Katika Uwanja wa Jamhuri wa Jijini Dodoma Simba imeichapa JKT Tanzania Mabao 4 kwa 0

Katika Uwanja wa Jamhuri wa Jijini Dodoma Simba imeichapa JKT Tanzania Mabao 4 kwa 0

Mm ushabiki sipendi sana japo naipenda yanga Ila ukweli usemwe tungeongezewa ata mwezi mmoja mbele kikosi chetu kielewane. Tukienda kichwa kichwa tarehe 18 tunaweza kufa nyingi. Simba inacheza mpira jamani. Nasasa hapo ulikuwa kwenye ule uwanja mbovu? Jiulize wangekutana Taifa issue ingekuwaje?
Ha ha ha, mkuu big up kwa kuwa muwazi, japo wana Yanga wenzio watakutukana.
 
Jana nilikuwa naangalia mashabiki wa yanga waliokaa katikati ya mashabiki wa simba. Nilipoangalia zaidi nikagundua yafuatayo

1. Nimashabiki wa simba pekee wanye uhakika kuwa muda timu yao itashinda

2. kumbe mashabiki wa yanga huwa wanainjoi soka biriani la ngamia lipigwalo na simba

3. Kuangalia mpira wa simba inàkufanya usahau shida zako kwa muda kwakuwa mpira hauwezi kwisha bila kupewa goli au pasi ya kuombea mkopo ambao utapewa bila riba

4. Kama una stress na pressure wataalamu wanaweza kukushauri kwa Tanzania uangalie mpira wa simba

5. Hata malaika mbinguni wakitaka kuangalia burudani ya soka Tanzania huangalia mechi za simba na kama mtoa roho akija kukutoa roho na akakuta unaangalia soka la simba ataahirisha kwa muda na kuungana nawe kuishangilia simba mpira ukiisha ndipo ataichukua roho
 
Mambo 10 nilioyaona JKT vs SIMBA

1: WOW. Just WoW. No doubt, Tumeshuhudia One of the best Entertaining football matches kwenye VPL. Pasi zimepigwa na kutembea katika pitch ya Jamuhuri? Unbelievable! Ile ndo Tofauti ya Pira Biriani na Pira Gimbi😀

2: Approach ya Sven ni Ishara kuwa alifanya home work yake vizuri ya kuifatilia JKT na Kuielewa pitch ya Jamuhuri. Kwanini alitumia 4-4-2 'Diamond'?

3: Zaidi ya Asilimia 80, mabao mengi yanayofungwa Jamuhuri yanatokana na mipira ya juu. Unahitaji kuwa na straika wawili wenye nguvu hewani, unahitaji kuwa na viungo bora wenye uwezo wa kupiga pasi ndefu za juu kwenye boksi ya wapinzani

4: Wapi JKT walikwama? Baresi alikosa nidhamu kwenye kuukabidi mpango kazi wa Simba. Alitakiwa kuiweka timu kwenye Low Block defensive systeam kwa dakika 15 za kwanza ili kuivuruga plan ya Sven. Bahati mbaya, alifunguka, akaitawanya timu, Akaadhibiwa

5: LUIS MIQUISSONE🙌 WHAT A PLAYER🙌 Brain yake ya soka inatisha sana. Movement zake, pasi zake na maamuzi yake kwenye eneo la mwisho zilivunja sana mistari ya kiungo na ulinzi ya JKT

6: Ile pacha ya mabeki wa kati wa JKT, ilikuwa poor sana kwenye mawasiliano. Walitegeana kwenye maamuzi. Ni kosa la jinai kuwa hovyo vile dhidi ya mastraika wenye uchu kama wa Simba

6: Meddie Kagere🙌 Asipokufunga kwa kichwa, atakufungwa kwa mguu. Yuko strong sana. Very Powerful kwenye kugombea mipira, chini na hewani. Siamini kama kuna Plan ya mechi ya mpira wa miguu isiyomuhitaji straika wa aina yake

7: Larry Bwalya🙌 Ball Dancer! Achana na uwezo wake wa kucheza na mpira, Vision ya huyu jamaa ni kiboko. Vipimo vyake vya pasi ya mita 20+ huwa havidanganyi

8: Marefa wawe Fair na Morrison. This is Too much🙌 Ni kama wapinzani wanamkamia. Anachezewa rafu za hovyo sana na hakuna adhabu zinazotolewa

9: Joash Onyango🙌 Nusu mtu, Nusu Chuma🙌 Wawa anawapa Simba utulivu na akili, Onyango anawapa nguvu, timing na kasi. Adam Adam na Kelvin Sabato walikuwa kwenye mateso makubwa sana

10: Mohammed Hussein, Kapombe, Manula🙌 Ni ngumu sana kushinda mechi dhidi ya Simba watatu hawa wakiwa kwenye ubora wao

Nb: Mwambieni Kocha mpya Asije na mabegi mengi 😀.

Source: KamweTv
 
Ili yanga waweze kulingana na Simba piint ni vema wakaomba tff simba wacheze michezo 10 pungufu vinginevyo simba itaendelea kuiburuza yanga
 
Back
Top Bottom