Katiba yetu ni ya kwanza kwa ubovu duniani

Katiba yetu ni ya kwanza kwa ubovu duniani

Omusolopogasi

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2017
Posts
7,101
Reaction score
18,051
Mwana JF,

Hebu fikiria hili. Katiba yetu inasema Tume ya Uchaguzi ikishamtangaza mtu hakuna mtu anaruhusiwa kupinga matokeo mahakamani. Ulishafikiria siku mwenyekiti wa tume akimtangaza mtu yeyote kuwa Rais itakuwaje? Yaani fikiria akitamka kuwa rafiki yake (mathalani Hashimu Rungwe) ndiye mshindi wa Urais, regardless ya kura zake, anakuwa Rais. Kwa katiba hii, hakuna mtu anaruhusiwa kupinga mahakamani.

Hii Katiba ni ya hovyo kabisa. Katika katiba za hovyo ni ya kwanza duniani. Watanzania tuikatae. Mtu mwenye nia njema hawezi kukataa katiba mpya yenye kutoa haki na usawa. Ni mafedhuli tu yanakataa haki. Yamezoea vya kunyonga km makaratasi ya kura ya kupigia majumbani kwao na mahotelini na kuyapeleka kwenye vituo vya kura kwa mabegi. Yanaogopa vya kuchinja. Yanataka yaendelee kufanya ufedhuli bila kuzuiwa.

Eti yanasema yanashughulikia maji, elimu na afya. Yalikuwa wapi kushughulikia hayo tangu 1961? Yaeleze ni nchi gani iliyoendelea ambayo siku moja ilifika hatua ya kuacha kushughulikia maji, elimu na afya? Haya ni mambo ambayo nchi zote zinaendelea kushughulikia mpaka mwisho wa dunia. Hata Marekani, UK, Japan... zinashughulikia haya mambo mpaka leo hii. Biden kasema bajeti yake kubwa inakwenda mwenye miundombinu. Hata Marekani bado inashughulika na miundombinu. Hakuna siku hii kazi itaisha. Mbona 1961, Nyerere hakusubiri kila kijiji kipate maji na umeme kwanza ndio nchi ipate katiba? Mbona 1977, Nyerere, Jumbe na akina Msekwa hawakusubiri mpaka tuingie uchumi wa kati ndio katiba ya 1977 iandikwe?

Halafu yanasema katiba siyo sera yao. Akina JK, Waryoba, Butiku... ni UKAWA? Yaleyale aliyopita kukusanya maoni (Polepole, Kabudi, etc.) leo yanasema katiba mpya haihitajiki!! Yaani Tanzania hii ina majitu ya ajabu sana sana. Tena yanaongoza nchi eti! What a shame and disgrace to the country!

Tuikatae hii katiba kwa nguvu zetu zote.
 
Mwana JF,

Hebu fikiria hili. Katiba yetu inasema Tume ya Uchaguzi ikishamtangaza mtu hakuna mtu anaruhusiwa kupinga matokeo. Ulishafikiria siku mwenyekiti wa tume akimtangaza mtu yeyote kuwa Rais itakuwaje? Yaani fikiria akitamka kuwa rafiki yake say Hashimu Rungwe ndiye mshindi wa Urais. Itakuwaje?...
Tunaomba hiyo comparative study report uliyofanya, ili tujue ipi ni bora na tukapate uzoefu huko.
 
Majitu ya ajabu kweli kweli. Kaulize wanafunzi wa masters hapo mlimani. Wanazo nyingi.
Tunaomba hiyo comparative study report uliyofanya, ili tujue ipi ni bora na tukapate uzoefu huko.
 
Katiba gani hii! Miaka nenda inaibeba tu ccm! Hii nchi ni ya watanzania wote! Na siyo ccm pekee.

Mabadiliko ya Katiba hayakwepeki.
 
Huko Marekani kina Kennedy walichagua Ndugu zao..
Donald Trump washauri wake wakuu ni ni binti yake na mumewe...

Punguza kukariri
 
Nchi hii ina majitu ya ajabu ajabu sana. Utakuwa lingine kwa akili zake za kijinga linalinganisha maembe na mapapai halafu linajiona lina akili sana. Kwa nini lisilinganishe maembe kwa maembe na mapapai kwa mapapai?
Huko Marekani kina Kennedy walichagua Ndugu zao..
Donald Trump washauri wake wakuu ni ni binti yake na mumewe...

Punguza kukariri
 
Mwana JF,

Hebu fikiria hili. Katiba yetu inasema Tume ya Uchaguzi ikishamtangaza mtu hakuna mtu anaruhusiwa kupinga matokeo mahakamani. Ulishafikiria siku mwenyekiti wa tume akimtangaza mtu yeyote kuwa Rais itakuwaje? Yaani fikiria akitamka kuwa rafiki yake (mathalani Hashimu Rungwe) ndiye mshindi wa Urais, regardless ya kura zake, anakuwa Rais...
Kipi kinakuwa kibovu zaidi cha kwanza ama cha mwisho?
 
Si ndio nikwambia tafiti utazikuta pale maktaba ya UDSM? Kama una usingizi lala, siyo lazima uendelee kumwaga pumba zako hapa.
Suala ninalohoji, umejuaje kama Tanzania ina katiba mbovu kuliko zote?
Leta Taarifa ya utafiti wako.
 
Mwana JF,

Hebu fikiria hili. Katiba yetu inasema Tume ya Uchaguzi ikishamtangaza mtu hakuna mtu anaruhusiwa kupinga matokeo mahakamani. Ulishafikiria siku mwenyekiti wa tume akimtangaza mtu yeyote kuwa Rais itakuwaje?..
Tume ya madikiteta
 
Tunaomba hiyo comparative study report uliyofanya, ili tujue ipi ni bora na tukapate uzoefu huko.
CCM inaipinga katiba mpya kwa nguvu zote. Kwa sasa hatuna katiba na ndio unamwona Magufuli anasema mahakama nyang'anya pesa watu wote washitakiwao, kisha anakuja Samia na kusema futa kesi zote na warudishie pesa zao. Magufuli anasema atakaekubali masharti ya ujenzi wa bandari ya bagamoyoni Mwendawazimu, anakuja Suluhu anasema ni anza ujenzi. Katiba haitapatikana kwa maombi, bali kwa gharama kubwa sana.
 
Back
Top Bottom