Kati ya matofali ya kuchoma na ya saruji unachagua yapi?

Kati ya matofali ya kuchoma na ya saruji unachagua yapi?

Huenda tunazungumza kitu kimoja lakini kwa lugha tofauti, nimeelewa lakini hadi hapa tulipofika ilikua sababu ya kile umeandika mwanzo. Btw nimeelewa vizuri tu nn ulimaanisha

Sema hiyo paragraph ya kwanza ni kama zile za uswahilini mkiwa mnajadili jambo utaskia mmoja anasema "...huyu anajifanya kasoma sana..."
Its a reckless statement ambayo Ina lengo la kufanya blackmail😂😂
Mwishowe nimejikuta natoa hizo kauli, ukweli unaujua ila unataka kuleta pigo za wanasheria utafute ka angle kamoja kabadilishe context nzima, wewe ulipaswa kusomea sheria tu.

Sikuwa na lengo la kuku-blackmaili, kuwa na amani mimi nipo hapa kujadili hoja.
 
Kwahiyo hujaona umuhimu wa kujadili udongo wa sehemu linapoenda kujengwa ghorofa au jengo.?


Unadhani namna ya kuuanza ujenzi wa ghorofa kwenye udondo wa kichanga (unaotitia kirahisi) na ule wa kawaida utakuwa sawa.?

Kwenye ghorofa huko ni mbali sana, jiulize anayejenga shimo la choo kwenye sehemu yenye udongo mfinyanzi (ambao obviously haunyonyi maji kirahisi) atakuwa na procedures sawa na anayejenga shimo hilohilo kwenye udongo wa kawaida unaonyonya maji kirahisi na kutitia kiuwepesi.?

Kaka tusifike mbali bwana😁
Mkuu narudia kusema hizi procedures ni kwenye commerical buildings na wale wa sky scrappers
Ghorofa nyingi za kuishi unazoona watu wamejenga kuholela bila hizo procedures. Of ourse procedures zinapaswa kufatwa lakini pamoja hazifuatwi bado wameweza kusimamisha hizo ghorofa na ndio hapo tulikua tumeanzia.
 
Mwishowe nimejikuta natoa hizo kauli, ukweli unaujua ila unataka kuleta pigo za wanasheria utafute ka angle kamoja kabadilishe context nzima, wewe ulipaswa kusomea sheria tu.

Sikuwa na lengo la kuku-blackmaili, kuwa na amani mimi nipo hapa kujadili hoja.
Thanks nami nimeelewa vyema tu nilikua naweka sawa hiyo paragraph yako ya kwanza😂😂
 
Mkuu narudia kusema hizi procedures ni kwenye commerical buildings na wale wa sky scrappers
Ghorofa nyingi za kuishi unazoona watu wamejenga kuholela bila hizo procedures. Of ourse procedures zinapaswa kufatwa lakini pamoja hazifuatwi bado wameweza kusimamisha hizo ghorofa na ndio hapo tulikua tumeanzia.
Ooooh hapo sasa nimekuelewa, kama ni hizo za kuishi na zile zinazojengwa kiholela pengine watu wanajenga tu bila kuzingatia hizo procedures, NI KWELI wanajenga hata mimi najua.

Ila mimi sikutaka kujadili ujenzi wa Ghorofa katika context ya kulijenga kiholela, mimi nilikuwa najadili as how inatakiwa kuwa kitaalamu, ndomaana hatukuelewana.

UWE NA USIKU MWEMA MKUU.
 
Ooooh hapo sasa nimekuelewa, kama ni hizo za kuishi na zile zinazojengwa kiholela pengine watu wanajenga tu bila kuzingatia hizo procedures, NI KWELI wanajenga hata mimi najua.

Ila mimi sikutaka kujadili ujenzi wa Ghorofa katika context ya kulijenga kiholela, mimi nilikuwa najadili as how inatakiwa kuwa kitaalamu, ndomaana hatukuelewana.

UWE NA USIKU MWEMA MKUU.
But sababu ya kufika huku ilikua ni je ghorofa litasimama, hapo ndio tulianzia bila hizo procedures za mwanzo ulizosema
 
Ukijenga kwa satandard zote ni imara ila zikitengenezwa kwa kubumba lazima zitakuwa za hovyo! sasa mtu tofali za saruji unatoa tofali 45 hadi 50 unategemea kweli zitakuwa nzuri? Jaribu kutoa 30 au 25 uone zitakavyotoka kama chuma
Sisi hapa Nyumba ya urithi mzee alijenga kwa saruji, tofali alinunua wapi sijui miaka ya 80 huko......
Kuta zipo ngangari kinoma msumari haupenyi Hadi concrete nail ndio zinapita kwa shida sana.
 
Nilibishana na rafiki yangu, yeye ameamua kujengea matofali ya kuchoma. Anasema ubora wa tofali la kuchoma liliokwa sawa sawa unazidi matofali ya saruji. Yeye pesa anayo ila ameamua kutumia matofali ya kuchoma katika ujenzi wake. Hivi ni kweli kuwa matofali ya kuchoma ni bora kuliko ya saruji?

