Kauli za Mkuu wa Mkoa wa Dar, Amos Makalla, zinakiuka Haki za msingi za Binadamu

Kauli za Mkuu wa Mkoa wa Dar, Amos Makalla, zinakiuka Haki za msingi za Binadamu

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu.

Najua Mkuu wa Mkoa, ametoa kauli hiyo kuhusiana na kukerwa na vitendo vya vijana wadogo, wanaofahamika kwa jina la Panyaroad, kwa vitendo vyao vya kuvunja nyumba za wakazi wa jiji la Dar, kufanya wizi wa vitu mbalimbali, kujeruhi hadi kusababisha vifo, kama ilivyotokea hapo majuzi huko Kawe.

Lakini nijaribu kumuuliza Mkuu wa Mkoa wa Dar, hivi yeye anadhani kwa kutumia vitisho hivyo, ndiyo atakuwa amepata ufumbuzi wa vitendo hivyo vya Panyaroad?

Hivi anajua "impact" ya kuyatamka maneno hayo hadharani, akiwa ndiye Mwenyekiti, wa Kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa huo wa Dar?

Nimuulize tena Mkuu wa Mkoa, hivi anajua kwa kuyatamka hayo maneno, ni kama ametoa "blessings" zake kwa Polisi wetu, waweze kujeruhi na hata kuua hao wanaoitwa Panyaroad, bila kwanza kuwahoji na kupata ushahidi wa hao wahalifu?

Hivi yeye Mkuu wa Mkoa, anatambua kuwa kwa tamko hilo anakiuka misingi ya Haki za binadamu?

Ninaposema hivyo, siyo kuwa naunga mkono vitendo hivyo vya kinyama vya hao wanaojiita Panyaroad, la hasha, nia yangu ni kulitaka Jeshi la Polisi, litende Kazi zake kwa Weledi mkubwa, kwa kufuata sheria.

Polisi wetu wanafahamu kuwa Hawama mamlaka ya kuua raia yeyote bila msingi wowote.

Tunafahamu pia kuwa Katika nchi yetu, ni mhimili wa Mahakama pekee, uliopewa mamlaka ya kumtia hatiani raia yeyote na kutoa hukumu.

Nchi hii inaendeshwa kwa kufuata misingi ya kisheria.

Hivi anaweza kutuambia kwa kuyatamka hayo maneno, ni sheria gani inayomruhusu yeye kama Mkuu wa Mkoa, aliagize Jeshi lake la Polisi, litekeleze majukumu yake, pasipo kuzingatia sheria za nchi hii?

Kwa hiyo Mkuu wa Mkoa, Amos Makala, anapaswa aombe radhi kwa wakazi wa Mkoa wa Dar, kwa matamshi aliyoyatoa, ambayo ni kinyume cha utawala bora, unaozingatia sheria.
 
Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu.
Siku ukikumbana na hao panya road wakikushughulikia, uje usome tena upuuzi uliouandika hapa
 
Watawala walioshindwa kuongoza sasa wameamua kuwapiga wanaowatawala, hao panyarodi uwepo wao ni matokeo ya sera zao mbovu za kiuchumi zilizofeli, wamewafukuza machinga barabarani, badala ya kuwaandalia maeneo rafiki wakafanyie biashara zao, wanawapeleka mafichoni pasipo na wateja.

Ajabu Mkuu wa Mkoa anakuja na kauli iliyojaa mihemko, bila kujali athari za kauli yake, hawa askari wetu waliozoea kupiga watuhumiwa vituoni, na kuwabambikia kesi, kusema watoto wakatafutwe mahospitalini hastahili kuendelea kuwepo ofisini, amefeli.
 
I wish I could be Police alafu nipangiwe hiyo operation hapo Dar es Salaam hao madogo wangejuta kuzaliwa ningekuwa radhi kupoteza hiyo kazi ila chamoto na wao wangekiona.

Nina roho mbaya kwa watu wapumbavu kama hao madogo yaani ukatili ambao ningewafanyia hata shetani angeshangaa. Pumbavu kabisa
 
I wish I could be Police alafu nipangiwe hiyo operation hapo Dar es Salaam hao madogo wangejuta kuzaliwa ningekuwa radhi kupoteza hiyo kazi ila changamoto na wao wangekiona.

