Inaniumiza sana.kila demu ninayempata anakuwa na shida moja tu. Yaani hazipiti siku 2 anaomba pesa. Hii tabia imekuwa kwangu kufanyiwa ni kawaida.
Nimepata msichana nikaanza sema moyo ngoja nikae hapa. Tumeonana mara moja kesho yake ananambia simu yake mbovu nimnunulie nyingine. Nlijisikia vibaya kidogo why so soon?
Mwingine ndani ya masaa 6 anaomba nimwongezee tsh 40,000 anunue gas imeisha. Nikamtumia 30,000. After two days ananambia simu yake imepasuka kikoo. Ni Samsung kioo kaambiwa 200,000 naye hana hela.so sitompata hewani baada ya ule muda.
Nikasikitika naye nikamwambia ntamwombea simu ipone.akakata simu.naendelea kumwona online.nikapost picha flani na wana Insta akaniona nakula maisha. Akanipigia kulaumu sana.kuwa nawezaje kwenda out huku sijamtumia pesa? Nlishangaa sana.
Nikaja pata mwingine.tumewasiliana kidogo tu siku mbili anasema biashara yake imekata sana anahitaji aongezewe 400,000. Ili achukue mzigo.nikamwambia hilo suala tuliweke kwenye maombi. Akakasirika. Meseji zangu hakujibu week nzima. Nikaja tuma text kuwa nimepata 350,000 akajibu akiniita sweet n.k nikamuuliza texts zangu mbona alikuwa hajibu akasema alikuwa tight sana kutafuta pesa.
Huyu mwingine ndani ya week moja amefiwa na mama yake wa kufikia(nlimuuliza why afikie kwa mtu wakati miaka yote amezaliwa Dar) hakunijibu. Ila nlishangaa huyu dada anasema wazazi wake wanaishi sinza. Amekulia sinza anafanya kazi Dar. Sasa why afikie kwa huyo mama?
Haya ....mara shangazi yake wa mwanza kafariki inabidi aende.asipoenda ndugu hawatamwelewa.so anaomba nauli.wakati huo hup she told me pesa zake anazitumia kumhudumia mama yake mgonjwa.nikisema nami nataka nikamsalimie.vipengele vinakuwa vingi sana.
Mwingine siku moja tu tumefahamiana tena kwenye mtandao wa kijamii.kesho yake anataka nimtumie 40,000 aende salon.
Huyu wa last week nampenda, naogopa mpigia au pokea simu yake.maana kila nikimpigia lazima ataomba pesa ya beer.kila akipiga mwishoni nimtumie pesa ya beer.nlimshauri sababu ana advanced diploma ya mambo ya management in something a apply TBL hakujibu kitu.
Basi tu nmejikunyata maskini naumia sana moyoni.WHY ME? NAJIULIZA. AU ndo nyota ya Buzi? This isnt fair kabisa. Wadada muwe na huruma. Tujaribu hata kupendana dada zanguni. Naumia sana, nakonda kwa mawazo.