Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Dada yangu Faiza Fox, wewe kama mama wa familia una majukumu yako kwa mumeo, familia, na jamii. Katika kutimiza majukumu hayo, unadhani unafanya favour?. Mfano kumvisha mwanao, kumsomesha etc, au kumpikia mumeo na kumpa vile 'vyakula' vyote is it favour?.

Hayo yote JK aliyoyafanya ni within majukumu yake, anatimiza wajibu wake, tumpongeze rais wetu kutimiza wajibu wake?.
Nakushauri anzisha thread ya " MEMA YA JK', au "MAZURI YA JK", tutachangia!.Humu tunajadili jinsi watu tuliowategemea kuupinga ule muswada, walivyoshindwa kuwasilisha pingamizi ambalo mimi naona ni kosa, na sio kujadili mazuri ya JK.

Wiki ijayo, atausaini huu muswada kwa mbwembwe zote, tumpongexze pia kwa kusaini maana atakuwa amewafanyia watanzani favour kubwa kuwaanzishia safari ya kuelekea katiba mpya!.

Kufanya jema si kufanya favour. Favour ni kitu kingine kabisa havihusiani na wema, umenena vyema kasoro:

Hapo nilipokuwekea nyekundu, kumbuka mimi ni Mwanamke wa Kiislaam, nna wajib wangu kwa mume wangu, watoto, jamii na kadhalika, hilo la kumpikia mume wangu si katika majukumu yangu, Waislaam wanaume hufundishwa "kumlisha na kumvisha mkeo", sasa tazama hiyo kauli halafu uniambie. Kupika ili anilishe ni jukumu lake kama hawezi kupika aniwekee mpishi, ikiwa mimi ntaingia kumpikia na kumlisha basi mawili, amma nnamfanyia "favour" kwa kupenda kwangu amma nipatane nae awe ananilipa ujira wa kazi yangu hiyo ya kumpikia.

Wengi wana dhanna kuwa kupika na kumfulia mume ni kazi za mwanamke, la hasha si wa Kiislaam, wafanyao hufanya kimila zilizo nje ya Uislaam amma hufanya kama "favour" si jukumu lao hata kidogo. Saa ngapi nijipambe kwa ma oud (udi) na ma liwa, saa ngapi nipike saa ngapi nifuwe saa ngapi nioshe vyombo? khaaa! hata hiyo mikono si itakuwa kama fundi mekanika halafu nije kumshikashika mume wangu si ntamchubuwa? Unanchekesha, mke nyumbani ni pambo babu na si "house girl".

Kuhusu hili la Kikwete hata kama ni majukumu yake basi bado ni jema, kwani hao wa mwanzo hawakuwa na jukumu hilo? mbona walikuwa wanatuwacha twende Kenya kwanza kabla ya kufika Mwanza. Hilo ni moja kati ya Mema ya Kikwete wala halina ubishi.
 
Duh nawakubali CDM wanakaba mpaka penalty ahaaa aaaa.

Sio suala la kukaba hadi penalty; kama mtoa mada ameshakiri kwamba wabunge CHADEMA hawakufanya kosa peke yao, bali wabunge wote walikosea katika kuupitisha huo muswada bila kuupinga, ni halali na haki kichwa cha uzi kibadilishwe ili uzi huu ubaki kama uwanja wa kuelimishana na kushauri namna ya kusonga mbele!!
 
Natanguliza samahani kwako Pasco kwa kujibu hoja isiyohusika, kwani nikiiacha nitakuwa sijamtendea haki huyu mnazi wa JK.

Naona umekurupuka tu hapa ili umsifie JK kwa kitu ambacho hakijafanyika.

Kwa taarifa ya waziri wa ujenzi Dr. John Magufuli, ya wiki iliyopita, hadi sasa barabara zilizojengwa kwa kiwango cha lami ni kiasi cha kilometa 5000 na ili kufikia lengo la kuwa na barabara za lami zenye urefu wa 10,000 km wamesaini mikataba na wakandarasi mbalimbali ambao wengi wao wako kwenye hatua za mobilization. Kwahiyo usitake kudanganya watu hapa kwa sababu ya mahaba yako ya kidini juu ya JK.

