Katibu Mkuu CCM, Daniel Chongolo kufanya mkutano na Waandishi wa Habari

Katibu Mkuu CCM, Daniel Chongolo kufanya mkutano na Waandishi wa Habari

Baraka Mina

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2020
Posts
586
Reaction score
590
Habari ya asubuhi ndugu wanajamvi, natumaini bila shaka mu wazima wa afya na mmeianza vema siku ya leo. Kwa ambao ni wagonjwa nawaombea kwa Mwenyezi Mungu Muumba wa awajalie nafuu ya haraka ili muweze kurejea katika majukumu yenu ya kila siku.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndg. Daniel Chongolo atafanya mkutano na waandishi wa habari siku ya kesho Alhamisi ya tarehe 20/05/2021 saaa sita kamili mchana (06:00 Mchana) katika ukumbi wa Halmashauri Kuu (NEC) Makao Makuu ya Chama jijini Dodoma. Matangazo ya moja kwa moja (mbashara) ya mkutano huu yatarushwa kupitia akaunti na kurasa za mitandao ya kijamii ya Chama Cha Mapinduzi, chaneli ya Youtube ya Chama Cha Mapinduzi, Chaneli Ten na vyombo mbalimbali vya habari vya nchini Tanzania.

Mkutano huu na waandishi wa habari utakuwa wa kwanza kwa Ndg. Daniel Chongolo kuufanya tangu alipoteuliwa na kuthibitishwa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho tawala mnamo tarehe 30/04/2021 kushika wadhifa huo katika Chama. Pia mkutano huu unafanyika wakati ambao Chama Cha Mapinduzi kimetoka kushinda kwa kishindo uchaguzi mdogo wa wabunge katika majimbo mawili ya Muhambwe na Buhigwe mkoani Kigoma.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kazi Iendelee. Nawatakia siku njema yenye mafanikio, tufanye kazi kwa maendeleo yetu na taifa.
Ndg. DANIELCHONGOLO. MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI.jpg

 
Sina shaka najua amelelewa vyema na Taasisi (Idara) pamoja na Baba yake Mzazi hivyo najua atatema Madini tupu na hatokuwa na Upuuzi kama aliokuwa nao Mpuuzi na Mnafiki aliyemtangulia na aliyemrithi hiyo nafasi Muhimu hasa Kiutendaji ndani ya Chama Tawala (CCM)
 
Sina shaka najua amelelewa vyema na Taasisi ( Idara ) pamoja na Baba yake Mzazi hivyo najua atatema Madini tupu na hatokuwa na Upuuzi kama aliokuwa nao Mpuuzi na Mnafiki aliyemtangulia na aliyemrithi hiyo nafasi Muhimu hasa Kiutendaji ndani ya Chama Tawala ( CCM )
Yajayo ni neema tupu.
 
Sina shaka najua amelelewa vyema na Taasisi ( Idara ) pamoja na Baba yake Mzazi hivyo najua atatema Madini tupu na hatokuwa na Upuuzi kama aliokuwa nao Mpuuzi na Mnafiki aliyemtangulia na aliyemrithi hiyo nafasi Muhimu hasa Kiutendaji ndani ya Chama Tawala ( CCM )
Huyu angalau ni mwanasiasa kuliko yule boya
 
Yule alikuwa kibaraka wa mwendazake....sasa anajutia muda..historia haitamuacha kamwe anajuta
 
Naona ccm inaenda kujivua gamba!!!ccm teka teka,lopoka lopoka,tisha tisha na mimina mimina marisasi mchana kweupe inaenda kuzikwa rasmi inakuja ccm ya hoja,mipasho na sanaa zenye lahaja za kisiasa! Hii ndio Tanzania ninayoijua Bwana!!!!ile ilikuwa Rwanda na Burundi ndani Tanganyika!!!
 
Naona ccm inaenda kujivua gamba!!!ccm teka teka,lopoka lopoka,tisha tisha na mimina mimina marisasi mchana kweupe inaenda kuzikwa rasmi inakuja ccm ya hoja,mipasho na sanaa zenye lahaja za kisiasa!!!!Hii ndio Tanzania ninayoijua Bwana!!!!ile ilikuwa Rwanda na Burundi ndani Tanganyika!!!
Mkuu hayo unayoyazungumza mbona unapotosha. Rwanda na Burundi ndani ya Tanzania?
 
