Akihutubia kwenye maazimisho ya miaka 20 ya jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro Septamba 17, 2024 rais Samia Suluhu Hassan amesema kuwa uovu wote uliopangwa kwenye mkutano wa chama kimoja cha upinzani (CHADEMA) anazo taarifa zote
Rais amesema kuwa interenjesia ya vijana wake ina uwezo mkubwa imepata taarifa za kikao chao chote kilichofanyika Septemba 11 mwaka huu na kwamba uovu wao wote waliopanga juu ya Serikali yake ameufahamu
Hivi karibuni baada ya kifo cha kada wake aliyetekwa na kuuwawa na watu wanaodaiwa wasiojulikana viongozi wa CHADEMA walikutana Arusha na kufanya kikao cha dharura cha kamati kuu
Kikao hicho kilitoka na maazimio kuwa ifikapo septamba 23 mwaka huu vijana wote wa chama hicho nchi nzima wakutane jijini Dar na kufanya maandamano ya amani
Lengo la maandamano hayo ni kushinikiza watu waliomteka na kumuua kada wao Ally Kibao wanafahamika na kuchukulia hatua za kisheria na makada wake watatu Soka na wenzake waliotekwa na watu hao hao wasiojulikana waachiwe huru au kama wameuwawa miili yao ikabidhiwe kwa ndugu zao ili izikwe
Kauli ya Rais Samia kuwa interejensia ya vijana wake iko vizuri na ndio maana kilichojadiliwa kwenye kikao hicho cha CHADEMA hotuba nzima anayo na kujua uovu wao mwingine waliopanga inamaanisha kuwa vijana wake wa kitengo ni miongoni mwa baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho
Pia kauli hiyo ya Rais inaashiria kuwa kama sio baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho kuwa watu wa kitengo basi vijana wake wa TISS au Polisi wameweka vifaa vya kunasa sauti kwenye ukumbi uliofanyika kikao hicho cha dharura cha CHADEMA cha kamati kuu ambacho ni cha viongozi wa juu tupu (Vingunge)
Kama ni kweli kiongozi mmoja wapo wa juu wa CHADEMA ni mtu wa TISS basi yamkini chama hicho hakiko salama na siri zake nyingi zitaendelea kutoka na kufika Serikalini bila yao kujua nani anazipeleka
Hivyo CHADEMA wanahitaji nao kufanya intelejensi yao iliyotukuka ya kumbaini kiongozi au viongozi hao wa kamati kuu ya chama hicho ambao ni watu wa kitengo
Comasa
PIA SOMA
- Rais Dkt. Samia: Nina taarifa ya kikao chao cha Arusha, wanapanga uhalifu, Serikali ya Tanzania haiondoshwi hivyo
Rais amesema kuwa interenjesia ya vijana wake ina uwezo mkubwa imepata taarifa za kikao chao chote kilichofanyika Septemba 11 mwaka huu na kwamba uovu wao wote waliopanga juu ya Serikali yake ameufahamu
Hivi karibuni baada ya kifo cha kada wake aliyetekwa na kuuwawa na watu wanaodaiwa wasiojulikana viongozi wa CHADEMA walikutana Arusha na kufanya kikao cha dharura cha kamati kuu
Kikao hicho kilitoka na maazimio kuwa ifikapo septamba 23 mwaka huu vijana wote wa chama hicho nchi nzima wakutane jijini Dar na kufanya maandamano ya amani
Lengo la maandamano hayo ni kushinikiza watu waliomteka na kumuua kada wao Ally Kibao wanafahamika na kuchukulia hatua za kisheria na makada wake watatu Soka na wenzake waliotekwa na watu hao hao wasiojulikana waachiwe huru au kama wameuwawa miili yao ikabidhiwe kwa ndugu zao ili izikwe
Kauli ya Rais Samia kuwa interejensia ya vijana wake iko vizuri na ndio maana kilichojadiliwa kwenye kikao hicho cha CHADEMA hotuba nzima anayo na kujua uovu wao mwingine waliopanga inamaanisha kuwa vijana wake wa kitengo ni miongoni mwa baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho
Pia kauli hiyo ya Rais inaashiria kuwa kama sio baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho kuwa watu wa kitengo basi vijana wake wa TISS au Polisi wameweka vifaa vya kunasa sauti kwenye ukumbi uliofanyika kikao hicho cha dharura cha CHADEMA cha kamati kuu ambacho ni cha viongozi wa juu tupu (Vingunge)
Kama ni kweli kiongozi mmoja wapo wa juu wa CHADEMA ni mtu wa TISS basi yamkini chama hicho hakiko salama na siri zake nyingi zitaendelea kutoka na kufika Serikalini bila yao kujua nani anazipeleka
Hivyo CHADEMA wanahitaji nao kufanya intelejensi yao iliyotukuka ya kumbaini kiongozi au viongozi hao wa kamati kuu ya chama hicho ambao ni watu wa kitengo
Comasa
PIA SOMA
- Rais Dkt. Samia: Nina taarifa ya kikao chao cha Arusha, wanapanga uhalifu, Serikali ya Tanzania haiondoshwi hivyo