Nikukumbushe pia kwamba hata hizo 5,000 km zilizofikiwa sasahivi ni miradi iliyoanzishwa na BWM na ikaja kukamilishwa wakati JK yuko madarakani. Kama unataka kumsifia JK kwa kujenga barabara, zungumzia zile tu zilizoanza kujengwa chini ya utawala wake, kwa maana ya miradi mipya ambayo imeanza kutekelezwa kuanzia bajeti ya 2006/2007!! Na baada ya kuifahamu hiyo miradi aliyoianzisha ambayo ndio wajibu wake mkuu kwa serikali kutoa huduma kwa wananchi wake, na hiyo haihitaji kusifiwa unless amefanya kitu extra hapo ndipo atahitaji kusifiwa. Kama alivyosifiwa kwa kuanza kujenga barabara ya chalinze segera kabla bajeti haijapitishwa, na baada ya selelii kuikalia kooni serikali wakatafuta uongo wa kujustify hayo matumizi. Kitu kingine tunachosubiri kumsifia ni kujenga bandari kubwa pamoja na uwanja wa ndege wa kimataifa bagamoyo!!

Wewe kweli u mzito kuelewa kwa hiyo na hizo 5000 zingine zikisha zitakuwa zaidi ya KM 14,000 ahsante kwa kunirekebisha, hapo umeniongezea hesabu yangu.

Hata hizo 5000 uzisemazo wewe kwa miaka 6 bado ni nyingi kuliko marais wote wa kabla yake pamoja na mkoloni. Upo hapo ulipo?
 
Wewe kweli u mzito kuelewa kwa hiyo na hizo 5000 zingine zikisha zitakuwa zaidi ya KM 14,000 ahsante kwa kunirekebisha, hapo umeniongezea hesabu yangu.

Hata hizo 5000 uzisemazo wewe kwa miaka 6 bado ni nyingi kuliko marais wote wa kabla yake pamoja na mkoloni. Upo hapo ulipo?

Kuna mawili, aidha hukusoma ama hujui kabisa hesabu ama la ulisoma na ukapata zero.

Kama tuna barabara za lami zinazofikia urefu wa km 5,000 na kuna wakandarasi wanajiandaa kuanza ujenzi ili tufikishe barabara zenye urefu wa km 10,000 hapo ni kusema takribani barabara za urefu wa km 5,000 ndio ziko kwenye maandalizi ya kujengwa, sasa sijui hiyo km 14, 000 umeitoa wapi!

Nimesema kwa mujibu wa waziri magufuli, hadi sasa tuna barabara za lami zinazofikia km 5,000. Hapo kwenye km 5,000 unazungumzia barabara zote alizojenga Nyerere, Mwinyi, Mkapa na alizomalizia Kikwete kutoka kwa mkapa. Na ni ukweli uliodhahiri kwamba Mkapa ndiye kajenga barabara nyingi za lami unazomsifia kikwete. Kama unataka kumsifia kikwte kwamba ndiye kajenga, subiri 2015 atakapokuwa ameondoka madarakani, na kama hizo ambazo ziko kwenye mobilization stage zitakuwa zimekamilika, kwakuwa tumewazoea mnapeleka wakandarasi site bila kuwalipa kwa ajili ya kujitafutia sifa za kijinga na umaarufu wa bei chee, lakini mwisho wa siku wanaishia kuondoka na barabara kubaki na mahandaki kama kawaida.

Narudia kusema kwenye barabara kikwete hawezi kuchukua credit yoyote hadi hapo atakapokamilisha miradi aliyoianzisha mwenyewe! wala usimtafutie kusifiwa kwa kazi nzuri ya Ben Mkapa.
 
Hayo yote hayahitaji kusifiwa mkuu kwavile ndio majukumu ya serikali na ilipoomba kura, iliahidi kutekeleza hayo majukumu. Mimi sioni kipi cha kusifia wakati inatekeleza/itakua inatekeleza majukumu yake iliyopewa na wananchi.

Mkuu naomba nikukumbushe kwamba miaka mingi yu iliyopita, serikali ilikuwa imependekeza na kuamuliwa ujengwe uwanja mpya wa kimataifa huko mkuranga na kulikuwa na mpango wa kuiboresha bandari ya mtwara na Tanga ili ziweze kukidhi mahitaji ya mizigo inayoingia na kutoka nchini.

Lakini all over sudden baada ya JK kuingia madarakani serikali imeanza kubadili mawazo na kutaka kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa bagamoyo badala ya mkuranga. Serikali hiyo hiyo imeanza kupanga kujenga bandari kubwa na ya kisasa bagamoyo na kuziacha bandari za tanga na mtwara.

Hapo sasa mimi ndo nikasema asubiri tumsifu kwa hilo! nadhani anataka kuigeuza bagamoyo kuwa kama yamousokrou ya ivory coast, nadhani hadi hapo utakuwa umenisoma.
 
Mkuu naomba nikukumbushe kwamba miaka mingi yu iliyopita, serikali ilikuwa imependekeza na kuamuliwa ujengwe uwanja mpya wa kimataifa huko mkuranga na kulikuwa na mpango wa kuiboresha bandari ya mtwara na Tanga ili ziweze kukidhi mahitaji ya mizigo inayoingia na kutoka nchini.

Lakini all over sudden baada ya JK kuingia madarakani serikali imeanza kubadili mawazo na kutaka kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa bagamoyo badala ya mkuranga. Serikali hiyo hiyo imeanza kupanga kujenga bandari kubwa na ya kisasa bagamoyo na kuziacha bandari za tanga na mtwara.

Hapo sasa mimi ndo nikasema asubiri tumsifu kwa hilo! nadhani anataka kuigeuza bagamoyo kuwa kama yamousokrou ya ivory coast, nadhani hadi hapo utakuwa umenisoma.

Hakika kwa hili atahitaji kupewa sifa maana he will accomplish the extraordinary!! Nimekusoma kamanda.
 
Ila Pasco wewe ni kiboko. All in all sijatoka mtupu hapa kuna elimu kubwa sana nimeipata hapa nadhani wengi watakiri hivyo.
 
Pasco,

..nadhani waliopaswa kusimamisha mswada wa katiba ndani ya bunge kupitia kifungu ulichokitaja ni wabunge wa CCM na siyo Chadema.

..nasema hivyo kwasababu CCM ndiyo wenye wabunge wengi mle bungeni na wanachoamua wao ndicho kinachopita.

..mabadiliko kupitia bunge la nchi hii kwa kweli yanategemea zaidi CCM kuliko chama chochote kile kinachowakilishwa ktk bunge la jamhuri.

..bila CCM kutanguliza maslahi ya taifa ndani ya bunge basi kwa kweli wananchi tuandike maumivu tu.

..mtawapigia kelele CDM lakini kwa mtizamo wangu they did what they could ktk mazingira magumu sana.
 
JokaKuu,

Nadhani waliopaswa kusimamisha mswada wa katiba ni wabunge toka chama chochote ambao walibaini kasoro za mswada.



Pasco,

..nadhani waliopaswa kusimamisha mswada wa katiba ndani ya bunge kupitia kifungu ulichokitaja ni wabunge wa CCM na siyo Chadema.

..nasema hivyo kwasababu CCM ndiyo wenye wabunge wengi mle bungeni na wanachoamua wao ndicho kinachopita.

..mabadiliko kupitia bunge la nchi hii kwa kweli yanategemea zaidi CCM kuliko chama chochote kile kinachowakilishwa ktk bunge la jamhuri.

..bila CCM kutanguliza maslahi ya taifa ndani ya bunge basi kwa kweli wananchi tuandike maumivu tu.

..mtawapigia kelele CDM lakini kwa mtizamo wangu they did what they could ktk mazingira magumu sana.
 
