Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Kilichofanyika na Tundu Lissu kimezaa matunda ya mbegu zile zilizopandwaBaada ya hotuba ya TL, mjadala uliendelea. Safi kabisa. Lakini walichofanya wabunge waliobaki kujadili kilionyesha ni kwa kiasi gani TL alifanikiwa na kambi yake ya upinzani. Hawakuweza kujadili mswada badala yake walijadili hotuba ya TL. Umeona. Hizo ni Mbinu za wanyama wenye akili wanavyojielekezea fikra ili wanyama wengine wakali wasiwaumize watoto wao.Wananchi wameona jinsi gani wabunge wa ccm na tanzu zao walivyo na uwezo mdogo. Hii haina tofauti na kichaa anapofukuzwa na mzima, wazima wengine watamchukulia mzima kuwa kama kichaa. Kwa maana nyingine waliunga mkono hotuba ya Lissu na sio mswada.
 
MM na FJM heshima sana kweni. Absolutely brilliant contributions with exceptional insight and analysis.

Mijadala kama hii ina faida sana. You're the peak of the bunch!
 
MMM na FJM heshima sana. Your contributions with exceptional insight and analysis really made my day
 
Mimi nawapongeza chadema kwa kazi nzuri wanayofanya kwani bila kuhoji baadhi ya Mambo tungekuwa bado gizani!!!
Kwa mtanzamo wangu najua hata wabunge wa CCM hawana imani na utendendaji wa Rais Kikwete na ndiyo maana wanataka kumuondoa katika nafasi ya Uenyekiti Taifa!!!

Naomba wananchi kokote mliko ondoeni uoga tuseme kweli!!!
Hapa sio madaraka makubwa aliyopewa Rais Kikwete lakini ni uadilifu wa JAKAYA MRISHO KIKWETE sio Mzuri kabisa!!

Je ,Kwenye sakata hili la katiba , angepewa madaraka hayo SLAA wananchi wangelalamika ???
Je , angepewa Mwakyembe ,au Mangufuli, au Shivji wananchi Wange lalamika??
Angalia mawazo ya SALIMU ,KITINE, WARIOBA je, Kunatatizo???

Angekuwa Nyerere Kuna tatizo ???

Hapa Kikwete kama kikwete anapaswa kujua kuwa Wananchi hawamtaki kutokea ndani ya CCM ,serikali hadi upinzani !!!

Hata hao CUF nao hawamtaki Kikwete angalia tayari ndani ya CUF kumetokea mpasuko wa Kutaka kumutoa SEIF issue kubwa ni Ndoa ya Mkeka!!!

Nataka Watanzani wote tujadili mambo ya maana kuwa , Kikwete hawezi kusimamia mchakato wa Katiba mpya bali atafutwe mtu mwingine!!!

Jambo hili linajulikana hata ndani ya CCM!!!

Hofu iliyopo ndani ya CCM ni Mchakato wa kumupata mgombea Urais Mwaka 2015, wanajua Kikwete hawezi kusimamia sasa kama hawezi kusimamia Mchakato wa Kumupata mgombea ndani ya CCM anaweza kusimamia mchakato wa Katiba mpya unao husisha vyama vyote???

Tafakari !!! uwe mkweli!!! Ogopa MUNGU!!!! Usijilimbikizie Mali!!! kumbuka kunasafari ya kwenda India!!!

 

Kama usemayo ni kweli kuwa vyama vyote vya upinzani ni hopeless isipokuwa chadema na nccr huoni kuwa hapa walikuwa wanapambana na nguvu isiyo ya kawaida? Manake ni CHADEMA VS CCM+CUF+UDP+TLP!! Endapo wangefanya kile unachoshauri unadhani probability ya kufanikiwa ungewapa asilimia ngapi? Kama ni karibu na sifuri basi they were right haikuwa na maana kuhangaika kubaki mle ndani!
 

.....kwa neema nadhani. lol
 

Bwana pasco mi nadhani umekosa kitu kinaitwa spirit of revolution, na kama unayo ni ya kishabiki. Wabunge wa ccm ni weng i mara tano zaidi ya wabunge wa chadema, ukiongeza ccm B ya cuf ndo usiseme! Hawa watu kwa hali ya democrasia ya wengi wape bila hoja, wanaweza kupitisha sheria yoyote na wakati wowote. The time has come now to show them that some of the things wanatufanyia wananchi sio, kama kujichotea rasilimali na mambo mengine bila kujali umasikini wetu. Ilikuwa ni sahihi na mapambano hayajaisha. Unaposema wakubali yaishe tusonge mbele, twende wapi? Ndugu yangu njia sio safi na ina miba lazima isafishwe kwanza!
 
