Katibu Tawala: Sabaya, hakupewa kibali chochote cha Maandishi kwenda kutekeleza majukumu nje ya kituo chake cha kazi

Katibu Tawala: Sabaya, hakupewa kibali chochote cha Maandishi kwenda kutekeleza majukumu nje ya kituo chake cha kazi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Katibu Tawala Msaidizi wa zamani wa Mkoa wa Kilimanjaro, Renatus Msangira (45), amepanda kizimbani akidai kwamba aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani humo, Lengai Ole Sabaya, hakupewa kibali chochote cha maandishi kwenda kutekeleza majukumu nje ya kituo chake cha kazi.

Msangira, ambaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa Jamhuri, ametoa madai hayo leo, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha wakati akitoa ushahidi wake akiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Filex Kwetukia.

Kwenye hii Kesi ya Uhujumu Uchumi inayomkabili aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Lengai Ole Sabaya na wenzake sita, Upande wa Serikali unatarajia kuwa na mashahidi 20 pamoja na vielelezo 16.

Washitakiwa wengine kwenye kesi hii ni Enock Mnken, Watson Mwahomange, John Aweyo, Sylvester Nyegu, Jackson Macha na Nathan Msuya.

Awali Wakili kwetukia aliwasomea maelezo ya awali ambapo alidai Januari 22,2021 Sabaya aliongoza genge la watuhumiwa wenzake sita na kwenda gereji inayomilikiwa na Francis Mrosso iliyopo eneo la Mbauda ambapo walikutana na mmiliki wa gereji hiyo na kumtuhumu anakwepa kodi, huku akifanya biashara hiyo ya gereji bila kutoa risiti za TRA.

Amedai kuwa Sabaya alimtisha Mrosso kuwa asipofanya kitu atampatia kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha.

Wakili huyo aliendelea kuieleza mahakama kuwa Sabaya alimtaka Fransis Mroso kutoa shilingi Milioni 90 ili awe huru ambapo kutokana na vitisho Mrosso alikubali kutoa fedha hizo.

Alidai kuwa mhanga huyo alitoa kiasi hicho cha fedha ambapo walienda benki ya CRDB tawi la kwa Morombo akiwa katika usimamizi wa washtakiwa wenzake Sabaya na kuwa kwa wakati huo Sabaya alikuwa nje ya benki hiyo akiwasubiri na baada ya kutoa fedha hizo walienda eneo la Sombetini ambapo Sabaya alikabidhiwa fedha hizo.

Pia soma;
Ole Sabaya asomewa mashtaka mapya 5 ya uhujumu uchumi. Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha yapewa mamlaka kusikiliza kesi
 
ngoja waje watetezi wake humu[emoji1787]
Huyu hapa.
 
Hakika Aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya HAI Bw.SABAYA Alikuwa na MADARAKA Makubwa sana yaliyomwezesha KUWATISHA Watu mbalimbali Wasiotekeleza Akitakacho kwa kuwaamulia Aina ys KESI za KUWAPA
Akimsomea Mashtaka yanayomkabili Sabaya na Wenzake 6 Mwendesha Mashtaka alisema Sabaya alimwambia Mmiliki wa Gereji Bw. MROSSO asipotoa Sh.Mil.90 Atamfungulia Mashtaka ya UHUJUMU
UCHUMI na KUTAKATISHA PESA Bw.Mrosso alitoa PESA hizo.
Najiuliza Baadhi ya Maswali
Je SABAYA alikuwa anashirikiana na Nani kuwafungulia Watu Mashtaka ya MAKOSA Anayoyataka Yeye?
Kwa vyovyote ni Polisi na DPP
Je Walinzi wa MBOWE Tukisema Aliwachagulia SHTAKA ili Awakomoe na Kumwingiza MBOWE tutakuwa tunakosea kwa Sababu UWEZO huo Alikuwa Nao

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Hakika Aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya HAI Bw.SABAYA Alikuwa na MADARAKA Makubwa sana yaliyomwezesha KUWATISHA Watu mbalimbali Wasiotekeleza Akitakacho kwa kuwaamulia Aina ys KESI za KUWAPA
Akimsomea Mashtaka yanayomkabili Sabaya na Wenzake 6 Mwendesha Mashtaka alisema Sabaya alimwambia Mmiliki wa Gereji Bw. MROSSO asipotoa Sh.Mil.90 Atamfungulia Mashtaka ya UHUJUMU
UCHUMI na KUTAKATISHA PESA Bw.Mrosso alitoa PESA hizo.
Najiuliza Baadhi ya Maswali
Je SABAYA alikuwa anashirikiana na Nani kuwafungulia Watu Mashtaka ya MAKOSA Anayoyataka Yeye?
Kwa vyovyote ni Polisi na DPP
Je Walinzi wa MBOWE Tukisema Aliwachagulia SHTAKA ili Awakomoe na Kumwingiza MBOWE tutakuwa tunakosea kwa Sababu UWEZO huo Alikuwa Nao

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
Hakuna shaka yoyote kwamba Sabaya alishirikiana na Mamlaka yake ya uteuzi kufanya yote aliyoyafanya ikiwemo ubakaji , yaani mamlaka ilikuwa inajua leo Sabaya atambaka nani na ni bar ipi atakunywa pombe bila kulipa .

Malalamiko kuhusu Sabaya Magufuli aliyasikia na kuyaona lakini bado alimuacha tu , unawezaje kumtenganisha na uchafu wa Sabaya ?
 
Anarukaruka tu huyo Sabaya kama Maharage ya Mbeya eti aliagizwa kutoka juu!!!!kwenda kufanya Ujambazi wa kijinga huo!!!!What Goes Around Comes Around
 
Ebu Kalime acha ujinga
Naona Walikutoa Ubongo wote
JamiiForums1980995331.jpg


Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom