Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

FaizaFoxy, bila kujigeuza kuwa mfanyakazi wako naomba nikuhakikishie I know what I am talking about. Muswada wa kuruhusu wakuu wa wilaya/mikoa kusimamia nidhamu ya mahakama ilikuwa ni makosa. Huwezi kuruhusu mhimili mmoja kuingilia kazi za mhimili mwingine hili ni kinyume kabisa na dhana ya separation of powers. Na ndio ilikuwa chimbuka la Lissu kupingwa, Zitto akasaidi lakini mwisho wa siku Spika alihoji wabunge wengi wakasema ndio sheria ikapita.

Na Nyerere aliporuhusu wajumbe wa nyumba kumi waamuwe kesi za watu nani alithubutu kunyanyuwa hata mdomo?
 
Una uhakika kwamba barabara ya Mayamaya Dodoma ina urefu wa km 11,600?? bila shaka umeangalia ITV kwa makengeza, ama hujui jiografia ya nchi hii!



Ona huyu naye sijui kakurupushwa na nani, hapa sio uwanja wa ku-propagate udini wa gerezani, ebo!!

"Kilomita 11,600 wakati huu wa Kikwete Tanzania nzima"

Soma na hapo ulipoacha kupawekea rangi nyekundu, umezowea kuchakachuwa, hapa huwezi unaonekana ni wakuja tu.
 
Hivi ndio fikra zako kuwa Rais hatousaini? umepotea step.

Muswada hauna tatizo, hao wenzako wanatafyta umaarufu tu, hawana pakutokea walisha kosea sasa hawataki kuoneka mambumbumbu. Maana kuna usomi w mwanasheria fulani ulikuwa questioned sana. Huwezi kama mwanasheria kweli kweli ukatowa maoni ya upinzani kuhusu muswaada halafu wakati unaanza kujadiliwa ujidai huutaki unasusa, huo ni upunguani.

Hakuna umbumbu wowote, ukweli kwamba muswada was a big flaw na sababu ni waleta muswada yaani CCM kuogopa kufedheheka kama walivyofedheheka Zanzibar kwa muswada kuchanwa na pili ni madaraka yao ya siasa za uchakachuaji.

Woga mkubwa wa CCM katika katiba hii ni kuundwa kwa serikali tatu katika muungano au kuvunjika kwa muungano na pia katiba itayohakikisha chaguzi huru. Ukumbuke Kikwete alisema hatokubali muungano uvunjikie mikononi mwake na katiba mpya inamwogopesha sana kwa hilo. Tatizo njia anayochukua kuulinda muungano ni ya kuchakachua na kulazimisha na pia kuwarubuni viongozi wachache wa CUF na CCM Zanzibar kwa mfano Hamad ametumika sana. Lakini mwisho ya yote bila maridhiano ya kweli kero za muungano ndio zitakayovunja muungano.
 
"Kilomita 11,600 wakati huu wa Kikwete Tanzania nzima"

Soma na hapo ulipoacha kupawekea rangi nyekundu, umezowea kuchakachuwa, hapa huwezi unaonekana ni wakuja tu.

Fundi wa kuchakachua ni weye na ccm yako kwa ushirikiano na nec na wale jamaa zako wengine.

Tangu lini barabara ya mayamaya Dodoma ikawa na urefu wa km 11,600? hilo ndio swali la msingi, achilia mbali kwamba bado haijajengwa!! Na kwakuwa una uzoefu wa kuchakachua huko nyuma, unajaribu tena kuutumia huo ujanja wako hapa!

Kama huifahamu jiografia ya nchi yako ni bora ukae kimya kuliko kushupaza shingo, wenye akili zao timamu watakuona "shake well before use".
 
Na Nyerere aliporuhusu wajumbe wa nyumba kumi waamuwe kesi za watu nani alithubutu kunyanyuwa hata mdomo?

