Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
IPUUZE KAULI YA "TUTAFUTE PESA" KWA HATMA ILIYONJEMA BASI MTAFUTE MUNGU WAKO.
Anaandika, Robert Heriel
Yule Shahidi!
Andiko hili lisomwe na Vijana wote.
Usiwe mtumwa wa Pesa.
Usiihusudu hata Kama unaambiwa ni tamu. Kamwe usije kujidanganya. Hakuna Raha yoyote ya kuwa na pesa kama huna Mungu.
Hakuna Raha yoyote ya kuwa na elimu kubwa Kama huna Mungu. Waliosoma wataungana na Mimi.
Hakuna Raha yoyote ya kuwa na Mke/mume mzuri kama hauna Mungu. Wenye wenza wazuri tunalijua hili fika na ni mashahidi.
Kila kitu Duniani ni chakawaida isipokuwa Mungu. Utakiona cha thamani ukiwa haupo nacho, lakini ukiwa nacho huwa chakawaida. Kabisa!
Ila kuwa na Mungu huwezi kuona ni kawaida, utakuwa na furaha kuliko kawaida.
Vijana acheni kujihangaisha na kutafuta pesa, nisikilizeni Mimi Taikon, mara nyingi ukiona Jambo ninalisema ujue nimelipima, nilimelichunguza, siongei Kwa mihemko.. naongea Kwa uhalisia.
Mtafute Mungu wako, mpende, mthamini, sikiliza sheria zake, fuata maagizo yake alafu ukiishi maisha mabovu nakuruhusu uniite MBWA! Nakuruhusu unitukane tusi lolote.
Falsafa ya Yesu (moja ya wanafalsafa ninaopenda Falsafa zake) anakuambia; Kwanza utafuteni Ufalme wa Mungu, na haki yake, na mengine yote mtazidishiwa.
Vijana, jaribuni kunielewa.
Nimeona Vijana wengi wakihangaika na kulialia, wamechanganyikiwa.
Ukijifanya Mkaidi, basi sio ajabu haya yatakupata,
Dunia itakuacha Kwa kila kitu Kwa sababu unakimbizana nayo, utachelewa Maeneo mengi tena nyeti;
Utachelewa kuoa na kuolewa kisa kutafuta Pesa.
Utachelewa kujenga na kuwa na mji wako.
Utakuwa Under attacks Hali Internal & External Attacks. Ndipo mtu anakuwa na Msongo wa Mawazo,
Kukata tamaa, kuchanganyikiwa Kwa kuenda huku na huko kutafuta msaada mara Kwa wachungaji mara masheikhe mara Waganga. Hiyo ni Dalili ya kushambuliwa.
Kujiingiza kwenye Madawa au pombe,
Kukataliwa na Wakati, watu na mahali unapoishi.
Kuwa mwaminifu Kwa Mungu wako.
Hakuna sababu yoyote itakayokufanya usimuamini Mungu aliyekuumba na kuumba huu ulimwengu.
Kumbuka Mungu ndiye mwanzo hivyo atakusaidia kuanza Jambo lolote, naye ndiye mwisho atakusaidia kumaliza Jambo lolote utakalolianza.
Tafuta Mungu ili upate Pesa
Taikon leo sitaki kusema mengi.
Nipumzike sasa!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel
Yule Shahidi!
Andiko hili lisomwe na Vijana wote.
Usiwe mtumwa wa Pesa.
Usiihusudu hata Kama unaambiwa ni tamu. Kamwe usije kujidanganya. Hakuna Raha yoyote ya kuwa na pesa kama huna Mungu.
Hakuna Raha yoyote ya kuwa na elimu kubwa Kama huna Mungu. Waliosoma wataungana na Mimi.
Hakuna Raha yoyote ya kuwa na Mke/mume mzuri kama hauna Mungu. Wenye wenza wazuri tunalijua hili fika na ni mashahidi.
Kila kitu Duniani ni chakawaida isipokuwa Mungu. Utakiona cha thamani ukiwa haupo nacho, lakini ukiwa nacho huwa chakawaida. Kabisa!
Ila kuwa na Mungu huwezi kuona ni kawaida, utakuwa na furaha kuliko kawaida.
Vijana acheni kujihangaisha na kutafuta pesa, nisikilizeni Mimi Taikon, mara nyingi ukiona Jambo ninalisema ujue nimelipima, nilimelichunguza, siongei Kwa mihemko.. naongea Kwa uhalisia.
Mtafute Mungu wako, mpende, mthamini, sikiliza sheria zake, fuata maagizo yake alafu ukiishi maisha mabovu nakuruhusu uniite MBWA! Nakuruhusu unitukane tusi lolote.
Falsafa ya Yesu (moja ya wanafalsafa ninaopenda Falsafa zake) anakuambia; Kwanza utafuteni Ufalme wa Mungu, na haki yake, na mengine yote mtazidishiwa.
Vijana, jaribuni kunielewa.
Nimeona Vijana wengi wakihangaika na kulialia, wamechanganyikiwa.
Ukijifanya Mkaidi, basi sio ajabu haya yatakupata,
Dunia itakuacha Kwa kila kitu Kwa sababu unakimbizana nayo, utachelewa Maeneo mengi tena nyeti;
Utachelewa kuoa na kuolewa kisa kutafuta Pesa.
Utachelewa kujenga na kuwa na mji wako.
Utakuwa Under attacks Hali Internal & External Attacks. Ndipo mtu anakuwa na Msongo wa Mawazo,
Kukata tamaa, kuchanganyikiwa Kwa kuenda huku na huko kutafuta msaada mara Kwa wachungaji mara masheikhe mara Waganga. Hiyo ni Dalili ya kushambuliwa.
Kujiingiza kwenye Madawa au pombe,
Kukataliwa na Wakati, watu na mahali unapoishi.
Kuwa mwaminifu Kwa Mungu wako.
Hakuna sababu yoyote itakayokufanya usimuamini Mungu aliyekuumba na kuumba huu ulimwengu.
Kumbuka Mungu ndiye mwanzo hivyo atakusaidia kuanza Jambo lolote, naye ndiye mwisho atakusaidia kumaliza Jambo lolote utakalolianza.
Tafuta Mungu ili upate Pesa
Taikon leo sitaki kusema mengi.
Nipumzike sasa!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam