Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,252
- 36,513
Baada ya tume ya Warioba kuileta rasimu ya Katiba mpya ijadiliwe, ni jambo lisilopingika kwamba Taifa linaelekea kugawanyika kutokana na hoja kubwa iliyozuka ya mfumo wa Muungano na serikali zake.
Ili nchi iweze kusonga mbele ktk nyanja zote ni budi iwe na TAASISI zilizo imara na si kuwa na viongozi imara. Taasisi zikiwa thabiti ni kwamba zitakuwa kwenye mstari mzuri wa kutumikia nchi kwani ni vigumu kupata viongozi imara wakati wote. Ili tuwe na viongozi thabiti ni budi wasimamiwe na taasisi zitakazoundwa na Katiba ili waweze kukidhi vigezo na matakwa ya nchi.
Nchi ikiwa na Mahakama imara, Bunge Imara, Jeshi Imara na Usimamizi imara wa uchumi tutaweza kuondoka kwenye mstari wa mataifa yanayoendelea na kujiunga na klabu za mataifa yanayojibeba kiuchumi.
Tatizo na unafiki wa wasomi wetu ni kujikomba kwa wanasiasa waliopo madarakani kwa minajili ya kujipatia ugali wa siku. Inawezekana hata Great Thinkers wengine wakawa wamenaswa na mfumo wa MAONI-SIASA ambao umefunika uwezekano wa Watanzania kupata Katiba mpya.
Mfumo wa Muungano umeteka nyara maoni ya Katiba mpya kiasi kwamba watu hawajadili tena maadili, usimamizi na mgawanyo wa rasilimali na hata muundo wa taasisi imara za nchi. Tumefika kwenye kupigana vikumbo kuhusu aina ya Muungano na idadi ya serikali. Tusidanganyike na hadaa za wanasiasa.
Ili nchi iweze kusonga mbele ktk nyanja zote ni budi iwe na TAASISI zilizo imara na si kuwa na viongozi imara. Taasisi zikiwa thabiti ni kwamba zitakuwa kwenye mstari mzuri wa kutumikia nchi kwani ni vigumu kupata viongozi imara wakati wote. Ili tuwe na viongozi thabiti ni budi wasimamiwe na taasisi zitakazoundwa na Katiba ili waweze kukidhi vigezo na matakwa ya nchi.
Nchi ikiwa na Mahakama imara, Bunge Imara, Jeshi Imara na Usimamizi imara wa uchumi tutaweza kuondoka kwenye mstari wa mataifa yanayoendelea na kujiunga na klabu za mataifa yanayojibeba kiuchumi.
Tatizo na unafiki wa wasomi wetu ni kujikomba kwa wanasiasa waliopo madarakani kwa minajili ya kujipatia ugali wa siku. Inawezekana hata Great Thinkers wengine wakawa wamenaswa na mfumo wa MAONI-SIASA ambao umefunika uwezekano wa Watanzania kupata Katiba mpya.
Mfumo wa Muungano umeteka nyara maoni ya Katiba mpya kiasi kwamba watu hawajadili tena maadili, usimamizi na mgawanyo wa rasilimali na hata muundo wa taasisi imara za nchi. Tumefika kwenye kupigana vikumbo kuhusu aina ya Muungano na idadi ya serikali. Tusidanganyike na hadaa za wanasiasa.