Wajumbe wa nyumba kumi walifanya hivyo katika mfumo usio rasmi kisheria na hata hii leo bado wanaendelea kufanya hivyo, katika kiwango cha mwanzo kabisa huko mitaani.

Sasa hii ya serikali ya ccm na kikwete kupitisha sheria ya kuwapa mamlaka makada wa chama kusimamia nidhamu ya mahakimu ndio kichekesho kikubwa na inaonyesha uwezo mdogo wa kutenganisha mipaka ya hii mihimili walionao baadhi ya makada wa ccm kama wewe.
 
Mkuu hicho kipande nilicho ki highlight unaweza kuthibitisha mbunge huyo ni nani ama tunaweza kupata hotuba nzima ya bunge siku hiyo...

Baada ya kuwa nimekutana na eyewitness ili ku'verify' nilichosema, alinieleza hivi:
1. Kabla ya Waziri wa Katiba na Sheria kusoma hotuba yake, Mnyika aliomba mwongozo wa Spika akitaka bunge liahirishe mjadala wa Muswada wa mchakato wa kupata maoni ya wananchi kuhusu utungani wa Katiba mpya.
2. Spika alipuuza mwongozo wa Mnyika na kumwita waziri asome hotuba yake.
3. Waziri Kombani alipomaliza, mbunge wa NCCR-Mageuzi Machali aliomba mwongozo wa Spika pia. Lakini Spika akapuuza na kumwita Mnajimu Mkuu wa Kambi ya Ushindani Tundu Lissu ili asome hotuba yake.
4. Baada ya Tundu Lissu kumaliza hotuba yake, Mnyika aliomba tena mwongozo wa Spika. Kama kawaida yake Spika akapuuza na kuruhusu wachangiaji waanze kuchangia.
5. Kwa kuona hilo, wabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi wakaona ni vizuri watoke nje kuliko kutumiwa ili waupitishe Muswada wenye utata.
 
Mkuu,

Wewe ni mtu pekee ambaye umeweza kufikiri na kuona upande wa pili wa maneno ya Pasco.

Narudia tena, ni mtu pekee. Nafikiri mjadala ungelibaki kuwa kati ya maneno yako VS maneno ya Pasco.

Hii habari yako ilifaa sana kuwa inajitegemea au niseme imekuja ikiwa imechelewa.

Yes, kuna uwezekano mkubwa sana kuwa kama wangeliweka pingamizi na kushindwa, basi wasingelipata pa kutokea na kila sehemu ambayo wangelienda, wangeliambiwa wao ndiyo wanataka kutumia mabavu kwa kulazimisha.

Sasa hivi wanatumia UMBUMBUMBU wa Spika kuonyesha jinsi ambavyo wananyanyaswa. Hii kitu inaweza hata siku moja ikamrudi Spika. Sijui kama Tundu Lisu/Marandu walikaa na kulipanga hili. Walimchokonoa Spika na akachukia na baada ya hapo, kaanza kufanya vitu bila kufuata kanuni. Mchezo umekwisha na wanashangilia ushindi, ingawa kusema ukweli hii ngoma bado kabisa ni mbichi. Yetu macho.

Jambo lingine ambalo Mushi lazima ulielewe ni kwamba kitendo cha Chadema kutoka nje ya ukumbi wa bunge kupinga mswaada kimeuathili sana mswaada mzima kwa maana the whole world is watching kwa kitendo chao walichokifanya.

Binafsi naamini kuwa endapo CDM wangekubali kupitia mlango wa 86 kama Pasco alivopendekeza hilo ndio lingekuwa kaburi lao maana CCM wangesema umeleta hoja yako ukasikilizwa na spika akaamuru kura hoja yako imeanguka na sasa unalazimisha hoja mara baada ya kushindwa kwenye kura.

Lakini kwa kitendo chao cha kukataa kushiriki kimewapa political cover ya kwenda kokote wanakotaka na huenda kama wangepitiakifungu hicho cha 86 na kushindwa huenda JK angekataa kukutana nao na angesema malalamiko yenu yalisikilizwa na spika kura zikapigwa mkashindwa kwao mnanipoteea muda.
 