Nilichomwambia ni kuwa, matofali ya kuchoma unauhakika ni udongo 100% kuliko upate ya saruji yawe 1/3 ni mchanga na 1/4 ni saruji. Lakini kuhusu uboara hui sina uhakika.

View attachment 1877635
Matofali ya kuchoma

View attachment 1877638
Matofali ya saruji


Za kuchoma ni imara zaidi.
 
Kwa life expectancy ya Tz na kipato cha kududuliza usihangaike kujengea tofali za kuchoma ni imara zaidi lakini inaitaji ukamilishe kila kitu unapoanza kujengea.

Tunaishi miaka isiyozidi 90 ukibahatika ujenzi wa wengi leo msingi mwakani boma mwaka kesho kutwa kupaua za saruji ni rafiki kwa hilo utaishi utakufa mwanao atarithi nae atakufa atarithi mjuu wako pia.
Kule Kijijini kwetu tofali zinazotumika zaidi ni za kuchoma. Nami nyumba yangu nimejengea tofali za kuchoma ila nilipiga plaster, yaani nyumba iko poa sana. Halafu nikajenga nyumba ya Wazazi wangu kwa tofali za kuchoma, sikupiga plaster, nilifanya pointing. Nyumba inapendeza ni balaa.
 
Ni kwasababu hatuna utaalamu mzuri wa kuoka matofali. Ulaya wanatumia matanuri ya gas na wanaoka kwa wingi kibiashara.

Kuna Mwarabu mmoja hapa kwetu ni mshika dini sana, yeye anafuata ratio ya 30:1 bag katika matofali ya saruji. Kwa kununua huyu anaaminika na matofali yake yananunuliwa sana.
hyo ratio bado ni famba, ratio sahihi ni 25:1, kuna mzungu ar alikuwa anafyatua kwa 20:1, tofauli linakaushiwa ndani kwenye unyevunyevu, ukienda kununua anakupa usafiri, ukifika site hakuna mambo ya kupakua moja moja, kitu inapigwa tip, likimeguka hata moja anakurudishia hela anarudi na tofali lake
 
Ninadhani unasababisha ubishani usio na sababu. Mtoa post aliuliza kiujumla. Na baadhi ya wachangiaji tumemjibu kuwa kama mambo yatafanyika kikanuni, kwa tofali zote, kuchoma ni namba moja. Wewe post hii ndo umeonesha kuwa kumbe unakiri la kuchoma ni kiboko mradi tu viwango viwepo. Ile hoja yako ya mwanzo hadi nikakujibu vile ni kwa vile uliongea kiujumla tu. Yani kama unafundisha basi mwanafunzi anaelewa la kuchoma halifai, na sababu ni vile huoni watu wakijengea. Hii ni dhambi aisee!

Halafu bado hoja zako si madhubuti sana. Eti za kuchoma hutumiwa na masikini. Umeipata wapi hii? wabongo baadhi kwa kutojua ama sababu za kimazingira ndo huchagua saruji. Na wanatumia matofali ya kiwango cha chini mno. tofali unakuta 1:40. ndo majengo yaliyojaa miji yetu hasa Dar na maeneo jirani. Sababu kubwa kwa hapa kwetu watu kutumia ya kuchomwa ama saruji ni mazingira. Mpaka mkazi wa Dar pale magomeni apate tofali la kuchomwa litamfikia kwa kiasi gani? Hali hii ni tofauti ukiwa Iringa. Yale majumba ya wazee vibopa wa Kikinga kule Kihesa na Gangilonga yote ni tofali za kuchomwa. Kuna nyumba zimejengwa Dar mwaka jana, lakini haziingii kwa nyumba zile aisee zenye miongo kadhaa. Kakague chuo kama Mkwawa, sekondari kama Ifunda n.k. kisha njoo utuambie ule ni umasikini ama la.

Cha ajabu, ukizungumza kuhusu saruji, unataja standard hiyo ya 1:25, na hzi za kuchomwa pia zina viwango vyake, vikifikiwa ni bora zaid ya saruji. Na wangapi bongo wanajengea tofali za 1:25? Tumuogope Mungu aisee!
Mkuu you have nailed. Mimi nimesoma Ifunda, yale Mabweni yetu yalijengewa tofali zilizoandaliwa kwa kuchomwa hapo Ihemi miaka hiyo ya 1920 lakini hadi leo ni kama jengo la jana tu. Kuna kipindi alikuja Wazir Mkuu Mstaafu Marehemu Mzee Kawawa hapo Ihemi akawahamasisha matajiri wajenge Kiwanda cha Vigae maana udongo uliopo hapo ni mzuri kwa matofali ya kuchomwa pamoja na vigae. Kwa kipindi hicho matajiri walikuwa hawapendi sana ishu za uwekezaji sababu ya masuala ya ujamaa hivyo kiwanda kikaishia katika maono tu..
 
Back
Top Bottom