Kati ya Mawaziri hawa; Nani unadhani atafuata kurejesha nyumba ya Serikali hivi karibuni?

Hizo ni zao, tutajenga nyingine kama shida ni hela tutakopa
 
Para ya pili toka mwisho inamaana sana, vyeo vitangazwe, au mtu akichaguliwa na Raisi adhibitishhhwe na kamati ya bunge ya utumishi itakayondwa na wabunge mchanga yuko. Wakiona Hana tija kwa taifa, wanatoa mrejesho anatafuta mwingine.
 
Rizi na january? Hapo meza mawe tuvumilie tu hadi wazeeke
 

Nafikiri haya ni majadiliano ya ndani ya Mnafu - mboga mboga
 
Kwa bashe umekosea, ndo kwanza ana miezi 3 ya uwaziri
 
2-3 excellent
1 hakuwa mwadilifu
Hapana mpaka Sasa hajathibitishwa kuwa aliiba wapi zaidi ya harakati za KIMTANDAO za kumtoa kwenye nafasi ya kupata Urais. Waliona alikua na kila nafsi za kupata Urais kama alivyo Ruto na Uhuru.
Hata hivyo Kwa Afrika Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kamwe wasipate nafasi ya kugombea Urais baada ya Rais anayekua madarakani kumaliza muda wake.
Il ilifanyika ili kubaki na mwiko huo mana Waziri Mkuu ndiye Mtendaji mkuu wa Serikali akiachwa akajipanga kuanza harakati za kugombea Urais ni hatari sana Kwa wengine mana ana nafasi ya kujipanga mpaka kitongojini na akafanikiwa kirahisi kupitia cheo chake. Lowasa hata kama angekuwa msafi kama Theluji lazima angeundiwa zengwe na watu wa sistm wenyewe ili asije akajipanga na akafanikiwa kumrithi Kikwete. Na Kwa Taarifa yako Role modal wa JPM alikua ni Lowasa kiutendaji.
Katika wote Mawaziri waliofanikiwa katika suala la maendeleo ya Haraka ni Lowasa na JPM. Lakini aliyekua na mtandao mkubwa na mvuto wa kuwa Rais alikua ni Lowasa zaidi hasa kutokana na uwezo wake,uvumilivu wake , ujasiri wake , busara zake na mipango yake ya kiuchumi na suala Zima la ndoto ya kuwapatia watoto wa kitanzania Elimu. Alijenga shule za kata nchi nzima Kwa Mwaka mmoja. Akiwa Waziri wa maji alipuuza Kwa ujasiri mkubwa mkataba wa Kikoloni wa maji Toka ziwa Victoria. Kwa muda mfupi maji yalikua yanasambazwa Kanda ya ziwa kuelekea Dodoma Kwa Kasi ,lakini alipoondoka mpaka Leo hayajafika Dodoma Kwa sababu ya pesa zilizokuwa zimemwagwa zilizokuwa na Misri Kwa wanamtandao waliotumika kumchagua zaidi na kujenga hofu kwenye mfumo kuwa tutaingia kwenye matatizo na Misri Kwa msimamo wake. Wakaanza kumtafuta tangu wakati huo alipokua Waziri wa maji.
Waliposikia amekua Waziri Mkuu ndio wakajua Sasa anaweza hata akafunga maji yasiende Misri hofu ikawajaa ndio wakawa wanamtafuta asije akaupata Urais.
Alikua anatafutwa ndani na nje ya nchi na pia kwenye mfumo wa kuhakikisha kuwa Waziri Mkuu hajiinui na kuupata Urais.

Usione ni Kwa nini Kwa Sasa Yule Waziri Mkubwa wa TZ anaonekana amepunguza kasi na mara Kwa mara anapondwa na kukosolewa na ngazi zile za Juu aende mdogo. Ni suala la kumfanya Waziri Mkubwa ajiepushe na mitandao na Mawazo ya kiruto ya miaka minne Kenya anawaza Urais badala ya kuwaza maendeleo ya Kenya.