Magobe T, hili la kushindwa kuchukua hatua kwa kuogopa defeat, kwangu ni udhaifu!, wangechukua hatua, washindwe na Watanzania katika umoja wetu tungesimama nao!.

1. Pasco, kutoka nje ya bunge kwa wabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi siyo defeat ilikuwa protest. Na walifanya hivyo kutokana na experience yao ya nyuma. Walisoma alama za nyakati kuanzia namna ya muswada wa manunuzi ulivyopitishwa jana yake. Wabunge kama Mnyika walijitahidi sana ili wasikubali kununua mitambo chakavu wakidai kama wakati wa sheria ya zamani ambayo ilikuwa hairuhusu mitambo chakavu, baadhi ya vigogo walinunua na je ikiwekwa kwenye sheria si ndiyo itakuwa worse? Baada ya kuona mapendekezo yao yametupiliwa mbali, walisema hata kama muswada utaruhusu manunuzi ya "mitambo chakavu" kama serikali ilivyotaka basi walau wa'define' nini maana ya 'emergency' na 'mitambo chakavu' na pia itolewe adhabu kali kwa wale wataobainika kuiingizia serikali hasara kubwa.

2. Lakini Attorney General alisimama mara kadhaa akidai hakuna haja ya kufanya hivyo na kusema wabunge wasipitishe sheria kwa jazba kama ilivyokwishafanyika wakati wa Awamu ya Kwanza kuhusu wahujumu uchumi. Hatimaye, sheria ile ilipitishwa bila kuweka definition ya 'emergency' maana AG alidai hiyo ibaki kwa waziri husika na ndiye atakayeona pia kama mitambo ile ni chakavu na inafaa kununuliwa au la.

3. Kwa hili la muswada wa mchakato wa kukusanya maoni ya Katiba mpya pia, hotuba ya waziri Kombani ilielezea baadhi ya mapendekezo ambayo serikali ilikubalina nayo na yale ambayo haikukubaliana nayo likiwemo la kusoma muswada kwa mara ya kwanza pia lilikuwa limekataliwa achilia mbali la kuwa na tume huru na kupunguza madaraka ya rais. Hata Jukwaa la Katiba na wanaharakati wa haki za binadamu, wanasheria na wasomi walisema muswada usisomwe kwa mara ya pili bali mara wa yakwaza na vile vifungu muhimu vifanyiwe marekebisho. Lakini baada ya kuona serikali ilikuwa imekataa na kwa experience ya muswada wa manunuzi ya "mitambo chakavu" ulivyopitishwa, isingewezekana kwa vifungu tajwa vifanyiwe marekebisho hna hasa kwa kuzingatia kuwa wabunge wa CCM na CUF wote waliona hivyo vifungu viko sawa tu. Kwa kuona hili, kama wabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi wangebaki ndani wangetumiwa tu kuupitishwa muswada ule bila marekebisho ya msingi na baadaya kama kungetoa malalamiko, wangeambiwa: "Si muswada ulipitishwa kidemokrasia bungeni"? Heri walivyofanya, maana inaonekana wazi kuwa walioupitisha walikuwa wa chama cha CCM na CUF na siyo Chadema na NCCR-Mageuzi kwa muswada wenyewe 'lacks political legitimacy'.
 
Mkuu,

Wewe ni mtu pekee ambaye umeweza kufikiri na kuona upande wa pili wa maneno ya Pasco.

Narudia tena, ni mtu pekee. Nafikiri mjadala ungelibaki kuwa kati ya maneno yako VS maneno ya Pasco.

Hii habari yako ilifaa sana kuwa inajitegemea au niseme imekuja ikiwa imechelewa.

Yes, kuna uwezekano mkubwa sana kuwa kama wangeliweka pingamizi na kushindwa, basi wasingelipata pa kutokea na kila sehemu ambayo wangelienda, wangeliambiwa wao ndiyo wanataka kutumia mabavu kwa kulazimisha.

