Katika Salaam za kukaribishamwaka mpya wa 2013, Rais wetu Mh. Jakaya Mrisho Kikwete alitoa taarifa yamaendeleo ya uundwaji wa Katiba Mpya. Katika maelezo yake alionyesha kuwaifikapo Novemba 2013 Bunge la Katiba litakaa kupitisha mapendekezo yatakayo kuwa yametolewa na Tume ya Katiba.
Rais pia alionyesha matumainikuwa April 2014, tutakuwa tayari na Katiba mpya ambayo itatumika katika uchaguzimkuu wa 2015. Mwenyekiti wa Tume ya Katiba pia alithibitisha maelezo haya na kwa muda fulani alisikika akisema kuwa Uchaguzi Mkuu ujao usipofanyika chini ya Katiba mpya tutakuwa na matatizo makubwa.
Swali la kujiuliza, je hata kama kweli April 2014 tutakuwa na Katiba mpya kutakuwa na muda wa kutosha kuandaa mifumo, taasisi n.k za kutekeleza/kusimamia uchanguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2015.
Kwa ratiba yake ya kawaida, Bungela Muungano litatakiwa kuvunjwa mwezi Agusti 2015 ili kuruhusu mchakato wa uchaguzi mkuu kufanyika. Hii inatoa muda wa takriban miezi 15 na vikao kama vinne hivi vya Bunge kuandaa na kupitisha miundo, sheria na taasisi za kutekeleza Katiba mpya.
Mapendekezo tunayoshuhudia ya Katiba mpya yanagusa mambo mengi ambayo kwa kila hali kutakuwa na mabadiliko ya muundo na mfumo wa utawala. Kwa mfano mapendekezo yanagusa muundo wa muungano. Ikiwa kutakuwana Serikali tatu, hii ina maana lazima tuwe na mchakato mwingine wa Katiba yaTanganyika. Ni vigumu kuona hili likifanyika katika muda utakaokuwa umebaki!
Hata kama tukibakiza mfumo waSerkali mbili – kitu ambacho sioni kama itakidhi mapendekezo ya pande zote zamuungano – bado kutakuwa na mabadiliko kwani wapendekezaji wa mfumo huu wanaweka masharti ambayo yatahitaji mchakato mwingine kutekelezwa. Tukichukua mfumo wa Serkali moja halikadhalika itahitaji mchakato.
Tukiacha ya muungano,mapendekezo mengine yanaonekana kujikita zaidi katika muundo wa utawala na taasisi zake. Kuna mapendekezo ya majimbo. Hili likikubaliwa litahitaji mchakato mwingine kuhainisha mipaka, kuweka sheria zitakaongoza mfumo huu n.k. Ni kwa vipi haya yatafanyika katika kipindi kitakachokuwa kimesalia kuweza kufanya uchaguzi mkuu ulio huru na haki, ni kitu cha kujiuliza.
Kwa vyovyote vile hata tusipochukua mfumo huu wa majimbo, ni lazima kutakuwa na mabadiliko ya muundo wautawala ambao utahitaji taasisi na mfumo mpya kusimikwa kabla ya uchaguzi. Vinginevyo tutakuwa hatujatengeneza Katiba mpya!
Suala lingine la muhimu naambalo linahusiana na uchaguzi ulio huru na haki, ni taasisi itakayosimamiauchaguzi. Itashangaza ikiwa Katiba mpya haitaleta mabadiliko makubwa katikaTume ya Uchaguzi ili siyo tu ionekane huru bali pia itende haki katikau simamizi wa chaguzi.
Kikubwa hapa ni kuwa Tume ya Uchaguzi mpya ni lazima iwe na muda wa kuthibitisha uwezo na u-huru wake katika majukumu itakayopewa ili kuwajengea watu imani hiyo. Ni vigumu kuona wataweza kufanya hili katika kipindi hicho kifupi kitakachokuwa kimebaki na ikiwa kutakuwa na chaguzi ndogo za kutosha kuwapa watu nafasi za kuitathimini.
Je kwa hayo na mengine yanayo husiana na mabadiliko yatakayo ambatana na Katiba Mpya, ni rahisi kujiaminisha kuwa uchaguzi mkuu wa 2015 utafanyika chini ya Katiba hiyo mpya? Auni vyema kuanza kujiandaa vinginevyo na kuacha mchakato wa Katiba Mpya uendelee bila kuhuwaisha ili tupate kilicho bora.
