Kauli ya Jaji Tiganga kwamba huenda Shahidi Ling'wenya alikuwa anapewa majibu ya maswali aliyoulizwa yawaibua Wadau

Sijui kwa waliokuwepo mahakamani labda watuambie ila kwa uelewa wangu mimi ni kama alikua anapiga kijembe kwa upande wa jamhuli ambao mashahidi wanao waleta wanajikoroga sana ila shahidi wa utetezi kaflow vizuri bila vifugumizi ndio jaji akapiga dongo hilo kama kuchombeza.
 
Kulikuwa na mtu anampatia majibu huyo shahidi hapo mahakamani?
 
Sasa kauli ya jana ya Tiganga unaisemaje? Waziwazi kuwa huyu anapewa majibu? ameonesha yuko biased vibaya sana. He must disqualify himself from the conduct of the case
 
unaweza kudhani hivyo na hii nimeiona twita, lkn kwa mwenendo wake tangu amepokea kesi hii, ndiyo maana majority have raised concern!
Definitely shahidi ameflow vizuri kwa vile alikuwa anaongea ukweli uliompata na si kubumba. Ukibumba utasahau tu na utajichanganya you can not perfect memory when telling lies
 
jamhuli ambao mashahidi wanao waleta wanajikoroga sana ila shahidi wa utetezi kaflow vizuri bila vifugumizi ndio jaji akapiga dongo hilo kama kuchombeza.
Kwa upande huu wa shilingi, nakubaliana na wewe, ila hoja ya msingi Jaji hakupaswa kutamka.
 
Si ndiye aliyesema hivi juzi, kwa ku'quote' msemo wa jaji maarufu wa Uingereza kwamba "Justice must not only be seen..." sijui ndiyo hivyo; lakini maana yake ikiwa kwamba yeye anasimamia sheria na haki.

Wasomi wetu hupenda sana kujionyesha kuwa wajuaji, huku matendo yao yakiwa ni tofauti kabisa.
 
Kwahiyo mama anakukeleketa sana acha ujinga ngosha wewe
Mna visingizio sana tulieni dawa iwaingie maana mlitamba sana mama anaupiga mwingi.

Mkome kabisa tabia ya kuingilia mahakama
 
Kulikuwa na mtu anampatia majibu huyo shahidi hapo mahakamani?
Apatiwe majibu ya nini wakati shahidi amefundishwa kwa theory na vitendo somo lake na akalielewa vizuri.
 
Majaji wenye hukumu zao mfukoni tayari ndio maana huwezi kusikia hata siku moja MAJAJI WATANZANIA WANAPEWA FURSA HATA JUMUIYA YA MADOLA hawana TRACK RECORD za kuwabeba kama wakenya zambia zimbabwe south africa nk
 
Kwa ratiba ya juzi jana tulisikia atakuja shadhidi mwingine upande wa mashitaka na wote walitarajia hivyo,ghafla upepo ukachange na kuambiwa utetez wapandishe shahidi wao.

Kilichonishangaza ni kuona ling'wenya anajibu maswali kwa kueleweka na mtitiririko unaoeleweka kuliko wale wa mo energy na mambo ya utalii, binafsi nimepata shida kujua kama aliandaliwa au vipi?

Kiukweli kama jana ameshitukizwa na ametoa maneno yale basi ule utakuwa na ukweli wenyewe kwa maana hakuonekana hata kufikiria katika kutoa majibu yake.

NB: Kiukweli kama unapanda mahakaman na kuhapa kwa jina lake then ukatoa uongo ambao hata nafsi yako inajua kuwa ni uongo hapo lazima karma ikukute tu.
 
Kwa ratiba ya Juzi Jana tulisikia atakuja shadhidi mwingine upande wa mashitaka na wote walitarajia hivyo,ghafla upepo ukachange na kuambiwa utetez wapandishe shahidi wao.
Watesi wa Mh Mbowe kwenye kesi hii wana jambo la kujifunza sana.
 
Kesi ina matobo matobo na usnitch mwingi sana.

Kwa ile ambush. Na wasi wasi Kuna mtu anampatia majibu.

Komando yuko makini na tayari muda wowote eh?
 
Kwa ratiba ya Juzi Jana tulisikia atakuja shadhidi mwingine upande wa mashitaka na wote walitarajia hivyo,ghafla upepo ukachange na kuambiwa utetez wapandishe shahidi wao...
Duh sisi watz bwwna mtu akifanya vizui basi ni shida akikosra ni shida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…