Sasa hivi wanatumia UMBUMBUMBU wa Spika kuonyesha jinsi ambavyo wananyanyaswa. Hii kitu inaweza hata siku moja ikamrudi Spika. Sijui kama Tundu Lisu/Marandu walikaa na kulipanga hili. Walimchokonoa Spika na akachukia na baada ya hapo, kaanza kufanya vitu bila kufuata kanuni. Mchezo umekwisha na wanashangilia ushindi, ingawa kusema ukweli hii ngoma bado kabisa ni mbichi. Yetu macho.
Sasa mkuu wewe ndo umegeuka sheick yahya kabisa?

Una uhakika gani kwamba wasingepokelewa na JK kwasababu walilipinga bungeni?

Ama ni utabiri tu?

Mimi mwanzoni sikukubaliana na Pasco, ni baada ya kuona kikao na rais kwajili ya shughuli ile ile ambayo pasco aliuliza kwanini haikufanywa bungeni.

Kama tungekuwa tunazijuwa agenda za kikao,maybe ingemake a difference.
 
Sidhani kama watu humu mumekisoma hicho kifungu na kufikiria vizuri kabla hujajituma mbele ya halaiki au public na kutoa maoni yako kifugu cha 86 kipo subject na kura za wabunge wa jamhuri wa muungano ambao wanapaswa kupigia kura sasa hapa wanandoa lazima wangeshinda

LAPILI Lissu alishasema kuwa mswada ule usomwe kwa mara ya kwanza na sababu zake akatoa je? je hili kwa mtu mwenye akili huoni kuwa ni pingamizi ? RAI watanzania tujenge tabia ya kujisomea na kuachana na ushabiki usio na hoja
 
Baada ya kuwa nimekutana na eyewitness ili ku'verify' nilichosema, alinieleza hivi:
1. Kabla ya Waziri wa Katiba na Sheria kusoma hotuba yake, Mnyika aliomba mwongozo wa Spika akitaka bunge liahirishe mjadala wa Muswada wa mchakato wa kupata maoni ya wananchi kuhusu utungani wa Katiba mpya.
2. Spika alipuuza mwongozo wa Mnyika na kumwita waziri asome hotuba yake.
3. Waziri Kombani alipomaliza, mbunge wa NCCR-Mageuzi Machali aliomba mwongozo wa Spika pia. Lakini Spika akapuuza na kumwita Mnajimu Mkuu wa Kambi ya Ushindani Tundu Lissu ili asome hotuba yake.
4. Baada ya Tundu Lissu kumaliza hotuba yake, Mnyika aliomba tena mwongozo wa Spika. Kama kawaida yake Spika akapuuza na kuruhusu wachangiaji waanze kuchangia.
5. Kwa kuona hilo, wabunge wa Chadema na NCCR-Mageuzi wakaona ni vizuri watoke nje kuliko kutumiwa ili waupitishe Muswada wenye utata.
Hapa ndugu Pasco labda utusaidie maanake ushahidi huu unamweka Spika mahala pabaya zaidi kulingana na jinsi Pasco alivyotujuza huko nyuma..Maanake kila ulichoandika hapa kinaonyesha wazi juhudi za kuvunja majadiliano ya muswada huo yalifanyika kulingana na kanuni za bunge lakini Spika alipuuza..
 
