Kauli ya Rais Samia kwa wananchi akiwa Kariakoo kwamba "Serikali inawabeba" ina ukakasi

Kauli ya Rais Samia kwa wananchi akiwa Kariakoo kwamba "Serikali inawabeba" ina ukakasi

Buyaka

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2010
Posts
1,705
Reaction score
1,953
Baada ya kuahidi kushughulikia changamoto za soko la Kariakoo, Mhe. Rais S.S. Hassan amewaambia wananchi "na nyinyi wakati serikali inawabeba, wanasema abebwae hujikaza, na nyinyi jitahidini kufuata sheria zinazowekwa katika maeneo mlipo maanake nimeona njia zote zimezingiwa, vibanda kila pahali..."

My take:
Tafadhali sana viongozi wetu, tunaomba muondoe huo mtazamo kwamba mnatufanyia hisani!

Serikali na Rais wa nchi hawambebi mtu. Wanatimiza wajibu wao. Rais aliomba kura anatimiza ahadi za kutatua matatizo. Watumishi wa umma wa kawaida wameajiriwa, wanalipwa mshahara, wanatimiza wajibu wao. Hakuna anaebebwa.

Isitoshe, utaratibu (au kutokuwepo na utaratibu) wa kuuza bidhaa njiani na kujenga vibanda ovyo ovyo ni serikali yenu imekuwa ikihubiri kwa nguvu kwamba hakuna sheria nchi hii inayosema Mmachinga haruhusiwi kufanya biashara popote.

Kama mmebadilisha mwelekeo msituambie mnatubeba! Please!

Clip hii hapa ya Rais na Makamu wake wa Rais wakidadavua kinaga ubaga policy za umachinga na haki zao kwa mtazamo wao, sio wa kwetu sisi Wamachinga.


 
Nadhani kauli yake imeeleweka, vibanda kila kona bila kufuata utaratibu wala sheria mpaka njia inazibwa ni kubebwa na serikali tofauti na hapo walitakiwa kuondolewa.
 
Kama jinsi ambavyo Mwendazake hakusikia ushauri juu ya kuwa Treat machinga (najua waliotangulia walimuonya)..Sasa hata mama namshauri aupuuze ushauri huu.
 
Nadhani kauli yake imeeleweka, vibanda kila kona bila kufuata utaratibu wala sheria mpaka njia inazibwa ni kubebwa na serikali tofauti na hapo walitakiwa kuondolewa.
Kwa hiyo serikali ilivunja sheria kwa kuwabeba Wamachinga ?

Kwa nini kawaambia wafuate sheria kama anawabeba ?
 
Back
Top Bottom