Faiza Fox asante kunisaidia kuelimisha hili, Mhe. Tundu hakutoa pingamizi, alitoa maoni. Ukitoa maoni bunge linasikiliza tuu, wanaweza kuamua kuyazingatia au kuyapuuza. Lakini kama angetoa pingamizi, spika hana mamlaka ya kuzuia, wala hana uamuzi asikilize au la, ni lazima asimamishe kila kitu, asikilize lile pingamizi na wabunge kulichangia na ndipo aliulize bunge kufikia uamuzi.

Naendelea kusisitiza kutowasilishwa pingamizi was a mistake, ila pia lazima niikubali hoja ya Mzee Mwanakijiji kuwa sio kosa la Chadema wala tuwatwishe huu mzingo wa lawama, kwa sababu kanuni ziko wazi, mbunge yoyote angeweza kuwasilisha pingamizi, sio lazima mpaka Lissu tuu au Chadema.
Mkuu sawa nimekuelewa vizuri sana lakini nachotaka kuelewa zaidi ni wakati gani PINGAMIZI hututolewa na mbunge? tuseme kuna mbunge wa CCM, NCCR, ama chama kingine ametaka kutoa PINGAMIZI utaratibu wake unakuaje?
 
Pasco,

Samahani narudi tena ingawa niliaga ila naona nimsaide hapa Mkandara kwani naona kaweka point moja muhimu sana na wewe umeijibu kisiasa zaidi.

Ulichojibu ni sawa na Mwanamke/Mwanaume aliyemuuwa mwenzi wake kwa sumu na alipopelekwa mahakamani, majibu yake yakawa kapa hapa chini.

Hakimu: Unashitakiwa kwa kumuuwa mpenzi wako kwa sumu uliyoweka kwenye chakula.
Mshitakiwa: Hapana hakimu, sikumuuwa mie. Wakati napika, moja ya VIUNGO nilivyotumia kwenye mbonga ilikuwa ni hiyo MERCURY. Na si hicho tu, niliweka pia DDT, pilipili, chumvi, binzari............

Hakimu anawaambia watu kuwa "Mshitakiwa hana makosa kwa sababu katika maelezo yake, tunaona wazi kabisa kuwa hakuwa na nia ya kumuuwa Mshitakiwa ila ametumia tu VIUNGO katika kumwandala chakula mke/mume wake."

Anakuja Pasco na kusema "huyu mama/baba, kama angelitumia neno SUMU, angelifungwa au hata kunyongwa ila kwa sababu alitumia neno KIUNGO, basi ni kweli HANA HATIA."

Kama kifungu 86 (3) b kinaelezea kuhusu KUSIMAMISHA MJADALA, basi ilibidi Hakimu/Spika asimamishe kikao. Alichokifanya Bibie ni kujifanya kasikia neno VIUNGO badala ya SUMU. Kamuachia mtuhumiwa huru na leo hapa tunajadili kwa nini Hakimu hakulitumia neno SUMU [kifungu 86 (3)b - Pingamizi] na badala yake akatumia neno VIUNGO [kifungu 86 (6) - Maoni] katika kuendesha kikao.

Mkuu Mkandara, mie nilikuelewa kama hapo juu.
Hapana mkuu wangu nimemwelewa vizuri Pasco... anachosema yeye ni kwamba mshtakiwa alitakiwa kusema maneno haya:- GUILTY ama NOT GUILTY kisha utaambiwa kaa chini na kesi itaahirishwa hadi baadaye mtakapo itwa tena, na sii kutoa maelezo ya kujitetea..

Hivyo, kulingana na utaratibu wa Bunge Mama Kilango alitakiwa kuisoma hotuba ya TL mapema na kukuta makosa yamefanyika hivyo kusema hili ni PINGAMIZI hivyo yachukuliwe maneno ya mwisho tu..Ndivyo ilivyo mahakamani mtu ukikosea na kuanza kujieleza wakati unatakiwa kusema guilty or not guilty jaji hutoa mwongozo. Hawezi kutoa hukumu kwa kufuata makosa ya kanuni wakati mtuhumiwa anatakiwa kukiri amekubaliana na amepinga..