Rais pia alionyesha matumainikuwa April 2014, tutakuwa tayari na Katiba mpya ambayo itatumika katika uchaguzimkuu wa 2015. Mwenyekiti wa Tume ya Katiba pia alithibitisha maelezo haya na kwa muda fulani alisikika akisema kuwa Uchaguzi Mkuu ujao usipofanyika chini ya Katiba mpya tutakuwa na matatizo makubwa.
Swali la kujiuliza, je hata kama kweli April 2014 tutakuwa na Katiba mpya kutakuwa na muda wa kutosha kuandaa mifumo, taasisi n.k za kutekeleza/kusimamia uchanguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2015.
Kwa ratiba yake ya kawaida, Bungela Muungano litatakiwa kuvunjwa mwezi Agusti 2015 ili kuruhusu mchakato wa uchaguzi mkuu kufanyika. Hii inatoa muda wa takriban miezi 15 na vikao kama vinne hivi vya Bunge kuandaa na kupitisha miundo, sheria na taasisi za kutekeleza Katiba mpya.
Mapendekezo tunayoshuhudia ya Katiba mpya yanagusa mambo mengi ambayo kwa kila hali kutakuwa na mabadiliko ya muundo na mfumo wa utawala. Kwa mfano mapendekezo yanagusa muundo wa muungano. Ikiwa kutakuwana Serikali tatu, hii ina maana lazima tuwe na mchakato mwingine wa Katiba yaTanganyika. Ni vigumu kuona hili likifanyika katika muda utakaokuwa umebaki!
Hata kama tukibakiza mfumo waSerkali mbili – kitu ambacho sioni kama itakidhi mapendekezo ya pande zote zamuungano – bado kutakuwa na mabadiliko kwani wapendekezaji wa mfumo huu wanaweka masharti ambayo yatahitaji mchakato mwingine kutekelezwa. Tukichukua mfumo wa Serkali moja halikadhalika itahitaji mchakato.
Tukiacha ya muungano,mapendekezo mengine yanaonekana kujikita zaidi katika muundo wa utawala na taasisi zake. Kuna mapendekezo ya majimbo. Hili likikubaliwa litahitaji mchakato mwingine kuhainisha mipaka, kuweka sheria zitakaongoza mfumo huu n.k. Ni kwa vipi haya yatafanyika katika kipindi kitakachokuwa kimesalia kuweza kufanya uchaguzi mkuu ulio huru na haki, ni kitu cha kujiuliza.
Kwa vyovyote vile hata tusipochukua mfumo huu wa majimbo, ni lazima kutakuwa na mabadiliko ya muundo wautawala ambao utahitaji taasisi na mfumo mpya kusimikwa kabla ya uchaguzi. Vinginevyo tutakuwa hatujatengeneza Katiba mpya!
Suala lingine la muhimu naambalo linahusiana na uchaguzi ulio huru na haki, ni taasisi itakayosimamiauchaguzi. Itashangaza ikiwa Katiba mpya haitaleta mabadiliko makubwa katikaTume ya Uchaguzi ili siyo tu ionekane huru bali pia itende haki katikau simamizi wa chaguzi.
Kikubwa hapa ni kuwa Tume ya Uchaguzi mpya ni lazima iwe na muda wa kuthibitisha uwezo na u-huru wake katika majukumu itakayopewa ili kuwajengea watu imani hiyo. Ni vigumu kuona wataweza kufanya hili katika kipindi hicho kifupi kitakachokuwa kimebaki na ikiwa kutakuwa na chaguzi ndogo za kutosha kuwapa watu nafasi za kuitathimini.
Je kwa hayo na mengine yanayo husiana na mabadiliko yatakayo ambatana na Katiba Mpya, ni rahisi kujiaminisha kuwa uchaguzi mkuu wa 2015 utafanyika chini ya Katiba hiyo mpya? Auni vyema kuanza kujiandaa vinginevyo na kuacha mchakato wa Katiba Mpya uendelee bila kuhuwaisha ili tupate kilicho bora.