Sina shaka najua amelelewa vyema na Taasisi (Idara) pamoja na Baba yake Mzazi hivyo najua atatema Madini tupu na hatokuwa na Upuuzi kama aliokuwa nao Mpuuzi na Mnafiki aliyemtangulia na aliyemrithi hiyo nafasi Muhimu hasa Kiutendaji ndani ya Chama Tawala (CCM)
Kwa ushabiki huu kwa katibu mpya wa CCM, mara utasikia GENTAMYCINE oh! Kanunuliwa, mara oh! GENTAMYCINE amerudisha kadi ya CHADEMA na anasubiri kupokea kadi ya CCM kutoka kwa katibu mpya wa CCM baada ya mkutano na waandishi wa habari! We subiri hawaishiwi na maneno.
 
Sina shaka najua amelelewa vyema na Taasisi (Idara) pamoja na Baba yake Mzazi hivyo najua atatema Madini tupu na hatokuwa na Upuuzi kama aliokuwa nao Mpuuzi na Mnafiki aliyemtangulia na aliyemrithi hiyo nafasi Muhimu hasa Kiutendaji ndani ya Chama Tawala (CCM)
Usipende sana kutukana wasitaafu Hawana nafasi ya kurekebisha walipokosea.

Tumuangalie huyu nae anakuja na nini?

Usije shangaa akaanza kumbwela tu.
 
Naona ccm inaenda kujivua gamba!!!ccm teka teka,lopoka lopoka,tisha tisha na mimina mimina marisasi mchana kweupe inaenda kuzikwa rasmi inakuja ccm ya hoja,mipasho na sanaa zenye lahaja za kisiasa! Hii ndio Tanzania ninayoijua Bwana!!!!ile ilikuwa Rwanda na Burundi ndani Tanganyika!!!
Tuseme tu ukweli CCM kabla ya JPM ilikuwa hoi taabani, watu walikuwa wakivaa sare za CCM wanazomewa mitaani. Leo hii Wana CCM wanavaa sare zao kwa kujiachia bila hofu yeyote.

Bashiru alifanya kazi kubwa ya kurudisha Mali za chama zilizokuwa zimeporwa na wajanja wachache ndani ya chama.
Bashiru amewezesha CCM iweze kujitegemea kimapato pasipokutegemea wahisani katika kuendesha Mambo yake ya chama.

CCM chini ya JPM, Bashiru na polepole imekuwa imara na yenye mvuto zaidi kuliko kipindi Cha kikwete.
 
Tuseme tu ukweli CCM kabla ya JPM ilikuwa hoi taabani, watu walikuwa wakivaa sare za CCM wanazomewa mitaani. Leo hii Wana CCM wanavaa sare zao kwa kujiachia bila hofu yeyote.

Bashiru alifanya kazi kubwa ya kurudisha Mali za chama zilizokuwa zimeporwa na wajanja wachache ndani ya chama.
Bashiru amewezesha CCM iweze kujitegemea kimapato pasipokutegemea wahisani katika kuendesha Mambo yake ya chama.

CCM chini ya JPM, Bashiru na polepole imekuwa imara na yenye mvuto zaidi kuliko kipindi Cha kikwete.
Ssm ya kipindi Cha jiwe ilikuwa imetekwa wanachama pamoja na viongozi wastahafu walikuwa na nidhamu ya woga yoyote aliyejaribu kwenda kinyume nae mkono wa chuma ulimfuata
 
Ssm ya kipindi Cha jiwe ilikuwa imetekwa wanachama pamoja na viongozi wastahafu walikuwa na nidhamu ya woga yoyote aliyejaribu kwenda kinyume nae mkono wa chuma ulimfuata
[emoji2][emoji2][emoji2] kwa hiyo na wananchi nao walitekwa na Jiwe wakaacha tabia ya kuwazomea Wana CCM mtaani.
 
Back
Top Bottom