Kwa hiyo Lowasa hakuwa Mchafu Bali alichafuliwa mana kwenye migao hajawahi kutajwa kuwa amepewa Rushwa kama akina Sandarusi wakati wa Escrow.
Hapa simzungumzii Lowasa wa 2015 baada ya kuwa amepigwa na kitu kama biological weapon na wanamtandao ili asikatize na kuupata Urais mana pamoja na kujiuzulu lakini Bado alionekana kuwa ndiye anayefaa hasa kutuvusha.

Mbadala wa Lowasa alikua ni JPM kiutendaji. Lowasa hata kivuli chake kilikua kinatisha kama alivyomuwa Mrema.

Ni viongozi watano TU mpaka Sasa waliotisha hata Kwa kivuli Chao yaani picha:-
(1)JK. Nyerere.
(2)Edward Moringe Sokoine
(3)Augustine Mrema.
(4)Edward Ngoyayi Lowasaa.
(5)John Pombe Magufuli.

Sifa zao kijamii ni kama ifuatavyo,:-

Watatu weusi na Wawili weupe.
Wawili Wana nywele za mvi za kuzaliwa na watatu nywele nyeusi.

Wawili Wana viipara kichwani na watatu hawana vipara.

Kati yao Wawili Wana sura ya kutabasam na mvuto na watatu Wana sura za ukauzu.
Watatu wanaongea Kwa utani mwingi na Wawili wanaongea bila utani.

Watatu wanathamini sana makabila yao ya kifugaji na hata kudhaniwa kuwa wanaukabila na Wawili hawakujali sana ukabila Kwa wazi ..

Watatu walitokea Kanda ya Kaskazini na Watatu Kanda ya ziwa.

Wawili walipata Urais na Watatu hawakupata Urais.

Watatu wametangulia Mbele za haki na Wawili Bado wapo hai.

Wawili walijiuzulu uwaziri mkuu.

Na Wawili walifarikii wakiwa madarakani.

Wawili walikua wanatokea kabila Moja la Wamaasai.
 
Hakuna waziri hapo hata mmoja ... Ila Riziwani bado Wacha tumpe muda
 
Kwa taarifa yako Lukuvi amekuwa waziri tangu 1995 Mkapa akiingia madarakani akiwa waziri katika ofisi ya waziri mkuu wakati huo Sumaye na akaendelea katika wizara tofauti kwa awamu zilizofuata ( lakini siyo wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi. Wizara ya ardhi alianza awamu ya tano ya JPM).
 
Hayo ni maoni yako japo umeandika kurasa nyingi mno.
Mtaje Waziri mmoja TU aliyeupiga mwingi Kwa kuibuliwa na JPM. Yaani aliyeweza kufanya kazi kama yeye wakati alilipokuwa Waziri wa Ujenzi. Ndio maana alikua anawafokea hadharani mana walikua wapo underperformance isipokuwa Lukuvi peke yake.
Hata Makonda aliibuliwa na JK na kupewa uDC kinaondoni.Japo alijisahau na kufanya mambo ya hovyo lakini alikua ana mwangwi wa uthubutu na alikua anafaa kuwa mnyapara endapo angeenda Gerezani.Angekua na cheti chake hata kama ni Cha Nursary angefaa sana kuwa Waziri wa wizara Moja wapo inayosumbua. Ana uwezo wake binafsi wa kuthubutu. Kwa Sasa ameshanuka kama muuza butcher. Hafai Tena !!

Sijasema kuwa Tatizo ni JPM kwenye kuwaibua Mawaziri wenye uwezo au askari wa mwavuli la hasha tatizo ni Chama Cha Mapinduzi kuondoka kwenye dira ya kuandaa viongozi na kubaki na mfumo wa viongozi chawa na Sasa mama anapata shida ya kupata viongozi ndio maana anateua angalau wazoefu wa awamu za zamani ili wamsaidie.
 