Kwa maana hii Spika aliyaona makosa ya kanuni toka kambi ya Upinzani ktk kujibu wanakubaliana ama wanapinga lakini akayaachia yaingie bungeni kwake makusidi ili pingamizi litakapo somwa litaonekana ni maoni ya kambi ya Upinzani kisheria..na ndio maana alikataa kutoa hata mwongozo makusudi.
 
MMM,

Nilivyomwelewa Pasco,ni kwamba CHADEMA wame imiss opportunity ya kuusimamisha na kuuzuia usisomwe mara ya pili kwa kutumia kifungu cha 86.

Wewe kwa upande wakonaona unapinga kwa kusema lisingewezekana.

Kwangu mimi hapo ndipo penye msingi wa hoja.

Je nani mkweli,nasubiri kuona kama ni kweli kuna namna ambayo CDHADEMA wangeweza kuzuia kama alivyosema Pasco.

As far as I remember, baada ya Waziri wa Katiba na Sheria Kombani kuwasilisha muswada bungeni kwa mara ya pili, alisikika mbunge akiomba mwongozo wa Spika kuahirisha bunge. Spika hakutoa nafasi ya kusikiliza mwongozo unasema nini na akasema hakuna mwongozo. Kisha akamwita msemaji wa Kambi Rasmi ya Ushindani (siyo Upinzani) bungeni. Tundu Lissu akashusha nondo zake na alipomaliza wanabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi wakatoka nje. Sioni kama Chadema wali'miss' any opportunity bali walijua maoni yao hayatasikilizwa. After all, kwenye hotuba ya Kombani zile sehemu zote muhimu ambazo zilihitaji marekebisho ya msingi alisema: "Serikali haikukubaliana na marekibisho hayo na hivyo serikali imeona ibaki kama ilivyo." Kwa maneno mengine, kubaki kwa Chadema bungeni kusingesaidia chochote badala yake kungetumiwa na serikali kwamba wamepitisha muswada pamoja na ili ilionekane kuwa hawakuunga mkono huo ujanja wa CCM ilibidi wapenda mabadiliko watoe msimamo wao.
 
Inasikitisha sana ndugu yangu. Huko nyuma nimeuliza kuwa hawa 'waandishi mahiri' watatumia kalamu zao kuwaonyesha wananchi ubaya wa sheria hiyo au kile ambacho Chadema hawakufanya??!!
punainem-red, japo zamani niliwahi kuwa mwandishi wa habari, bahati mbaya sikuwahi kufikia kiwango cha 'mwandishi mahiri'.
Anayetembea akajikwaa na kuanguka, akiinuka na kuangalia pale alipoangukia, next time atajikwaa tena pale pale na alipojikwaa mwanzo.

Yule anayetembea na akajikwaa na kuanguka, anapoinuka na kutazama pale alipojikwaa na sio alipoangukia, huyo next time, hatajikwaa tena pale pale!.

Naamini kwa kuonyesha tuliowaaminia, wamejikwaa wapi, next time hawatajikwaa tena pale pale!
 
As far as I remember, baada ya Waziri wa Katiba na Sheria Kombani kuwasilisha muswada bungeni kwa mara ya pili, alisikika mbunge akiomba mwongozo wa Spika kuahirisha bunge. Spika hakutoa nafasi ya kusikiliza mwongozo unasema nini na akasema hakuna mwongozo. Kisha akamwita msemaji wa Kambi Rasmi ya Ushindani (siyo Upinzani) bungeni. Tundu Lissu akashusha nondo zake na alipomaliza wanabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi wakatoka nje. Sioni kama Chadema wali'miss' any opportunity bali walijua maoni yao hayatasikilizwa. After all, kwenye hotuba ya Kombani zile sehemu zote muhimu ambazo zilihitaji marekebisho ya msingi alisema: "Serikali haikukubaliana na marekibisho hayo na hivyo serikali imeona ibaki kama ilivyo." Kwa maneno mengine, kubaki kwa Chadema bungeni kusingesaidia chochote badala yake kungetumiwa na serikali kwamba wamepitisha muswada pamoja na ili ilionekane kuwa hawakuunga mkono huo ujanja wa CCM ilibidi wapenda mabadiliko watoe msimamo wao.
Mkuu hicho kipande nilicho ki highlight unaweza kuthibitisha mbunge huyo ni nani ama tunaweza kupata hotuba nzima ya bunge siku hiyo...
 