Nina roho mbaya kwa watu wapumbavu kama hao madogo yaani ukatili ambao ningewafanyia hata shetani angeshangaa. Pumbavu kabisa
Kwa upeo wenu mdogo mnadhani hao panyarodi wamekaa sehemu wanawasubiri mkawakamate, hamjui wale ni waviziaji wanaofanya mambo yao kwa kificho, ili kuwapata inahitajika akili ya ziada tofauti na hii mihemko yenu mnayoandika hapa kama ya Mkuu wa Mkoa.
 
Ndugu yangu hujawahi kumbana na hawa mapanya aisee, hutaandika haya ukikutana nao. Haki za binadamu waanze wao...
Hofu ya aliyetoa hii mada ni huenda ambae sio panya road nae akashughulikiwa. Tatizo lipo hapo. Umakini unahitajika. Usifikiri kwamba panya road Wana alama sehemu kwamba inakua rahisi polisi kuwajua. Hapo Kuna mambo ya kutajana na Kuna ambao hawahusiki nao watakuwemo
 
Ndugu yangu hujawahi kumbana na hawa mapanya aisee, hutaandika haya ukikutana nao. Haki za binadamu waanze wao...
Najua madhara wanaosababisha hao mapanyarodi, lakini hivi kweli hayo maneno yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa, Amos Makala, unadhani ndiyo ufumbuzi wa kuwakomesha hao madogo wasiendelee kuwepo?
 
Siku ukisikia ndugu au rafiki yako unayemfahamu tabia zake sio mbovu, yuko hospitali amelazwa kwa kudhaniwa panya rodi, nawe uje usome huu ujinga wako ulioandika hapa.
sawa. at least I can sure and get compansated. lakini wewe unayetetea wapuuzi ni muovu.

ni heri uteseke kwa kutenda na kutetea haki kuliko kutetea uovu kama unavyofanya
 
Mimi naona kuna umuhimu kuanzisha kikosi kazi kitengo maalumu cha muda wote kuzibiti magenge kama haya sio dar tu magenge haya ya kialifu yapo mikoa yote
 
Hofu ya aliyetoa hii mada ni huenda ambae sio panya road nae akashughulikiwa. Tatizo lipo hapo. Umakini unahitajika. Usifikiri kwamba panya road Wana alama sehemu kwamba inakua rahisi polisi kuwajua. Hapo Kuna mambo ya kutajana na Kuna ambao hawahusiki nao watakuwemo
Nimemuelewa sana, ila kwa meseji ile ya mkuu wa mkoa hata wale waliokuwa wanajiandaa kuwa panya road wataacha. Hawa vijana hawafai, panga likinyanyuliwa halirudi....

Mimi naunga mkono kauli ya mkuu wa mkoa, ingawa polisi wawe makini, wazazi tudhibiti sana mienendo ya vijana wetu
 
Najua madhara wanaosababisha hao mapanyarodi, lakini hivi kweli hayo maneno yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa, Amos Makala, unadhani ndiyo ufumbuzi wa kuwakomesha hao madogo wasiendelee kuwepo?
Kutokomeza ni ngumu, maana miaka ya nyuma kulikuwa na commando yoso. Hawa hutakiwi ku deal nao kichungaji, inatakiwa ku deal nao kidunia. Wazazi ndo tuanze na kudeal na watoto wetu kiroho, tukishindwa ulimwengu utawafunza.

Najua kwenye huu mtego hata wasiohusika watanasa, lakini vyombo vya ulinzi viwe makini kwenye ku deal na hawa vijana.

Hali ni tete, sikia tu kwa mwenzio... Watu wanalia kama watoto wakipigwa na watoto wao... Miaka 14 hadi miaka 19 wanafunga mtoto
 
Ni kwanini Jeshi letu la Polisi, pamoja na nguvu Kazi waliyo nayo na vifaa vya kisasa vya kutambua wahalifu, washindwe kuwatambua hao vijana wadogo, ambao wanatumia silaha za jadi, kama mapanga pekee?
Polisi wetu Hawa ninavowafahamu huwa huwa hawapendi kufanya vitu ambavyo havina maslahi anajua kabisa akimkamata panya hatokuwa na hela ya kumuhonga ndio mana huwa wanaangalia sehemu zenye madili
 
Back
Top Bottom