Hapa ndugu Pasco labda utusaidie maanake ushahidi huu unamweka Spika mahala pabaya zaidi kulingana na jinsi Pasco alivyotujuza huko nyuma..Maanake kila ulichoandika hapa kinaonyesha wazi juhudi za kuvunja majadiliano ya muswada huo yalifanyika kulingana na kanuni za bunge lakini Spika alipuuza..
Mkuu Mkandara, Mjadala huu tumeshaufunga kilichobaki ni kuendelea tuu kuelimishana kuhusu kanuni.
1. Mijadala ya bunge inaendeshwa kwa kanuni.
2. Hoja zote rasmi zinawasilishwa kwanza kwa spika kwa maandishi ndipo zinakuja kusomwa. Hata yale maswali yalishawasilishwa kwanza ofisi ya spika kwa maandishi. Na yale majibu pia yako kwa maandishi.
3. Mbunge yoyote mwenye hoja, ataiwasilisha kwa spika kwa maandishi.
4. Mpaka ninapoandika hapa, hakuna hoja yoyote ya kuhusu pingamizi iliyowasilishwa kwa maandishi kwa spika!.
5. Kanuni ya 86 inamuamuru spika asipokee hoja yoyote swali lolote wala kutoa muongozo wowote isipokuwa 86.3. Hakuna pingamizi lolote lililowasilishwa hivyo alikuwa right kukataa kila aliyetaka kuzungumza.
6. Hotuba ya TL aliiwasilisha kwa mujibu wa 86.6 ambayo ni maoni ya kambi ya upinzani. Kwenye maoni hayo ndipo akaweka na pingamizi mumo kwa mumo.
7. Maoni ni maoni, na pingamizi ni pingamizi!. Kanuni inasema pingamizi ikiwasilishwa kwa mujibu wa 86.3, Bunge litasitisha mchakato, kusikiliza pingamizi na bunge kupiga kura kuhusu kupitisha pingamizi hilo au kutopitisha.
8. Kwa vile ofisi ya spika ilishapewa hotuba ya TL in advance, na ikaona kuwa imechanganya maoni na pingamizi, ingekuwa ni enzi za SS wangetengua kanuni na kusikiliza pingamizi lililowasilishwa kama sehemu ya maoni. Hapa lazima tumkumbuke yule mzee wa kasi na viwango, Speed & Standards, SS.
9. Kanuni inaelekeza baada ya TL kuwasilisha maoni, majadiliano huanza bila kupokea hoja nyingine yoyote, swali au muongozo wowote!.
10. Namalizia kwa msisitizo, HAKUNA PINGAMIZI LOLOTE, LILILO WASILISHWA NA YEYOTE KUUPINGA MUSWADA HUO!. Alichowasilisha TL ni maoni na sio pingamizi!.
 
Mkuu Mkandara, Mjadala huu tumeshaufunga kilichobaki ni kuendelea tuu kuelimishana kuhusu kanuni.
1. Mijadala ya bunge inaendeshwa kwa kanuni.
2. Hoja zote rasmi zinawasilishwa kwanza kwa spika kwa maandishi ndipo zinakuja kusomwa. Hata yale maswali yalishawasilishwa kwanza ofisi ya spika kwa maandishi. Na yale majibu pia yako kwa maandishi.
3. Mbunge yoyote mwenye hoja, ataiwasilisha kwa spika kwa maandishi.
4. Mpaka ninapoandika hapa, hakuna hoja yoyote ya kuhusu pingamizi iliyowasilishwa kwa maandishi kwa spika!.
5. Kanuni ya 86 inamuamuru spika asipokee hoja yoyote swali lolote wala kutoa muongozo wowote isipokuwa 86.3. Hakuna pingamizi lolote lililowasilishwa hivyo alikuwa right kukataa kila aliyetaka kuzungumza.
6. Hotuba ya TL aliiwasilisha kwa mujibu wa 86.6 ambayo ni maoni ya kambi ya upinzani. Kwenye maoni hayo ndipo akaweka na pingamizi mumo kwa mumo.
7. Maoni ni maoni, na pingamizi ni pingamizi!. Kanuni inasema pingamizi ikiwasilishwa kwa mujibu wa 86.3, Bunge litasitisha mchakato, kusikiliza pingamizi na bunge kupiga kura kuhusu kupitisha pingamizi hilo au kutopitisha.
8. Kwa vile ofisi ya spika ilishapewa hotuba ya TL in advance, na ikaona kuwa imechanganya maoni na pingamizi, ingekuwa ni enzi za SS wangetengua kanuni na kusikiliza pingamizi lililowasilishwa kama sehemu ya maoni. Hapa lazima tumkumbuke yule mzee wa kasi na viwango, Speed & Standards, SS.
9. Kanuni inaelekeza baada ya TL kuwasilisha maoni, majadiliano huanza bila kupokea hoja nyingine yoyote, swali au muongozo wowote!.
10. Namalizia kwa msisitizo, HAKUNA PINGAMIZI LOLOTE, LILILO WASILISHWA NA YEYOTE KUUPINGA MUSWADA HUO!. Alichowasilisha TL ni maoni na sio pingamizi!.
Mkuu naomba subira yako..mimi nataka kujiifunza achana hao wanaotaka kubishana tuu ili mradi kufurahisha baraza..Swala hili sio la CDM wala CCM sasa hivi lipo mikononi mwangu mimi kama raia na kujaribu kuelewa haswa hizi kanuni za bunge..

