Kati ya timu ya Brasil na ya England ipi inapendwa zaidi.

Kati ya timu ya Brasil na ya England ipi inapendwa zaidi.

Hizi ni timu za taifa za soka. Pana mtangazaji pale Clouds FM aitwae Lwambano, sijui utafiti huwa anaufanya vipi, yeye anaamini ligi ya England ndio inapendwa zaidi eti duniani na hii huwa anaisemasema.

Leo kaja na timu ya taifa ya England eti inapendwa. Kwa kweli kanichanganya na kujiuliza hivi Brasil inaionaje? Ukiachilia tu timu ya nchi yake yaani Tanzania?
Brazili kwa muda mrefu imekuwa na mpira mzuri wa kuvutia (samba), hata kama huipendi basi unakuwa na shauku ya kuona vile wanatandaza soka. Kwa tuliobahatika kumwona nabii wa mwisho wa soka, Ronaldinho, alipokuwepo tulikuwepo.
England ni kama simba, ukimsikia Haji Manara akiongea, hutaamini timu anayoizungumzia haiweezi Prisons.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Sasa unataka wote washabikie kile unachoshabikia wewe!!
Sio mimi ni Lwambano anae tulazimisha kuamini eti England ni timu pendwa. Na hii kama ungeelewa kile nilichokiandika hapo juu.
 
Timu ya taifa ya England n overated Sana kwa ss wenye umri wa 33+wengi tunashabikia Brazil

Kiukwel timu ya England nimetokea kuichukia bila sababu za msingi

Ila ligi yao naielewa Sana na nakiri hakuna ligi yenye ushindan Kama EPL

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
England huwa wanahakikisha kitu chao kinatangazwa kwa kila juhudi ili kionekane kizuri hata kupita chako, na ukijitambua utapigwa vita kila kona.
 
Sio mimi ni Lwambano anae tulazimisha kuamini eti England ni timu pendwa. Na hii kama ungeelewa kile nilichokiandika hapo juu.

Wapo wanaoipenda na wasioipenda pia wapo. Ni kama Argentina na Brazili wako wanaozishabikia na wapo wasiozishabikia.


Mimi sikufichi, katika timu ambazo hazipo akilini mwangu, na haitatokea nishabikie ni England, Marekani na Brazil.
 
Acha kukariri,hiyo Brazil yako tangu ichukue ubingwa mwaka 2002 miaka iliyofuata 2006, 2010, 2014, 2018 hakuna maajabu yoyote iliyofanya. Kuna kizazi kimeongezeka cha 2000 ambapo wakati brazil wanachukua ubingwa (2002) hawakuwa na idea yoyote na soccer lakini sasa wana miaka 20+.

Kwa hiyo jibu swali ni utafiti upi unaokuaminisha kizazi cha 2000 kinaipenda Brazil? Halafu pia ni utafiti upi unakuaminisha kizazi cha 1980 kushuka kilichokuwa kinaipenda brazil bado kinaipenda pamoja na kuchabangwa 7-1 na Germany mwaka 2014?
Duh, kaazi kweli kweli! Mie sijazungumzia ubingwa hata Lwambano vilevile. Alichozungumzia Lwambano ni UPENZI kwa timu ya England kwa kuongeza SANA ilhali bila tafiti tu pana timu za taifa kama Brasil zinazopendwa mno na wanasoka dunia nzima.
 
Pole sana, kwanini uwe na 'stress' ndugu yangu kwa hao wapenda misifa?

Ndio maana nikasema, usilazimishe wote wakufuate wewe, kila mmoja na mapenzi yake. Mimi hapa ni shabiki wa kutupwa wa Argentina na Spain, but siwapi asilimia zote.
 