Pasco,

..nadhani waliopaswa kusimamisha mswada wa katiba ndani ya bunge kupitia kifungu ulichokitaja ni wabunge wa CCM na siyo Chadema.

..nasema hivyo kwasababu CCM ndiyo wenye wabunge wengi mle bungeni na wanachoamua wao ndicho kinachopita.

..mabadiliko kupitia bunge la nchi hii kwa kweli yanategemea zaidi CCM kuliko chama chochote kile kinachowakilishwa ktk bunge la jamhuri.

..bila CCM kutanguliza maslahi ya taifa ndani ya bunge basi kwa kweli wananchi tuandike maumivu tu.

..mtawapigia kelele CDM lakini kwa mtizamo wangu they did what they could ktk mazingira magumu sana.
Joka Kuu, hii ni kweli ndio maana nikaikubali hoja ya Mzee Mwanakijiji iliyofunga mjadala, na nikasema wazi, tuusiitwishe mzigo huu Chadema.
 
Ngongo said:
Nadhani waliopaswa kusimamisha mswada wa katiba ni wabunge toka chama chochote ambao

Ngongo,
..nakubaliana na wewe 100%...nilichomaanisha mimi ni kwamba CCM, kwa kuzingatia kwamba ndiyo wengi ktk bunge, had a better chance ya kufanikiwa kusitisha mswada huo kwa ku-invoke kifungu anachokitaja Pasco.

..tunawalaumu CDM bure, quite frankly they can only do so much ndani ya bunge lililosheheni wana CCM walioweka mbele maslahi binafsi na ya chama chao.

..binafsi nilipoona mswada mbovu kiasi kile umeshafika bungeni tayari niliandika "maumivu." there was no party other than CCM ambao wangeweza kuuzuia mswada ule usipite.

..lawama zangu nazielekeza kwa Raisi, Mwanasheria Mkuu, na Waziri wa Sheria, na wabunge wa CCM. hao ndiyo waliokuwa na UWEZO wa kutupatia mswada mzuri unaozingatia maslahi ya taifa.
 
Mkuu sawa nimekuelewa vizuri sana lakini nachotaka kuelewa zaidi ni wakati gani PINGAMIZI hututolewa na mbunge? tuseme kuna mbunge wa CCM, NCCR, ama chama kingine ametaka kutoa PINGAMIZI utaratibu wake unakuaje?
Naomba ipitie ile update 3 kwenye maandishi mekundu.

Baada ya hotuba ya mtoa hoja, serikali, mbunge yoyote atasimama na spika atakampa nafasi, atatangulia kusema yale maneno kwenye red. Spika atasimamisha kila kitu na kusikiliza hilo pingamizi na sababu za pingamizi hilo.
 
Hapana mkuu wangu nimemwelewa vizuri Pasco... anachosema yeye ni kwamba mshtakiwa alitakiwa kusema maneno haya:- GUILTY ama NOT GUILTY kisha utaambiwa kaa chini na kesi itaahirishwa hadi baadaye mtakapo itwa tena, na sii kutoa maelezo ya kujitetea..

Hivyo, kulingana na utaratibu wa Bunge Mama Kilango alitakiwa kuisoma hotuba ya TL mapema na kukuta makosa yamefanyika hivyo kusema hili ni PINGAMIZI hivyo yachukuliwe maneno ya mwisho tu..Ndivyo ilivyo mahakamani mtu ukikosea na kuanza kujieleza wakati unatakiwa kusema guilty or not guilty jaji hutoa mwongozo. Hawezi kutoa hukumu kwa kufuata makosa ya kanuni wakati mtuhumiwa anatakiwa kukiri amekubaliana na amepinga..

