Katibu Tawala Mkoa wa Songwe akagua kiwanda cha makaa ya mawe STAMICO na Mradi wa Barabara ya London - Kiwila

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe akagua kiwanda cha makaa ya mawe STAMICO na Mradi wa Barabara ya London - Kiwila

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Ileje, 08 Januari 2025 - Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda, amefanya ziara muhimu katika Kiwanda cha Makaa ya Mawe Stamico pamoja na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya London-Kiwila yenye urefu wa kilomita 5, iliyopo katika Wilaya ya Ileje.

Barabara hiyo ni kiungo muhimu kwa kiwanda hicho, kwani inasaidia kusafirisha malighafi kutoka mgodini yanakochimbwa makaa ya mawe hadi kiwandani ambako nishati safi ya makaa inatengenezwa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bi. Seneda amesema, "Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imetoa takribani shilingi bilioni 5.72 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii, hususan katika maeneo korofi ambapo daraja kubwa limejengwa ili kuhakikisha barabara inapitika muda wote."

Awali, katika kipindi cha mvua, barabara hiyo ilikuwa haipitiki, hali iliyokuwa ikisimamisha uzalishaji kiwandani. Hata hivyo, baada ya kukamilika kwa mradi huo, uzalishaji umeboreshwa na unafanyika bila kusimama kwa msimu, jambo ambalo limeongeza tija na ufanisi na kukuza uchumi wa Mkoa wa Songwe.
 
Barbara ya Kms 5, msiwe mnatujulisha!
Fanyeninmkimaliza mnyamaze.
Tunataka kusikia mradi kuanzia 50kms +
 
Back
Top Bottom