Pale namba tano (5) umemaanisha ili kutumia kanuni ya 86 (3)b ya kuahirisha majadiliano nayo mbunge hutakiwa hupeleka barua kwa Spika kwanza au mtu yeyote anaweza kusimama na kutoa hoja hiyo! - sielewi mkuu wangu.

Najua mara nyingi mpangilio wa wabunge kusimama na kuzungumza (HOJA) huwa imepangwa na hata atakayosema Spika huwa tayari anayajua.. Nachotaka kujua tu ktk kipande hiki Mjumbe anayetaka kuahirisha bunge pia huwa anatakiwa kupeleka barua yake na kama ndivyo wale baadhi ya wabunge huomba mwongozo kabla ama baada ya hotuba ya waziri huwa tayari wamewakilisha barua zao sio?.

Pili ni wakati gani mwongozo unaombea ktk pingamizi au niseme hoja. Yaani bunge linapofikia hatua gani? maanake kama nimekusoma vizuri TL na yaliyofuatia yote yalikuwa maoni kwa sababu ilikuwa ni wakati wa maoni na kifungu cha 86(6) cha kanuni za bunge ndicho kinachotumika..Je, ni wakati upi kifungu cha 86 (3) kinatumika na kwa utaratibu gani?.
 
Mkuu Mkandara, Mjadala huu tumeshaufunga kilichobaki ni kuendelea tuu kuelimishana kuhusu kanuni.
1. Mijadala ya bunge inaendeshwa kwa kanuni.
2. Hoja zote rasmi zinawasilishwa kwanza kwa spika kwa maandishi ndipo zinakuja kusomwa. Hata yale maswali yalishawasilishwa kwanza ofisi ya spika kwa maandishi. Na yale majibu pia yako kwa maandishi.
3. Mbunge yoyote mwenye hoja, ataiwasilisha kwa spika kwa maandishi.
4. Mpaka ninapoandika hapa, hakuna hoja yoyote ya kuhusu pingamizi iliyowasilishwa kwa maandishi kwa spika!.
5. Kanuni ya 86 inamuamuru spika asipokee hoja yoyote swali lolote wala kutoa muongozo wowote isipokuwa 86.3. Hakuna pingamizi lolote lililowasilishwa hivyo alikuwa right kukataa kila aliyetaka kuzungumza.
6. Hotuba ya TL aliiwasilisha kwa mujibu wa 86.6 ambayo ni maoni ya kambi ya upinzani. Kwenye maoni hayo ndipo akaweka na pingamizi mumo kwa mumo.
7. Maoni ni maoni, na pingamizi ni pingamizi!. Kanuni inasema pingamizi ikiwasilishwa kwa mujibu wa 86.3, Bunge litasitisha mchakato, kusikiliza pingamizi na bunge kupiga kura kuhusu kupitisha pingamizi hilo au kutopitisha.
8. Kwa vile ofisi ya spika ilishapewa hotuba ya TL in advance, na ikaona kuwa imechanganya maoni na pingamizi, ingekuwa ni enzi za SS wangetengua kanuni na kusikiliza pingamizi lililowasilishwa kama sehemu ya maoni. Hapa lazima tumkumbuke yule mzee wa kasi na viwango, Speed & Standards, SS.
9. Kanuni inaelekeza baada ya TL kuwasilisha maoni, majadiliano huanza bila kupokea hoja nyingine yoyote, swali au muongozo wowote!.
10. Namalizia kwa msisitizo, HAKUNA PINGAMIZI LOLOTE, LILILO WASILISHWA NA YEYOTE KUUPINGA MUSWADA HUO!. Alichowasilisha TL ni maoni na sio pingamizi!.

