balibabambonahi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2015
- 15,771
- 14,294
Hata wakishikishwa ukuta bado wanaume wa dar watabaki wanaume wa dar.Wala chips,soseji,miguu ya kuku na shingo na utumbo wa kuku.Mnasubiri watoto wadogo washikishwe adabu na polisi.Kazi na nguvu zenu zilikwina?Ila madogo acha washikishwe adabu, maana ndo tunaitwa wanaume wa Dar.
Ndiyo maana nikasema hao Polisi wanapashwa kufanya Kazi kwa kufuata Weledi.Hao vijana wanatoka sayari ya Mars?
Jamii ya kihalifu huzalisha jamii ya kihalifu...
Wana intelijensia ya kudhibiti wapinzani tu sio wahalifuNi kwanini Jeshi letu la Polisi, pamoja na nguvu Kazi waliyo nayo na vifaa vya kisasa vya kutambua wahalifu, washindwe kuwatambua hao vijana wadogo, ambao wanatumia silaha za jadi, kama mapanga pekee?
Una ndugu, hiyo sakua sakua haibagui na haina Haki,Ila madogo acha washikishwe adabu, maana ndo tunaitwa wanaume wa Dar.
Ina maana huwaamini polisi mpaka uanzishe vikosi mbadala?...Mimi naona kuna umuhimu kuanzisha kikosi kazi kitengo maalumu cha muda wote kuzibiti magenge kama haya sio dar tu magenge haya ya kialifu yapo mikoa yote
Mimi nionavyo mkuu wa mkoa yuko sahihi, Sasa unavyotaka wewe Ikiwa mwanao kapotea hajarudi nyumbani siku moja au mbili simu humpati sasa ufanye nini kama sï kwenda kuripoti polisi au kwenda kutafuta hospitali kama unatafauti na mkuu wa mkoa tuambie tu.Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu...
Better do in whatever way, ila wamezidi.Una ndugu, hiyo sakua sakua haibagui na haina Haki,
Na wewe utuambie kama ni sahihi kwa wazazi wa Dar es salaam kuwaacha watoto wao bila malezi mazuri na kutuzalishia kundi la watukutu linalopora na kuua raia jijini ?Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu.
Najua Mkuu wa Mkoa, ametoa kauli hiyo kuhusiana na kukerwa na vitendo vya vijana wadogo, wanaofahamika kwa jina la Panyaroad, kwa vitendo vyao vya kuvunja nyumba za wakazi wa jiji la Dar, kufanya wizi wa vitu mbalimbali, kujeruhi hadi kusababisha vifo, kama ilivyotokea hapo majuzi huko Kawe.
Lakini nijaribu kumuuliza Mkuu wa Mkoa wa Dar, hivi yeye anadhani kwa kutumia vitisho hivyo, ndiyo atakuwa amepata ufumbuzi wa vitendo hivyo vya Panyaroad?
Hivi anajua "impact" ya kuyatamka maneno hayo hadharani, akiwa ndiye Mwenyekiti, wa Kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa huo wa Dar?
Nimuulize tena Mkuu wa Mkoa, hivi anajua kwa kuyatamka hayo maneno, ni kama ametoa "blessings" zake kwa Polisi wetu, waweze kujeruhi na hata kuua hao wanaoitwa Panyaroad, bila kwanza kuwahoji na kupata ushahidi wa hao wahalifu?
Hivi yeye Mkuu wa Mkoa, anatambua kuwa kwa tamko hilo anakiuka misingi ya Haki za binadamu?
Ninaposema hivyo, siyo kuwa naunga mkono vitendo hivyo vya kinyama vya hao wanaojiita Panyaroad, la hasha, nia yangu ni kulitaka Jeshi la Polisi, litende Kazi zake kwa Weledi mkubwa, kwa kufuata sheria.
Polisi wetu wanafahamu kuwa Hawama mamlaka ya kuua raia yeyote bila msingi wowote.
Tunafahamu pia kuwa Katika nchi yetu, ni mhimili wa Mahakama pekee, uliopewa mamlaka ya kumtia hatiani raia yeyote na kutoa hukumu.
Nchi hii inaendeshwa kwa kufuata misingi ya kisheria.
Hivi anaweza kutuambia kwa kuyatamka hayo maneno, ni sheria gani inayomruhusu yeye kama Mkuu wa Mkoa, aliagize Jeshi lake la Polisi, litekeleze majukumu yake, pasipo kuzingatia sheria za nchi hii?
Kwa hiyo Mkuu wa Mkoa, Amos Makala, anapaswa aombe radhi kwa wakazi wa Mkoa wa Dar, kwa matamshi aliyoyatoa, ambayo ni kinyume cha utawala bora, unaozingatia sheria.
Najua ulichokisema ni sahihi kabisa.Mimi nionavyo mkuu wa mkoa yuko sahihi, Sasa unavyotaka wewe Ikiwa mwanao kapotea hajarudi nyumbani siku moja au mbili simu humpati sasa ufanye nini kama sï kwenda kuripoti polisi au kwenda kutafuta hospitali kama unatafauti na mkuu wa mkoa tuambie tu.
Ulitaka asemeje?Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu.
Hawa syo wa kuonewa huruma kbsHuyo labda kama hajakutana na hao panya road. Nipo hapa nauguza majeraha na nimechukuliwa vitu. Acha washughulikiwe.
SASA kawe Ndio viongozi wanakaa na kuna kambi za jeshi na wameenda kufanya matukio ni hatari sanaNi kwanini Jeshi letu la Polisi, pamoja na nguvu Kazi waliyo nayo na vifaa vya kisasa vya kutambua wahalifu, washindwe kuwatambua hao vijana wadogo, ambao wanatumia silaha za jadi, kama mapanga pekee?
Hao vijana wa panya road hawakuleta mbwembwe awamu ya Tano walijua wanacheza na kifo Sasa ivi wanapetiwa patiwa na mamlaka na nyinyi haki za binadamu,natamani siku wakubane kwenye Kona na Panga la kukukata bega kisha ulete haki za binadamu,tuchangie.Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu....
UlimakafuKauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu...
Tatizo mkuu wa nchi wa sasa haijui vizuri hii nchi. Anadhani JPM alikuwa katili ilihali alijitahidi kukomesha uhalifu na wahalifu kwa kushirikiana na kamanda Siro!Hao vijana wa panya road hawakuleta mbwembwe awamu ya Tano walijua wanacheza na kifo Sasa ivi wanapetiwa patiwa na mamlaka na nyinyi haki za binadamu,natamani siku wakubane kwenye Kona na Panga la kukukata bega kisha ulete haki za binadamu,tuchangie.