Pasco, unakubali kuwa kwa kutumia kanuni ya 86:3b Lissu angepewa nafasi ya kuelezea sababu za kwanini mswada ule ukataliwe na Spika angempa nafasi hiyo?
Argument ya Pasco ni kwamba hatuwezi kujuwa unless angefanya hivyo.

Sasa sijui kwanini hataki ku accept past experience one of the factor.

Ni kweli ana argument,na mjadala huu utawaacha watu kwenye mawazo waliokuwa nayo awali kila mmoja kwa upande wake anavyoona ie CDM was wrong vs whthere they were right, unless kama kuna hayo ya nguvu ya umma ku take place.
 

Mkuu, nimefuatilia huu uzi pamoja na posts za wadau; mdau mmoja kwa jina la FJM alisema kwamba kutokana na mwenendo wa bunge hili chini ya Makinda, CHADEMA wameshawahi kupinga baadhi ya mambo hapo bungeni, lakini kutokana na wingi wa wabunge wa upande mwingine, siku zote hawakufanikiwa. Sasa kwanini katika hilo la muswada wa marekebisho ya katiba wapinge wakati hawajawahi kufanikiwa katika kupinga?

Pia Mzee Mwanakijiji, aliweka hadi hiyo kanuni ya 86 unayoizungumzia; nayo ametoa maelezo ya kutosha ya kwamba kupinga tu hakutoshi, bali kunakamilika kwa spika kuhoji bunge zima kama linaafiki upingaji huo! Hapa tunarudi kwenye historia iliyotolewa na FJM; mambo yangekua yale yale. Wakati mwingine assumptions uwa hazikwepi. Katika hilo assumptions hazikwepi pia; kwani hata theories zote uzijuazo zimetengenezwa kwa assumptions!

Sitaki kuamini kwamba wewe ulitaka CHADEMA wapinge tu kwa kufuata protocol za upingaji ilihali wenyewe walielewa fika kwamba upingaji wao husingekua na manufaa yoyote kutokana na aina ya bunge lililopo!

Pia suala la kukihoji CHADEMA juu ya muswada huo halijakaa vyema; wadau humu wamekuuliza ya kwamba, kwani huo muswada ni mali ya CHADEMA?

Wewe kama mpenda mabadiliko/mageuzi (or whatever you may name it) unahisi hili suala lilistahili kupingwa? Kama ndio hakuna taratibu ambazo zinakuruhusu wewe kama mpenda mabadiliko/mageuzi kwenda kufungua kesi mahakamani ili kupinga? Maana hapa unavyojionyesha ni as if CHADEMA has to be blamed for this!!

Naomba majibu!
 
Pasco,
Mkuu wangu nadhani ku face reality ndio muhimu zaidi inapotokea hoja kama hii. Mimi nadhani Chadema wamefanikiwa sana kuonyesha vitu kabla hata havitatokea ni kama vile utabiri wao umejionyesha wazi pale CCM na NCCR walopotoka kisha CCM wakaupitisha muswada bila pingamizi. Kwa hali yoyote ile muswada huu ungepita na yaonyesha wazi Spika asingesimama na CDM/ NCCR bila support kutoka upande wa CCM hata baada ya wao kuondoka bungeni hapakuwa na pingamizi..

Kuuputisha muswada bila pingamizi toka upande wa pili kumeonyesha wazi kwamba mawazo nje ya yale ya wanaCCM hayawezi kupewa nafasi na mfumo wetu ni wengi wape usisahau hilo...Na binafsi yangu, sio tu tunahitaji katiba mpya bali ku re define - Articals of Union ambazo zinawapa baraza la Mapinduzi nguvu kubwa ya ku oversee maswala yote yasiyoihusiana na Muungano kuhusu Zanzibar. Maadam sasa tuna mfumo wa vyama vingi sidhani kama ni haki Baraza la Mapinduzi ambalo wajumbe wake wote ni wanachama wa ASP ambacho leo ni CCM na hawa ndio walokuwa sababu kubwa ya Salim. A. Salim kuondolewa haki yake ya kugombea Urais.
 
Hii issue ni sawa na mtu ambaye anataka kufa lakini dawa ya kumwokoa iko kwenye himaya ya simba wenye njaa...

Je mtu huyo asubiri afe kwasababu anajuwa kwamba akienda kwenye himaya ya Simba wakali wenye njaa hawatamwacha na hivyo matokeo kuwa yale yale yani kifo?

Ni uamuzi unaoweza kuchukuliwa kwa utofauti na watu wa tofauti.

Ndo jinsi hii issue ilivyokaa.
 
Mkuu Mkandara,

Naona Pasco anapingana zaidi na Lissu kuhusiana na maadili ya kisheria kama nimwelewa, kwamba the process should have been exhausted.