Pasco, hivi kuna kanuni ya bunge inayoweza kukiuka ibara ya 18 ya Katiba? Afer all, kuna ibara kwenye Katiba inasema sheria yoyote inayopingana na Katiba inakuwa batili. Sasa kwa jambo kubwa kama la Katiba sidhani kama kanuni inayopingana na Katiba ina'prevail'.
 
Pasco,
Pale nilipoweka nyekundu (Unless) ni wakati gani na kwa utaratibu gani mtu akitaka kuyasema ya kifungu cha A au B...hutumika toka kanuni hii:-

(3) Haitakuwa halali katika hatua hii kuleta hoja ya kufanya
mabadiliko katika hoja isipokuwa tu kwamba:- ( Kanuni inatamka wazi kuweka zuio kwa spika kuruhusu hoja yoyote, hivyo alikuwa right kumzuia Mnyika, Kafulila au yoyote, unless otherwise hii inayofuatia,
(a) mabadiliko bila kutoa sababu yanaweza kutolewa
kwa kusema:
"Kwamba, Muswada huu usisomwe mara ya Pili
sasa na badala yake usomwe baada ya …..
kuanzia …..", na hapo muda ambao Muswada
huo unaokusudiwa kusomwa utatajwa.
Hapa ndipo ulipopotea Mkuu Mkandara, hapa hapano hoja kwangu kwa vile hili ni pingamizi tuu la kuomba bunge liusiupokee muswada husika siku hiyo na badala yake kuomba liupokee siku nyingine, kwa case yetu, this is immaterial.

(b) mabadiliko yenye kutoa sababu yanaweza
kutolewa kwa kusema:
"Kwamba, Bunge hili likatae Muswada huu
Kusomwa
Mara ya Pili kwa sababu zifuatazo …….", na hapo
sababu za kupinga Muswada Kusomwa Mara ya
Pili zitatajwa kwa ukamilifu.
 
Pasco, hivi kuna kanuni ya bunge inayoweza kukiuka ibara ya 18 ya Katiba? Afer all, kuna ibara kwenye Katiba inasema sheria yoyote inayopingana na Katiba inakuwa batili. Sasa kwa jambo kubwa kama la Katiba sidhani kama kanuni inayopingana na Katiba ina'prevail'.
Magobe, hili nalo neno!. Bunge ndilo linalotunga sheria, Mahakama ndiyo inayotafsiri sheria. Bunge lilitinga sheria ya kuzuia mgommbea binafsi. Mahakama ikatoa hukumu sheria hiyo inapingana na uhuru wa kwenye katiba. Serikali ikapeleka marekebisho ya katiba, ukiukwaji huo wa haki za msingi za binaadamu ukaingizwa rasmi kwenye Katiba, Mahakama Kuu ikaamuru kipengele hicho kiwe scraped off, Serikali ikakata rufaa kuwa Mahakama haina uwezo wa kuliamuru bunge!. Kanuni za bunge zinapingika mahakamani. Soma mwanzo wa hiyo 86.1,
 
Pasco,
Pale nilipoweka nyekundu (Unless) ni wakati gani na kwa utaratibu gani mtu akitaka kuyasema ya kifungu cha A au B...hutumika toka kanuni hii:-

