Katibu Mwenezi wa CHADEMA wilaya ya Hai alalamikia uamuzi wa Halmashauri Kuu kujitoa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Katibu Mwenezi wa CHADEMA wilaya ya Hai alalamikia uamuzi wa Halmashauri Kuu kujitoa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Huyo kijana anaakili mno,amechoka kutumika na watu wabaya
Ana akili sana? Kwa nini hakuhoji wagombea wote wa hai kukatwa? Nani alikuwa agombee sasa hapo Hai? Amechoka kutumiwa na watu wabaya?! kwa hiyo sasa anatumika na Sabaya ni mtu mzuri?? Tapeli wa kimataifa huyu?msweeee!
 
Kumekuwa na malalamiko Mara kwa Mara kuwa mkuu wa wilaya ya Hai anawatumia kwa maslahi yake Reporters wa Mtandao wa Millard Ayo kinyume na maadili ya uandishi wa habari kwa siku nyingi lakini ushahidi haukuwekwa hadharani.

Lakini majuzi Katibu mwenezi wa Chadema alionekana akitoa taarifa kulaumu uongozi wa kitaifa kuhusu kujitoa uchaguzi wa serikali za mitaa.

Sasa ili kujua kuwa Sabaya DC wa Hai amefikia kutumia mbinu za KIJAMBAZI katika siasa huku maripota wa Millard Ayo wakitumika sikilizeni maongezi yaliyo naswa kati ya Lema mbunge wa Arusha na Humphrey Katibu mwenezi wa Hai akieleza alivyo chukuliwa na watu wa Sabaya wakiwa na silaha na kupewa statement ya kusoma au yampate yaliyo wapata wengine huku akirekodiwa na Millard Ayo reporter.

Je, credibility ya huyu kijana Millard Ayo imefikia that much low? Mtandao wake ambao ameujenga kwa jasho na damu na kupewa support na makundi mbalimbali anakubalije utumike na wahuni kama Ole Sabaya katika mambo ya hovyo?

Tumtaarifu tuu Sabaya kuwa wewe ujinga wako unaeleweka na watu wamekupuuza lakini usiharibie vijana wajasiriamali wabunifu shughuli zao kwa kuwashirikisha na utekaji.

Millard aelewe kuwa ingekuwa ni nchi ya utawala wa kidemokrasia kama hata hapo Kenya tukio hilo ni la mahakamani na kifungo cha utekaji nadhani ni 20 years, na kingemhusu.
 
Mwanzo wa mwisho wa Millard Ayo , tuliwaonya mara nyingi sana hawa vijana kwamba kutengeneza brand ni kazi ngumu mno na inaweza kuchukua miaka mingi sana , lakini kuiharibu yaweza kuchukua dk 5 tu .

Sabaya Mtu aliyefumaniwa akiomba rushwa ndogo ya mil 2 atakulipa nini Millard Ayo kiasi cha kukubali kutumikishwa kizembe namna hii ?
 
Lile tukio la kumkamata mlinzi aliekuwa anataka kufanikisha wizi wa hela ndio naweza amini amini
 
Yote sawa tu, hata ninyi mnamtukana, kumdhalilisha na kumdhihaki Raisi Magufuli kila siku hapa na hakuna kitu kinawapata, kuna wengine hadi wanatukana matusi ya nguoni lkn wanadunda tu, mpaka hata mlimzushia kifo lkn yote ni sawa tu, hivyo ni sawa pia na Ayo kufanya anavyotaka kwani ni Mtandao wake na hajakulazimisha kuutembelea.
 
Hivi kama una akili unatumwaje kufanya DHAMBI na unakubali? Sababu umepewa bastola. Alafu yanayoyatuma utayasikia tunapambana na mabeberu.utapambana na beberu kwa akili za kipuuzi kiasi hiki? LABDA MTAWEZA KUPAMBANA NA MABEBERU YA MBUZI ULIOWAFUGA. SIO MZUNGU.
 
Back
Top Bottom