Sasa sijui kama ni right kumu hold to those standards given the fact kuwa sidhani kama procedure ilikuwa ya kisheria ama ni taratibu za bunge.

Ama kama taratibu za bunge ie kwenye issue ya muswada hii zina angukia kwenye "sheria"

Nadhani mwishowe tutaelewana tu.
 

Ngongo,
Kwanza nataka kukukumbusha kwamba sio tu mimi ni mpenzi wa chadema, bali mimi ni mwanachama hai na ni Kiongozi ngazi ya Jimbo.
Wala usijidanganye bure ndugu yangu, mimi siburuzwi hata siku moja. Katika hili la muswada wa katiba mpya ninawaunga mkono viongozi wangu mia kwa mia. Siwaungi mkono kwa sababu tu ni viongozi wangu/wabunge wa chama changu, bali ni kwakuwa nimejitahidi kuusoma muswada pamoja na kufuatilia kwa karibu hoja mbalimbali zinazotolewa na makundi mbalimbali ya watanzania, kuanzia kwa wanaharakati, majaji wastaafu na hata wazee wastaafu wa ccm na serikali. Wote hao wamekuwa na mtazamo sawa na wa chadema, sasa usije ukaniambia kwamba jukwaa la katiba, majaji wastaafu na wazee wastaafu wa ccm na serikali nao wanaburuzwa na hoja dhaifu.
Hoja hii ukiita dhaifu, bila shaka wewe ndiye utakuwa dhaifu kwakuwa utakuwa umeshindwa kuona uzito wa hoja ambao umemlazimu mwenyekiti wa ccm taifa kuizungumzia kwa marefu na mapana yake katika kujitetea, sasa hapo wewe unaiona ni hoja dhaifu? utakuwa na matatizo ya kupima hoja mkuu si bure.

Sijamfunga mdomo mtu yeyote anayewahoji viongozi wangu/wabunge wangu, bali ninahoji hoja yake kama anavyohoji wabunge wangu. TL alitoa hoja bungeni kwa mujibu wa kifungu hicho anachokitaja lakini spika hakumuelewa. Kama tutakubaliana kwamba Mnyika na Machali hawakutoa taarifa mapema kwa spika ili watoe hoja yake lakini nitakukumbusha kwamba kwenye hotuba ya Lisu alitoa hoja ya kusitisha huo mjadala wa muswada kwa kifungu hicho lakini spika akapindisha makusudi ili kuinusuru serikali kwa kuwa wlaishakuwa na kikao chao mapema na kukubaliana kuendelea hivyo hivyo bila kusikiliza wadau wengine.
 
......
  • pia tuwe na tahadhari kwani, kuna theories zingine huwa zinashindwa kufanya kazi kwenye practical ....
  • na wakati mwingine sound logic huwa zinakuwa zaidi ya moja ...
Hivyo Pasco anaweza kuwa right ama wrong pia. Lakini possibility ya Pasco kuwa wright inakuwa affected na determination ya CCM waliyoonesha ndani ya Bunge. Hivyo Mwanakijiji anaonekana kuwa na possibility kubwa ya kuwa sahihi zaidi.

Mimi ni mwana CCM lakini nina simanzi kubwa na kinachoendelea katika nchi na ndani ya CCM. Natamani katiba ijadiliwe kwa uwazi na muungano pia. Lazima tukubali kuwa sasa ya mabadiliko imefika na itakuwa vigumu sana kuyasimamisha (to stop the wind of change is rather impossible..). Si Libya tu, mabadiliko yametikisa hadi Ulaya na Asia, na mwangwi wake umefika hadi Amerika. Sisi wa-Tz na Kikwete wetu hatuwezi kushindana na upepo huo, haiitawezekana.

Mimi naamini kabisa kuwa, tukikaa chini na kujadiliana ni amani, na tukifanya siasa na kushindana kwa haki na kubadilishana katika uongozi kwa taratibu zetu, itakuwa amani zaidi. Tatizo ni ubinafsi na hofu ya watawala kuumbuliwa madhambi yao ya ufisadi... Hicho ndiyo kitaangamiza Tanzania na Tanganyika yake...
 
Sawa lakini nachojua mimi inategemea TL ameyazungumza haya katika hatua gani ya bunge..Kama nilimwelewa vizuri JK ktk hotuba yake inaonyesha wazi CDM na NCCR wamepinga muswada huu ktk hatua za mwanzo kabisa za kanuni ya 70 kujia 72... sasa huwezi mtu kuzungumzia kanuni ya 86 nje ya kamati ya bunge wakati muswada umekwamishwa ktk hatua ya 70 kwa kutumia vifungu vya kanuni ya 71...
 