(3) Haitakuwa halali katika hatua hii kuleta hoja ya kufanya
mabadiliko katika hoja isipokuwa tu kwamba:- ( Kanuni inatamka wazi kuweka zuio kwa spika kuruhusu hoja yoyote, hivyo alikuwa right kumzuia Mnyika, Kafulila au yoyote, unless otherwise hii inayofuatia,
(a) mabadiliko bila kutoa sababu yanaweza kutolewa
kwa kusema:
“Kwamba, Muswada huu usisomwe mara ya Pili
sasa na badala yake usomwe baada ya …..
kuanzia …..”, na hapo muda ambao Muswada
huo unaokusudiwa kusomwa utatajwa.
Hapa ndipo ulipopotea Mkuu Mkandara, hapa hapano hoja kwangu kwa vile hili ni pingamizi tuu la kuomba bunge liusiupokee muswada husika siku hiyo na badala yake kuomba liupokee siku nyingine, kwa case yetu, this is immaterial.

(b) mabadiliko yenye kutoa sababu yanaweza
kutolewa kwa kusema:
“Kwamba, Bunge hili likatae Muswada huu
Kusomwa
Mara ya Pili kwa sababu zifuatazo …….”, na hapo
sababu za kupinga Muswada Kusomwa Mara ya
Pili zitatajwa kwa ukamilifu.
Mkuu Mkandara, anayeleta hoja ya pingamizi, hupelekwa kwanza kwa spika kwa maandishi, hivyo hapo baada tuu ya hoja ya serikali, Mbunge atasimama na kutamka maneno yale, Spika atausimamisha mchakato na kusikiliza pingamizi. Kwa vile hakuna pingamizi lolote lililowasilishwa kwa spika, wote ambao spika aliwazuia, amewazua kwa mujibu wa kanuni 86.1.

Kuomba muongozo wa spika, hakuhitaji kibali cha maandishi, ni kusimama tuu na kutaja kanuni, kama yalivyo maswali ya nyongeza na majibu yake hayahitaji maandishi kabla sambamba na majadiliano ambayo yanahitaji kutuma jina kwa spika kuwa una nia ya kuchangia hoja.
 
Pasco, hivi kuna kanuni ya bunge inayoweza kukiuka ibara ya 18 ya Katiba? Afer all, kuna ibara kwenye Katiba inasema sheria yoyote inayopingana na Katiba inakuwa batili. Sasa kwa jambo kubwa kama la Katiba sidhani kama kanuni inayopingana na Katiba ina'prevail'.

Kweli kabisa hai-prevail...ila haijaandikwa! unafikiri common sense kama hii yako Makinda anayo?
 
Pasco, hivi kuna kanuni ya bunge inayoweza kukiuka ibara ya 18 ya Katiba? Afer all, kuna ibara kwenye Katiba inasema sheria yoyote inayopingana na Katiba inakuwa batili. Sasa kwa jambo kubwa kama la Katiba sidhani kama kanuni inayopingana na Katiba ina'prevail'.
Labda sijaelewa vizuri, kanuni za bunge ni sheria au si sheria? kama ni sheria, uhuru wa kutoa mawazo uko granted.... as long as hakuna ukiukwaji wa sheria zilizopo. Unaweza kutoa mawzo yako, ila usikuke sheria.
 
Pasco,

..tatizo ni kwamba CDM wana wabunge wachache mno.

..Lissu hata angewasilisha pingamizi bado wangeshindwa na nguvu ya wingi wa kura za CCM.

..nasema hivyo kwasababu sidhani kama hoja za kwenye hilo pingamizi zingekuwa tofauti na kile kilichokuwemo kwenye hotuba ya Lissu.

..Labda utuambie, kwanini unafikiri CCM na CUF ambao walipinga[ na matusi juu ]hoja zote za Lissu ktk hotuba yake, wangemuunga mkono ktk pingamizi.
 
Back
Top Bottom