Brazili kwa muda mrefu imekuwa na mpira mzuri wa kuvutia (samba), hata kama huipendi basi unakuwa na shauku ya kuona vile wanatandaza soka. Kwa tuliobahatika kumwona nabii wa mwisho wa soka, Ronaldinho, alipokuwepo tulikuwepo.
England ni kama simba, ukimsikia Haji Manara akiongea, hutaamini timu anayoizungumzia haiweezi Prisons.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Walicho fanikiwa Ulaya ni kuua aina ya mchezo wa Latin America. Nilipata habari kuwa kila mchezaji yeyote atakaeibuka huko lazima aende Ulaya kwa njia yoyote, ndo maana utakuta siku hizi timu za taifa siku hizi zinzcheza soka la Ulaya.
 
Ndio maana nikasema, usilazimishe wote wakufuate wewe, kila mmoja na mapenzi yake. Mimi hapa ni shabiki wa kutupwa wa Argentina na Spain, but siwapi asilimia zote.
Lah! Nielewe, mie silazimishi watu waipende timu ya taifa ya soka ya Brasil ila kitendo anachofanya mtangazaji wa Clouds FM ya kutulazimisha anachokiamini yeye kuwa ndo cha dunia nzima ndo nakihoji hapa.
 
Lah! Nielewe, mie silazimishi watu waipende timu ya taifa ya soka ya Brasil ila kitendo anachofanya mtangazaji wa Clouds FM ya kutulazimisha anachokiamini yeye kuwa ndo cha dunia nzima ndo nakihoji hapa.

Poa mkuu Jacobus
 
England ni over rated tena na vyombo vyao vya habari. Hawana lolote wale. Tena ngoja wakutane na timu kama France, Italy, Belgium hapo ndo utaona ubovu wa England.
 
Heh, hivi mara yako ya kwanza kuangalia kombe la soka la dunia ilikuwa mwaka gani?
Nikwambie tu brazil ilikuwa inapendwa zamani lakini sio sasa, timu za taifa unaweza hamisha mapenzi, kwa mfano mimi kipindi brazil inapendwa karibia na kila mshabiki wa soka duniani nilikuwa nashabikia brazil na Germany lakini sasahivi naangalia wanacheza nani na nani nachagua upande, pia naangalia ni timu gani ya taifa inawachezaji wa club yangu ndio nashabikia
 
Duh, kaazi kweli kweli! Mie sijazungumzia ubingwa hata Lwambano vilevile. Alichozungumzia Lwambano ni UPENZI kwa timu ya England kwa kuongeza SANA ilhali bila tafiti tu pana timu za taifa kama Brasil zinazopendwa mno na wanasoka dunia nzima.
Duh umgumu kuelewa. Luambano kazungumzia uwezakano wakupendwa zaidi kwa england kwa sababu ya ligi yake kufuatiliwa zaidi. Ukiachana na England , huamini kama timu za taifa zinapendwa zaidi kutokana na mafanikio ya mara kwa mara kwa taifa hilo? Je huamini kama brazil ilikuwa inapendwa zaidi hiyo miaka ya 90 kutokana na mafanikio yake ya mara kwa mara kama vile 1998 kufika fainali na 2002 kuwa bingwa. Sasa kile kizazi ambacho hakijawahi shuhudia mafanikio ya brazil ni utafiti upi unakuaminisha kuwa kinaipenda zaidi brazil kuliko mataifa mengine?
 
Duh umgumu kuelewa. Luambano kazungumzia uwezakano wakupendwa zaidi kwa england kwa sababu ya ligi yake kufuatiliwa zaidi. Ukiachana na England , huamini kama timu za taifa zinapendwa zaidi kutokana na mafanikio ya mara kwa mara kwa taifa hilo? Je huamini kama brazil ilikuwa inapendwa zaidi hiyo miaka ya 90 kutokana na mafanikio yake ya mara kwa mara kama vile 1998 kufika fainali na 2002 kuwa bingwa. Sasa kile kizazi ambacho hakijawahi shuhudia mafanikio ya brazil ni utafiti upi unakuaminisha kuwa kinaipenda zaidi brazil kuliko mataifa mengine?
Ulimsikiliza au unazungumzia nilichokiandika kiushabiki tu? Mie nilimsikiliza na ndo maana nimehoji.
 
Back
Top Bottom