"Kwa sababu hizi zote, Mheshimiwa Spika,naomba kutoa hoja chini ya kanuni ya 86(3)(b) ya Kanuni za Kudumu za Bunge hili tukufu kwamba Bunge hili likatae Muswada huu Kusomwa Mara ya Pili kwa sababu Serikali imeleta Muswada Mpya na wenye mabadiliko makubwa na ya msingi bila kufuata masharti ya kanuni ya 84(3) ya Kanuni za Kudumu za Bunge; na pia kwa sababu Serikali haijatekeleza maagizo ya Bunge hili tukufu kuhusu kutoa muda zaidi kwa Kamati na wananchi kuufikiria, kuuelewa na kuutolea maoni Muswada huu kinyume na matakwa ya ibara ya 18(a) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano juu ya uhuru wa wananchi kutoa maoni yao; ibara ya 21(1) na (2) juu ya haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wan chi, na haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayowahusu wananchi, maisha yao au yanayolihusu Taifa".


Hayo ni maneno yaliyomo kweye hotuba ya kambi ya upinzani (Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria). Sasa sielewi Pasco anachokitaka.

Nakumbuka baada ya kumaliza kuongea Tundu Lissu alisema "Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha". Nilivyomuelewa na kumsikia Spika siku ile ni kwamba Tundu Lissu alipaswa kusema "Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja" ili suala ilo liweze kuhojiwa; lakini kwavile alikosea ndio maana Spika alikataa.

Lakini ukweli unabaki kwamba, licha ya Lissu kukosea, Spika angekua yupo pale kwa maslahi ya taifa (angekua hasie wa kuegemea upande wowote) angeweza kumpa nafasi Lissu ya kusema kwa usahihi; lakini kwavile nia yake ni kukomoa upinzani hakufanya hivyo. Mara ngapi tumeona mawaziri na hata wenyeviti wa kamati wanakosea katika namna ya kumalizia hotuba zao, lakini spika anawasahihisha na kuwapa nafasi ya kusema kwa usahihi?

Hivyo ndugu Pasco, labda kama una dhumuni jingine, lakini katika hili sidhani kama utakua na substance ​tena.
 
pasco, move ya chadema ilikuwa ni anticipation of the inevitable.
anticipation signifies brilliance and maturity in a person.
 
Mkuu wangu shukuran sana..Ndio uzuri wa JF ni darasa wakati wote..Kwa hiyo, nimejifunza kuwa mbunge anaweza tumia kifungu cha 86 (3) baada ya muswada kutoka kamati ya bunge na kuwasilishwa...
 

Pasco,

Unapokuwa unasoma sheria ama kanuni usiishie kuitazama katika makaratasi tu, ni muhimu sana kuitazama practically na usisahau katika huu uwanja wa siasa za ushindani wa vyama vingi ni muhimu sana kukumbuka historia. Wanabodi wengi wamegusia hili, kwamba ni chadema wametazama nyuma wakaona historia inasema kwamba ccm wamekuwa wakitumia wingi wao vibaya bungeni kupitisha sheria zisizokuwa na manufaa ama maslahi kwa umma wa watanzania.

Wewe unaweza kuja hapa ukasema kwa kususa chadema wamepata nini, lakini ukumbuke kwamba si suala la chadema kupata nini at first hand, bali wananchi wa Tanzania wamejifunza nini na wananufaikaje na huo utaratibu wa msuso wa chadema. Tangu chadema waje na hizi strategy kali na mpya kabisa katika siasa za Tanzania, kila mara baadhi ya watu wamekuwa wakisema chadema imekosea na kuwatabiria wananchi kuwatupa mkono, na wewe ni mmoja wao. Lakini ukweli ni kwamba tumekuwa tukishuhudia ushawishi wa chadema ukiongezeka kila kukicha. Sasahivi huku mtaani(nilipo mimi) agenda imekuwa ni katiba mpya, kila mtu anazungumza katiba mpya. Kwahiyo utaona kuna athari za moja kwa moja wazopata wananchi kutokana na matendo ya chadema.

Wananchi sasahivi wanapata fursa ya kuelimishwa na kujielimisha mapungufu ya muswada uliopitishwa ili kutaka kujua sababu ya chadema kuususia. Kama wangeendelea kuujadili, sasahivi tungekuwa tunaongea habari ya jairo na luhanjo lakini svyo, habari sasahivi kila kona ya nchi ni katiba mpya!!
 

Ahsante sana Nyanda kwa kipande hiki cha hotuba ya mh. Tundu Lisu. Bila shaka hakuna ubishi kwamba msemaji wa kambi ya upinzani alikitumia vizuri kifungu hicho isipokuwa spika ndiye alishindwa kutimiza wajibu wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…