wapuuz hivyo ?
 
Wewe mpuuzi unaweza taja silaha zozote za kimarekani zinazotumika kwenye vita Africa hii ,? , Kuna nchi au kikundi cha uasi kinaweza nunua silaha za kimarekani Africa hii ?,hivi ninyi vichwa vyenu huwa vina kinyesi cha wapi ? ,Mbona huwa ni wapuuz hivyo ?
Hizi hasira za kutukana watu dalili ya ufukara wa hoja ndugu. Staarabika sio Kila kitu mpaka utukane ndo ueleweke.
 
Hawa wanafanya biashara kubwa ya silaha. Kwa hiyo vita kwao ni biashara
Wewe mpuuzi unaweza taja silaha zozote za kimarekani zinazotumika kwenye vita Africa hii ,? , Kuna nchi au kikundi cha uasi kinaweza nunua silaha za kimarekani Africa hii ?,hivi ninyi vichwa vyenu huwa vina kinyesi cha wapi ? ,Mbona huwa ni wapuuz hivyo ?
 
Wewe mpuuzi unaweza taja silaha zozote za kimarekani zinazotumika kwenye vita Africa hii ,? , Kuna nchi au kikundi cha uasi kinaweza nunua silaha za kimarekani Africa hii ?,hivi ninyi vichwa vyenu huwa vina kinyesi cha wapi ? ,Mbona huwa ni wapuuz hivyo ?
Silaha nyingi ni za mrussi sababu ni bei rahis ndo zinatumika afrika mfano AK 47
 
Yaani kuna watu ni mambwa sana ,hujui hata historia ya hiyo nchi , chuki za kidini na kikabila zilizomo humo ,mauaji ya Darful nayo yalisababishwa na mmarekani au sio ,? ,Civil war iliyosababisha mpaka kujimega kwa south Sudan ilisababishwa na Marekani sio ?
Kenge
 
Huyo hemet kiongoz wa janjaweed hatakiwi kabisa kwa sababu kitu walichokua wanawafanyia waafrika kule darfur ulikua ni ukatili mkubwa sana
Habari nyingi zilizohusu Sudan kabla kupinduliwa kwa Omar Albashir zilikuwa na lengo la upotoshaji,.Hivyo mimi siwezi kumtaja generali Hemeti kama unavyosema wewe.
Ukitaka kujua kuwa upotoshaji ulikuwa ni mkubwa ni katika kusemaj kuna makundi ya waarabu wakiuwa waafrika.Hilo kwa Sudan ninayoijua mimi halipo.Kiarabu ndio lugha kuu ya wenye rangi na weusi.Hata ukiangalia safuj zote za uongozi watu wenye rangi nyeupe ni wachache sana.
 
Back
Top Bottom