Katibu Mkuu wa CCM atoa maagizo wakati huu chaguzi ndani ya chama zikiendelea

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
KATIBU MKUU WA CCM ATOA MAAGIZO WAKATI HUU CHAGUZI NDANI YA CHAMA ZIKIENDELEA.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Daniel Chongolo amewaagiza Makatibu wa Wilaya maeneo yaliyobainika kuwa na kasoro ikiwemo baadhi ya watia nia kunyimwa fomu kwenye uchukuaji fomu ngazi ya shina nchi nzima kurudia zoezi hilo kwa sababu CCM sio Chama cha mtu binafsi bali cha wanachama wote.

Maagizo hayo ameyatoa leo Jumatano tarehe 20 Aprili, 2022 jijini Dar es Salaam alipokuwa kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Wilaya ya Ubungo na Kinondoni.

"Nawaagiza Makatibu wa wilaya, Ubungo na wilaya zote nchini, maeneo yote ambayo tumebaini yana changamoto ya watu kunyimwa kuchukua fomu za kugombea ndani ya chama, tunarudisha zoezi la kutoa fomu, tunataka wale wote wenye dhamira ya kuchukua fomu wachukue bila kuwekewa vizuizi, hiki sio chama cha mtu, hiki sio chama cha maslahi binafsi, hiki chama ni cha wanachama, na ni lazima tutende haki kwa kuwa katiba yetu ya CCM inatutaka tufanye hivo." Katibu Mkuu Ndg. Chongolo ameeleza

Aidha ameoneza kuwa, "Dhamana tulizonazo hazijatupa haki ya kufanya maamuzi kwa ubinafsi, maeneo ambayo tumegundua yana hiyo changamoto napiga marufuku kuwanyima fomu wanachama, naagiza fomu ziendelee kutolewa kwa watu wote, zoezi la uchaguzi lisitishwe, wanachama wote wenye nia wapate haki ya kuchukua fomu na kugombea, kura ndizo zitakazo amua na sio vinginevyo", Katibu Mkuu Ndg. Chongolo amesisitiza

"Tunafuatilia na tukibaini kuna maeneo ambapo vitabu vilivyokuwa vimehakikiwa vimeongezwa majina ya watu wasiokuwemo kwenye utaratibu wa daftari la wanachama, Wakurugenzi /Makatibu wa uchaguzi watawajibika, hili sihitaji kusisitiza sana tutakutana baadae na hili ni kwa ngazi zote." Ameeleza Katibu Mkuu Ndg. Chongolo

Ameyataja baadhi ya maeneo yaliyobainika kuwa na changamoto hiyo kuwa ni pamoja na Wilaya ya Ubungo, Babati, Mbeya, Tabora na kusema ni lazima haki itendeke ndani ya chama kwa wanachama wote bila ubaguzi


Pia Katibu Mkuu amewaasa vijana kuacha kuwa wapambe tu wa wagombea, nao wana haki ya kugombea "Acheni kubaki vijana wa hamasa tu ama wapambe wa wagombea, chukueni fomu gombeeni na mkiona kuna mazingira ya kuwafungia milango, tuambieni haraka sisi tuna funguo za kufungulia."

Aidha Katibu Mkuu ameongeza kwa kuwapa Maelekezo Wenyeviti na Makatibu wa Umoja wa Vijana nchini Kukaa na vijana, kuwahamasisha kugombea na kusisitiza kuwa, hilo ni jukumu na wajibu usio na hiyari.
Your browser is not able to display this video.


Your browser is not able to display this video.
 
Kwa nini zisipatikane kwenye website yao? Haya mambo ya kutaka watu wafike ofisini kuchukua na kurudisha fomu yamepitwa na wakati. Wangetumia njia zote mbili ili kurahisisha zoezi.

Amandla...
 
Duu kweli mambo yanabadilika enzi zile yule jamaa alikuwa anasema " nireteeni yure " ole wenu sasa mfanye kinyume. Poleni wana ccm
 
Ndambi ya kupitia bila kupingwa inaitafuna ccm.
 
Kaziiendelee
 
Kuchukua fomu ni haki ya kila mwanachama
Mengine yatafuata baadaye sio kumnyima

Katibu mkuu yuko sahihi

Wapewe wote
 
Duu kweli mambo yanabadilika enzi zile yule jamaa alikuwa anasema " nireteeni yure " ole wenu sasa mfanye kinyume. Poleni wana ccm
Yule alijua nani mchapa kazi na nani mwizi!, wakati mwingine hii mifumo na taratibu zisizo na misingi imara inachelewesha maendeleo!
 
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…