Huyo wazir kapata remote hpo wizaran. Hanna maamuz
 
Da Joi Ndalichako Muache Siyo Rahisi Kuachia Ngazi
Zabayanga Yupo Anambeba Haraka
Wapo Tele Uliowaja Kuachia Ngazi
 
I₩€ "'vq@!l€ q!q! #0l₩@ng0 l0g0 ¿ 0l€q€l€ €!t!"'@ .
====
Jaribu kuvunja kizuizi cha utambuzi hapo juu mleta mada! Ha ha ha haaa
 
Mbna Kina lukuvi kawatoa.. awamu ya Tano na sita kiukwel haijatoa mawazir wenye uthubutu, labda kangi lugola alithubutu, Jpo mwishon alionekana kituko. Itachukua muda na wengi wanaonekana waoga kuthubutu maana hizo nafasi muda wowote unatolewa ubabaki kuchekwa na kidhihakiwa na watu. So wengi wamejifunza kufanya vitu vyao kimya kimya. Jafo Naye mwanzon alipopewa tamisem alikuwa mkali sana baadaye akalegea
 
Khee! Hata kipindi cha probation bado! Halafu angalau ungekuwa specific flani amefail ktk nini? Kwa mfano, Ridhiwan ndiyo unamuonea tu. Hiki ulichokiandika ni fallacy generalization.
 
Magu kamwibua bashe
Ni marcenary!! Ikitokea vita na somalia atatugeuka.

Yupo kibiashara zaidi angefaa apewe Wizara ya mipango. Kilimo bado hajaweza kuibua mbinu za kuifanya Tanzania kuwa Taifa la kuzalisha na kuuza Chakula Afrika nzima na Ulaya.
Tatizo sio Mbole TU . Tanzania ni nchi ya pili Kwa mifugo barani Afrika. Anapaswa ahamasishe matumizi ya Mbolea ya asili Kwa kiwango Cha juu mpaka pale wazalendo watakapozaliwa na kuweza kugundua mbinu za kutengeneza Mbolea za viwandani. Wafanyabiashara wakiona wananchi wameamka na kuzalisha bila kutegemea mbole zao za dili watashusha Bei wenyewe.
Tuna wafungwa maelfu wanajambiana TU magerezani wakati Kuna Malaki ya hekari za ardhi ambazo hazijalimwa na Kuna maji ya kumwagilia kutoka kwenye maziwa na mito na hata ardhini sijamsikia akiweka mikakati na majeshi yaliyoundwa Kwa ajili ya kujenga Taifa yaani JKT matokeo yake wanajazana makambini kuimba nyimbo za CCM yajenga nchi.
Mkoloni aliingia Tanganyika Kwa muda mfupi Tanganyika ikaonekana kwenye Ramani kwenye mkonge, karafuu, Pamba, korosho,michikichi, ngano(Bahati ) , maharage (Arusha) ,shayiri.Nazi Ukanda wa Pwani wote. Machungwa, maembe n.k mpaka Leo ni mazao hayo hayo ambayo yaaliibuliwa na wakoloni na kuanzishwa mashamba makubwa sana wakati huo Tena Kwa zana duni na mawasiliano duni .
Leo Viongozi Bado wanaacha ardhi inabaki kama maeneo ya watu kujimilikisha binafsi badala ya kuyalima kibiashara kupitia taasisi kama JKT na magereza ili pawe na akiba kubwa ya ardhi lakini inayozalisha.

Bashe anajitahidi Sina shaka naye ,awe Mzalendo kweli kweli na ajisikie Yuko nyumbani.,[emoji1787][emoji1787]
 
Para ya pili toka mwisho inamaana sana, vyeo vitangazwe, au mtu akichaguliwa na Raisi adhibitishhhwe na kamati ya bunge ya utumishi itakayondwa na wabunge mchanga yuko. Wakiona Hana tija kwa taifa, wanatoa mrejesho anatafuta mwingine.
Kuna Wilaya Moja nilifika nikamwona DED nikajiuliza huyu alipataje kazi hiyo mana Hana sifa kabisa hata maadili ya kitanzania na Kiafrika Hana. Yupo kama fasheni TU lakini hakuna ubunifu wowote. Tukiwa na teuzi za kama tu unyapara gerezani ambapo hakuna ubunifu hatutaweza kuendelea.
Pasiwe na nafsi za kuteuliwa TU kirafiki au kujuana au kupumzishana na kula Kodi TU eti walisoma pamoja n.k. Ni uhuni!!
 
Wakisharudisha nyumba za Serikali,labda Beatrice Kamugisha atachaguliwa kuwa waziri.
 
Kwa vigezo vipi?

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…