Kwa maana hii Spika aliyaona makosa ya kanuni toka kambi ya Upinzani ktk kujibu wanakubaliana ama wanapinga lakini akayaachia yaingie bungeni kwake makusidi ili pingamizi litakapo somwa litaonekana ni maoni ya kambi ya Upinzani kisheria..na ndio maana alikataa kutoa hata mwongozo makusudi.
Mkandala, hakukuwa na makosa kwenye hotuba ya TL, kwani yale ndio maoni ya kambi ya upinzani, tatizo, kwenye maoni hayo, ndio akaweka na kipengele cha pingamizi ambalo spika makinda, alilikataa. Enzi za Sitta, wangetengua kanuni, kile kipengele cha pingamizi kirudishwe kwenye pingamizi na lingesikilizwa, na Sitta ni miongoni wa wana CCM bold sana ambaye asingekubali upuuuzi upuuzi wowote wa serikali. Nakumbula alipobishana na Jaji Mkuu kuhusu ulegevu wa mahakama, na ile siku JK analihutubia lile bunge jingine, Sitta alimshutumu kuwa amezidi upole, pale alipowasamehe wezi wa EPA!.

Tumuombee Mama Makinda nae apate busara kama za Sulemani, vinginevyo, tumekwisha!.
 
As far as I remember, baada ya Waziri wa Katiba na Sheria Kombani kuwasilisha muswada bungeni kwa mara ya pili, alisikika mbunge akiomba mwongozo wa Spika kuahirisha bunge. Spika hakutoa nafasi ya kusikiliza mwongozo unasema nini na akasema hakuna mwongozo. Kisha akamwita msemaji wa Kambi Rasmi ya Ushindani (siyo Upinzani) bungeni. Tundu Lissu akashusha nondo zake na alipomaliza wanabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi wakatoka nje. Sioni kama Chadema wali'miss' any opportunity bali walijua maoni yao hayatasikilizwa. After all, kwenye hotuba ya Kombani zile sehemu zote muhimu ambazo zilihitaji marekebisho ya msingi alisema: "Serikali haikukubaliana na marekibisho hayo na hivyo serikali imeona ibaki kama ilivyo." Kwa maneno mengine, kubaki kwa Chadema bungeni kusingesaidia chochote badala yake kungetumiwa na serikali kwamba wamepitisha muswada pamoja na ili ilionekane kuwa hawakuunga mkono huo ujanja wa CCM ilibidi wapenda mabadiliko watoe msimamo wao.
Magobe T, hili la kushindwa kuchukua hatua kwa kuogopa defeat, kwangu ni udhaifu!, wangechukua hatua, washindwe na Watanzania katika umoja wetu tungesimama nao!.
 
Pasco said:
Joka Kuu, hii ni kweli ndio maana nikaikubali hoja ya Mzee Mwanakijiji iliyofunga mjadala, na nikasema wazi, tuusiitwishe mzigo huu Chadema.

Pasco,

..u have very good points.

..lakini nadhani huenda uliweka matumaini makubwa mno wa CDM, tena ktk mambo ambayo hawana uwezo nayo.

..hivi umejiuliza kwanini imefika mahali KANUNI ndiyo zitumike kuupinga mswada wa katiba na siyo HOJA zenye uzito?

..binafsi nadhani njia nzuri ya kuboresha mswada wowote ule ni kupitia HOJA na MAPENDEKEZO mbadala na siyo kanuni.

..kanuni can only buy u sometime, lakini at the end of the day, mswada unaboreshwa kupitia maoni, na zaidi unapitishwa kwa kura za wabunge.

NB:

..nasisitiza kwamba hoja zako ni nzuri ktk kutoa "somo" kuhusu masuala ya kanuni za bunge. wasiwasi wangu ni kwamba "somo" hili unalojaribu kutoa kwa CDM peke yao linaweza kutumika vibaya na kuwa upenyo wa kutokea kwa wale ambao hawakufanya kazi kwa maslahi ya taifa hili, yaani Raisi, Mwanasheria Mkuu,na Waziri wa Sheria.

..ukitaka kujua kwamba Raisi hana nia njema ni pale alipoamua kuwadanya wazee wa DSM, watu wazima wanaoweza kumzaa, kwamba CDM walisema wataandika katiba mpya ndani ya siku 100.
 
Back
Top Bottom